Mkuu DALLAI LAMA mtu akidai haki yake basi anakuwa anatumika? Hii kitu kwa Dr. Slaa inaonekana kuwa janga. Mahimbo anatumika, Rose Kamili anatumika!
Mkuu kabla ya kuendelea na hizi 'brouhaha' ambazo ninaamini kwa 100% kuwa zina mkono wa CCM wakidhani ni karata ya kuiangushia CDM, mtueleze kwanza ile kesi aliyofungua Mahimbo wakati wa uchaguzi mwaka 2010 kwa msukumo wa Rajab Makamba na kundi lake iliishia wapi?. Je zile hela walizompatia wakati ule zimeishia? wamemuahidi nyingine?.
Hivi tukianza hasa kuchambua maisha binafsi ya viongozi wa CCM na mawaziri kuna mtu atabaki salama. Si bora Dr slaa yeye ameweka wazi uhusiano wake na Josephine na kuamua kufunga ndoa kuliko wale wanaochukua vibinti vya vyuoni na hata kuwapatia madaraka wake za watu na kuwafanya nyumba ndogo zao?.
Hizi ni politics ambazo CCM will be the biggest loser, maana wananchi wanawafahamu na kuwajua viongozi wote wa CCM vizuri sana linapokuja suala la infidelities.