Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Kwa muda nimeungana na waandishi wengine katika kukemea mauaji ya Watanzania wenye matatizo ya kijenetiki ya upungufu wa rangi (Albino). Wapo watu wengi na vikundi vingine ambavyo vinashirika katika harakati za kupiga vita na hatimaye kukomesha mara moja na daima aibu hii ya Taifa letu na vitendo hivi vya kinyama dhidi ya binadamu wenzetu.
Kwa muda nimekuwa nikizungumza na watu mbalimbali nyumbani na wengine nao wamekuwa wakifanya hivyo. Hatimaye kundi hili la watu mbalimbali ambao wote tumeguswa na vitendo hivi tumeamua kuunganisha nguvu zetu, vipaji vyetu, na resources zetu kufanya kitu ambacho kitakuwa ni cha kihistoria.
Baadaye mwezi ujao taasisi kadhaa zisizo za kiserikali kutoka US na Canada na zilizoko Tanzania zikiongozwa na Chama cha Maalbino Tanzania zimeandaa safari maalumu ya kuonesha mshikamano na ndugu zetu Maalbino wa Tanzania kwa kutumia elimu na pia kutoa misaada mbalimbali ili kufanya maisha yao yawe ya amani, utu na usalama zaidi. Katika kufanya hivyo:
Kuna petition ambayo ilianzishwa na Mtanzania mwenzetu Pius Pius Mikongoti na taasisi ya "Under the Same Sun" kuichukua na kuifanya ya Kimataifa. Nimezungumza na baadhi ya viongozi wa taasisi hizo na natarajia weekend hii kufanya mazungumzo zaidi na kutoa kila ya msaada uliomo katika uwezo wangu kuweza kufanya trip hii kuwa muhimu.
Ninachoomba kwa leo ni kitu kimoja cha pili nitasema tukikamilisha mazungumzo na kundi tunaloenda nalo nyumbani kwenye tripu hii ya kihistoria. Ninachoomba leo ni kuwa tembelea site ya UNDER THE SAME SUN na utie sahihi Petition ukionesha kukubaliana na mambo yafuatayo. Orodha hii inatarajiwa kukabidhiwa kwenye tripu hii kwa viongozi wa serikali (bado hatujajua for sure nani atakuwepo nyumbani kuipokea):
- Declaring my support for and solidarity with persons with albinism living in Tanzania during this time of dire crisis within the albinism commmunity.
- Reminding persons within the Tanzanian albinism community that they are NOT ALONE and that many throughout the world are standing with them in defense of their fundamental human right to safety, security and freedom.
- Calling on the Government of Tanzania to ensure that the 173 detainees presently in custody as suspects in the savage murders of at least 28 albinos during the last 18 months be brought before the courts and that those found guilty be prosecuted to the fullest extent of the law.
- Asking that the Government of Tanzania provides resources to the albinism community in terms of public education and protection with the goal to reduce the crippling discrimination albinos experience in their schools and communities.
Tafadhali usitoe thanks kwa post hii; ila kama unaona ina maana tia sahihi petition! And if you really care, usisite kuituma kwenye mailing list yako au kwa wabongo wengine. We need to make this OUR (Tanzanians) campain na hawa ndugu zetu toka US na Canada wamekuja kutuunga mkono. Can we do that?