90 Minutes in raid on Entebbe: Tukio la ukombozi wa mateka wa Israel Nchini Uganda - THUNDERBOLT

donlucchese

JF-Expert Member
Mar 23, 2011
17,047
21,522
Operation Entebbe was a counter-terrorist hostage-rescue mission carried out by commandos of the Israel Defense Forces (IDF) at Entebbe Airport in Uganda on 4 July 1976. A week earlier, on 27 June, an Air France plane with 248 passengers was hijacked, by members of the Popular Front for the Liberation of Palestine and the German Revolutionary Cells, and flown to Entebbe, the main airport of Uganda.

The local government supported the hijackers and dictator Idi Amin personally welcomed them. Sasa hapo ndipo kilinuka baada ya israel kutuma makomandoo wao kuja kupiga moja ya greatest hostage rescue in the history.

Hii hapa documentary inayoelezea bayana nini kilichojiri katika operation hiyo:



Jenerali Idd Amin Aliporatibu Ugaidi Wa Kimataifa Akiwa Kampala..( Uchambuzi)
Ndugu zangu, Waziri Mkuu wa Israel , Benjamin Netanyahu ametua leo uwanja wa ndege wa Entebbe.

Netanyahu yuko Kampala Uganda kushiriki kusanyiko la wakuu wa nchi saba za Afrika kujadili masuala ya usalama ikiwamo mapambano dhidi ya ugaidi. Ni kwenye uwanja wa Entebbe, takribani miongo minne iliyopita, kaka yake Benjamin Netanyahu, aliuawa mahali hapo. Ni kwa nini?

Nitakumbushia hapa, tukio la utekaji wa ndege ya abiria ya Ufaransa iliyokuwa na abiria wengi wa Kiyahudi. Na mmoja wa wahusika wakuu katika tukio hili la kigaidi alikuwa Jenerali Idd Amin Dadah wa Uganda.

Ndio, licha ya Jenerali Idd Amin kuendesha ugaidi wa dola kwa maana ya State Terrorism, kwenye tukio hili, Jenerali Idd Amin alishiriki rasmi kwenye Ugaidi wa Kimataifa. Maana, tukio lile la utekaji ndege lilianzia Ulaya, likaambaa Mashariki ya Kati na kumalizikia kwenye ardhi ya Uganda. Ni kwenye uwanja wa ndege wa Entebbe huku Idd Amin mwenyewe akishiriki kuratibu harakati za kigaidi.

Maelezo marefu juu ya sakata ya Entebbe yanasimuliwa kwa umahiri mkubwa na mwandishi William Stevensson katika kitabu chake cha (90 Minutes At Entebbe), Yaani Dakika 90 katika Entebbe.

Ndege hiyo ilitekwa nyara Juni 27, 1976 mara ilipoanza kurukakutoka uwanja wa ndege wa Athens nchini Ugiriki kuelekea Tel Aviv. Miongoni mwa watekaji nyara, walikuwemo Wapalestina, lakini raia mmoja wa Ujerumani naye alishiriki utekaji huo. Mjerumani huyo alikuwa ni mfuasi wa kikundi cha kigaidi cha Ujerumani kulichojulikana kama ”Baader-Meinhof.”

Inasadikiwa, kuwa Dr. Wadi Hadad, mwanaharakati na Kiongozi wa chama cha ukombozi wa Wapalestina cha PFLP (Popular front For Liberation of Palestene) alishiriki kwenye kupanga kazi hii ya kigaidi. Bila shaka, inaaminiwa pia, kuwa aliyekuwa gaidi nambari moja wakati huo, Ramirez Carlos, ambaye pia alijulikana kama ”The Jackal”, alikuwa na mkono wake kwenye kazi hiyo.

Baada ya kutua na kujaza mafuta Tripoli , Libya, ndege hiyo iliendelea hadi Uganda na kutua Entebbe.

Wakati huo Idd Amin alishakorofishana na maswahiba wake Waisrael na kutangaza kuunga mkono harakati za
Wapalestina kuikomboa nchi yao. Kuna wakati, Idd Amin alishawahi kutamka, kuwa anawaandaa askari wake kwenda kushiriki mapambano ya kuwandoa Wayahudi kwenye milima ya Golan waliyoiteka toka kwa Wapalestina. Na Idd Amin alishaviamrisha vikosi vyake kufanya mazoezi ya kivita kujiandaa na operesheni ya kuikomboa milima ya Golan.

Naam, ndege ilipotua Entebbe, abiria wote walikaribishwa na Idd Amin mwenyewe. Siku mbili baadae, watekaji nyara walianza kutoa madai yao; walidai mateka wangeachiwa huru kama idadi kubwa ya wafuasi wa vikundi kadhaa vya kigaidi wangeachiwa huru kutoka kwenye magereza ya Ulaya na hata Afrika.

Ni katika tukio hili la utekaji nyara ndege ambapo kwa kiasi fulani mateka walihisi kuwepo kwa tumaini la kukombolewa. Ni kwa vile maofisa wengi wa jeshi la Israel wamefanya kazi Uganda ikiwemo kutoa mafunzo ya kijeshi. Na kama kuna watu duniani waliokuwa wakimjua vema Idd Amin ikiwemo uwezo wa jeshi lake, basi, watu hao ni Waisrael. Maofisa wengi katika jeshi la Idd Amin walipata mafunzo yao ya kijeshi Israel.

Kabla ya operesheni hiyo iliyopewa jina la Thunderbolt kuanza, Mossad, Shirika la Ujasusi la Israel, liliamua kumtumia Jenerali wake mstaafu aliyeitwa Chaim Bal Lev. Bwana huyu alikuwa ni rafiki mkubwa na wa siku nyingi wa Jenerali Idd Amin. Wawili hawa walifanya mazungumzo ya muda mrefu na ya kirafiki kwa kutumia simu. Waliongea karibu siku zote kabla ya mateka kuokolewa.

Kwa kumtumia Jenerali huyu rafiki wa Amin, Waisrael walikuwa wanaiba muda ili kujiandaa zaidi, na vile vile kujaribu kumshawishi Amin asiwadhuru mateka hao na pengine kuwaachia huru. Hata kama majasusi ya Kiyahudi walikuwa na michoro yote ya uwanja wa Entebbe ambao waliuchora wenyewe na kuujenga, lakini, kazi ya vikosi vya Israel kutua Entebbe haikuwa rahisi sana.

Hawakuwa na hakika ya ukubwa wa vikosi vya Amin uwanjani hapo. Walitegemea zaidi, ufahamu wao wa uwanja wa ndege wa Entebbe. Maana, ni Waisrael waliojenga uwanja huo. Kutoka Tel- Aviv hadi Entebbe ni mwendo wa takribani saa nne kwa ndege.

Uganda na Israel wamekuwa na mahusiano mazuri ya muda mrefu. Mahusiano hayo yangalipo hadi hii leo. Ni kutokana na sababu za kihistoria. Kabla ya Jumuiya ya Kimataifa kupendekeza makazi ya Wayahudi waliokuwa wametapakaa dunia nzima yawe katika Israel ya sasa, nchi ya Wapalestina, kulikuwepo na wazo la Wayahudi kutafutiwa makazi mapya katika nchi ya Uganda. Mpaka miaka ya karibuni, nchi pekee ya Kiafrika ambapo raia wa Israel hakuhitaji kuomba viza ni Uganda. Raia wa Uganda pia hawakuhitaji pia kuomba viza ya kuingia Israel.

Tukirudi kwenye tukio lile la utekaji ndege. Kwa haraka, Waisrael waliendesha operesheni ambayo si rahisi kusadikika. Makomandoo wa Israel waliruka kwa ndege kubwa kutoka Tel-Aviv kuelekea Entebbe. Ndege yao ilitua saa sita na dakika moja usiku kwenye pembe ya mbali ya Uwanja wa Entebbe. Taa za ndani na nje ya dege lile kubwa zilizimwa wakati ndege ilipoukaribia uwanja wa Entebbe ikiwa na mwungurumo dhaifu. Mwungurumo usiosikika kwa mbali.

Waisarel walikuja na ndege mbili, moja ilibaki Nairobi ikiwa na vifaa vya tiba na vingine muhimu. Iliyotua Entebbe ilibeba gari mbili, Landrover na Mercedes Benz nyeusi. Gari hizo zilitumiwa na makomandoo wa Kiyahudi kufika kwenye jengo walilokuwamo mateka. Waliwakuta mateka wote na wateka nyara wakiwa katika ukumbi wa mapunziko kwa abiria.

Amri ilitolewa kwa lugha ya Ki-hebrenia ikiwataka Wayahudi wote wajilaze chini mara moja. Wote waliobaki wamesimama au kuinama kwa kusitasita, hawakupata sekunde zaidi za kutafakari. Risasi za makomandoo wale ziliwamiminikia miilini mwao.

Operesheni ya kikomandoo iliyochukua takribani dakika tisini pale Entebbe iliwaacha watekaji nyara saba bila uhai. Idadi ya askari wa Amin takribani ishirini nao waliuawa pale Entebbe. Mateka wotewalikombolewa isipokuwa mama wa miaka 75 Dora Bloch aliyekuwa hospitalini Mulago, Kampala.

Inasemekana, kuwa mateka huyo akaja kuuawa na Idd Amin mwenyewe.Habari hiyo haijathibitishwa.

Kwa upande wao, Makomandoo wale wa Kiisrael walimpoteza Kanali Yoni Netanyahu. Komandoo yule aliuawa kwa kupigwa risasi ya usoni na askari mmoja wa Idd Amin. Miaka ishirini baadae, kaka wa Yoni Netanyahu akaja kuwa Waziri Mkuu wa Israel na ambaye ni Waziri Mkuu wa Israel wa sasa, jina lake ni Benjamin Netanyahu, ambaye leo ametua Entebbe Airport.
Huu ni Uchambuzi Endelevu..

Imeandikwa na Josephat Keraryo Nyambeya

AMBATANA NA MIMI

Oparesheni Entebbe ni operesheni ya kuokoa mateka wa Kisrael waliotekwa na magaidi , oparesheni hii ilifanywa na makomando wa Israel (IDF) katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Entebbe tarehe 4 July 1976, wiki moja kabla yaani tarehe 27 June ndege ya shirika la Air France ikiwa na abiria 248 ilitekwa na wanachama wawili wa chama cha vuguvugu a ukombozi wa Palestina (PFLP-EO) baada ya amri ya mtu aliyefahamika kama Wadie Haddad, pia katika utekaji huo kulikuwa na wanachama wawili wa vuguvugu za kimapinduzi huko Ujerumani.

Watekaji walikuwa wanadai Israel iwaachie huru wafungwa 40 na wengine 13 waliokuwa wamefungwa kwenye magereza mbalimbali nchini humo ili iwaachie mateka hao. Ndege hiyo iliyoanzia safari yake mjini Tel-Aviv nchini Israel ikiwa inatarajiwa kutua jijini Paris-Ufaransa ilibadilishwa uelekeo na kushuka jijini Athens-Ugiriki kwa ajili ya kujaza mafuta kabla haijapaa kuelekea Benghazi-Libya kasha Entebbe uwanja mkuu wa ndege nchini Uganda.

Serikali ya Uganda ilikuwa inawasapoti watekaji hao, na binafsi dikteta Idd Amin aliwakaribisha watekaji hao (huyu Idd Amin akili zake zilimtosha mwenyewe). Baada ya kuwaondoa mateka wote kutoka uwanjani na kuwapeleka kwenye jengo lililokuwa halitumiki hapo uwanjani, watekaji waliwatenganisha Waisrael na wasio Waisrael .

Siku mbili baadae mateka 148 ambao hawakuwa raia wa Israel waliachiwa na kurejea jijini Paris. Raia 94 wa Israel ikiwemo na wafanyakazi 12 wa shirika hilo la ndege waliachwa kama mateka na kutishiwa kuawawa .

Jeshi la Israel (IDF) lilizipata taarifa walizopewa na shirika la Ujasusi la nchi hiyo Mossad juu ya tishio la mateka hao kuuliwa kama Israel haitatii matakwa ya watekaji hao ambayo yalikuwa kuwaachia huru wafungwa wote wa Kipalestina waliokuwa kwenye magereza nchini humo. Kitisho hiki kilipelekea IDF kupanga misheni ya Uokozi, operesheni hii ilipangwa ikiwa ni pamoja na kukabiliana na Mapambano kutoka Jeshi la Uganda maana walijua fika kuwa endapo watafanikiwa kuingia Uwanja wa Entebbe kwa ajili ya uokoaji huo lazima wangekabiliana na upinzani kutoka jeshi la Idd Amini hivyo walijiandaa kwa ajili ya hilo.

Oparesheni ilifanyika usiku , Israel ilichukua ndege iliyobeba makomandoo 100 na kusafiri zaid ya Maili 2500 (Kilomita 4000) kuelekea Uganda kwa ajili ya uokozi. Oparesheni iliyochukua wiki nzima kuiandaa ilipangwa kuchukua dakika tisini tu kukamilika, Mateka 102 waliokolewa , makomando watano wa Israel walijeruhiwa, Kamanda aliyekuwa akiongoza Operesheni hiyo Lt. Kanali Yonathan Netanyahu aliuwawa. Watekaji wote, mateka watatu, na wanajeshi 45 wa jeshi la Uganda waliuliwa . Pia ndege vita 11 za jeshi la Uganda ziliharibiwa.

Opareheni hii iliyopewa jina la fumbo (codename) la Oparesheni Thunderbolt, mara nyingine huitwa oparesheni Yonathan kama kumbukumbu ya Kiongozi aliyeiongoza oparesheni hii. Kiongozi wa oparesheni hii alikuwa kaka mkubwa Benjamin Netanyahu waziri mkuu wa sasa wa Israel.

Katika uwanja wa ndege wa Entebbe watekaji wane waliungana na wenzao wanne wakiwa wanapewa sapoti na Jeshi la Uganda. Idd Amini alikuwa akiwatembelea mateka kila siku na kuwapa maendeleo ya mazungumzo juu ya kile kilichokuwa kikiendelea, na kuwaahidi kuachiwa huru kama maafikiano yatafikiwa. Tarehe 28 siku moja baada ya utekaji watekaji walidai fidia ya dollar Millioni 5 ili waiachie ndege na pia wapalestian 53 waliokuwa wamefungwa kwenye magereza ya Israel wachiiwe huru. Walidai kama madai yao hayatatekelezwa wataanza kuwaua mateka kuanzia tareh 1 July mwaka huo wa 1976.

Wiki hiyo Israel ilijaribu kutumia majukwaa ya kisiasa ili kuwaokoa mateka. Vyanzo vingi vinadai baraza la Mawaziri la Israel lilipanga na kukubaliana kuwaachia wafungwa hao wa Kipalestina ili kuokoa roho za waisrael hao waliotekwa. Burka bar-Lev afisa mstaafu wa jeshi la Israel alikuwa anamjua Idd Amin kwa mda mrefu alipewa jukumu la kumbembeleza Idd Amin ili awaachie mateka hao, Bar-lev alikuwa akimpigia simu mara nyingi Idd Amin kumuomba awaachie mateka bila mafanikio, Idd Amin hakuelewa somo. Israel iliomba Marekani kuongea na rais wa Misri Anwar Sadat aliyekuwa na mahusiano mazuri na Idd Amin kumuomba awaachie mateka bila mafanikio. Sadat alijaribu kuongea na PLO na seriakli ya Uganda , pia Mwenyekiti wa PLO wa kipindi hicho Yasser Arafat alituma ujumbe wake nchini Uganda kuongea na watekaji ila watekaji walikataa katakata kuonana na mjumbe huyo aliyetumwa.

Tarehe ya mwisho ilifika (yaani tarehe 1, July) na hapo baraza la mawaziri la Israel liliomba watekaji kusogeza mda hadi tareh 4 ili waweze kukubalina . Idd Amin pia aliwaomba wasogeze siku hadi tarehe hiyo hadi arudi kutoka kwenye mkutano mkuu wa Umoja wa Afrika (Kipindi hicho OAU) alipokuwa anaenda kukabidi Uenyekiti wa mkuu mwingine wan nchi.

Kukubaliwa kwa ombi hili kuliwafanya Waisrael kujipanga zaidi jinsi ya kuifikia Entebbe. Tarehe 3 July saa 12:30 jioni Baraza la mawaziri la Israel lilibariki kufanyika kwa oparesheni hii, utekelezaji wa Oparesheni hii ukiwasilishwa na Meja Jenerali Yekutiel Kuti Adam na Brigedia Jenerali Dan Shomron mbele ya baraza hilo.

Mwanzoni operesheni ilipangwa kwa kuwadondosha makomando wa Kiyahudi ndani ya ziwa Vicktoria na kuwaacha watumie boti za mipira hadi kwenye ncha ya uwanja wa ndege wa Entebee ulipo pembezoni kabisa mwa Ziwa Vicktoria. Walipanga kuwauwa watekaji wote na kuwaokoa mateka, ila baadae Israel iliukaaa mpango huu kwa sababu ya kuwa walipata taarifa kuwa Ziwa Vicktoria lina mamba wengi hivyo ingekuwa hatari kwa mateka waliokolewa.

Wakati wakipanga oparesheni hiyo walijiuliza watajazia mafuta wapi kwenye ndege yao waliyopanga kuitumia kufika Entebbe, walikosa ndege ya kuweza kufika Entebbe na kurudi Israel bila kujazwa mafuta, hivyo kitu hicho kikawaumiza kichwa tena. Walipanga kuongea na moja ya mataifa ya Afrika ya Mashariki ili kuweza kuwaruhusu kutumia uwanja wao wa ndege kwa ajili ya ndege yao kutua na Kujaza mafuta. Katika kuitafuta nchi ambayo ingewakubalia ombi lao wakaamua kuichagua Kenya na kuwatuma mabalozi wake waliokuwepo nchini Kenya pamoja na wafanyabiashara wa Kiyahudi wenye ushawishi mkubwa nchini Kenya kwenda kuongea na Rais Jomo Kenyatta juu ya ombi lao hilo, msomaji naomba ufahamu kuwa Tanzania haikuwa na uhusiano mzuri na Israel kwa hiyo njia pekee iiyokuwepo ni kuitumia Kenya.

Oparesheni hii isingeweza kufanikiwa bila msaada wan chi yoyote ya Afrika Mashariki, waliotumwa kwa Kenyatta walibubujikwa na machozi ya furaha baada ya ombi lao la kuutumiwa uwanja wa kimataifa wa Jomo Kenyatta kukubaliwa. Kenyatta pia aliwaruhusu MOSSAD kuitumia Kenya kama njia ya kukusanya taarifa za kiintalenjesia.

Mossad ilipata picha kamili ya mahali walipo mateka, idadi ya watekaji pia walizipata taarifa za juu ya uhusikaji wa Jeshi la taifa la Uganda kutoka kwa wale mateka walioachiwa na kurudi Paris (moja ya udhaifu wa watekaji hawa). Taarifa za mateka hao waliochiwa zililisaidia sana Jeshi la Israel na Mossad kujua idadi ya kikosi watakachokituma Entebbe.

Kama bahati ya mtende kuota Jangwani Mossad pia ilipata taarifa za kuwa kuwa Uwanja huo wa ndege wa Enttebe ulijengwa na kampuni moja la Kisrael mnamo mika ya sitini, hivyo iliwasiliana na kampuni hilo liitwalo Solel Boneh na kupata ramani kamli ya uwanja huo na majengo yaliyopo uwanjani hapo.

Kikosi kazi kikiwa na Makomandoo wapatao 100 na silaha nzito nzito walijindaa kuelekea Uganda. Kikosi kazi hizi kiligawanyika katika vitengo vitatu,

Moja, kamandi ya Ardhini iliyoongozwa na Brigedia dan Shomron na muwakilishi wa Kikosi cha anga Kanali Ami Ayalon, kikosi hiki kilikuwa na jukumu moja tu la kuhakikisha ulinzi unaimarishwa uwanjani hapo pamoja na kuyakata mawasiliano yote kutoka uwanjani hapo. Kikosi cha pli kikiongozwa na Kamanda kijana wa miaka 29 tu Luteni Kanali Yonathan Netanyahu kikosi hiki kilikuwa na makomando kutoka kambi ya Sayeret Matkal kilipewa kazi ya kuuteka uwanja wa ndege wa kuingia kwenye terminal na kuwaokoa mateka, Meja Betser alichukua nafasi ya kukiongoza kikosi hiki baada ya Yonathan kuuwawa kwa risasi. Kikosi kazi kingine kilipewa jukumu la kuzilinda njia za Kutulia ndege (runways-siko vizuri Kiswahili mnisamehe) na kulinda sehemu ya kujazia mafuta na kuhakikisha ndege za Israel zinajaza mafuta uwanjani hapo kabla ya kupaa (Yaani hii ni sawa na kuvamiwa na Majambazi ukiwa umelala na mkeo wewe unainamishwa nay eye anainamishwa mbele yako). Kikosi hiki kiliongozwa namakamanda watatu walikouwa na majukumu tofauti, kikosi hiki pia kilipewa jukumu la kuharibu ndege vita zote za jeshi la Uganda zilizokuwepo uwanjani hapo.

Kikosi hiki makini cha makomando wa kiyahudi kilipaa kutoka Sharm el-Sheikh ndege iliyowabeba makamanda hawa ikiwa inaruka umbali wa Mita 30 (futi 100) tu ili kuepuka kunaswa na Rada za Sudan, Misri na Saudi Arabia (kwa wataalamu wa RADAR nadhani watakubaliana na mimi) kilipita bahari ya shamu kuelekea Kusini na kasha kupita Djibouti kutoka huko walitua uwanja wa ndege jijini Nairobi, wakiwa na ndege mbili za Boeing 707 ndege moja ikiwa ikiwa imebeba madawa na vifaa tiba na ndege ya pili kikiwa imewabeba makamanda.

Jeshi la Israel lilitua uwanja wa Entebbe saa tano kamili usiku July 3, ndege ya mizigo ikiwa tayari imefunguliwa milango gari nyeusi aina ya Mercedes Benz iliyofanana na ile aliyokuwa anatembelea rais Idd Amin ilishuka kutoka kwenye ndege ikiwa imeambatana na Land Rovers kadhaa sawa na zile zilizokuwa zinampa Idd Amin eskoti, walizitumia hizi kupita check points zote za uwanjani hapo. Ndege ya pili iliyowabeba makamanda wa kazi ilitua dakika sita baadae na hapo hapo wakayadandia magari hayo kuelekea kwenye jengo walipo mateka wakiwa wanafanana sawa sawa kabisa na Idd Amin, wakiwa wamekaribia terminal ya pili Maaskari waliokuwa guard wakiwa wanatambua kabisa kuwa Idd Amin alikuwa siku chache zilizopita alikuwa kanunua Mercedes nyeupe na kuachana na ile nyeusi walisimamisha msafara huo, makomando hao waliwafiatulia risasi kwa kutumia bastola za sailensa lakini hawakuwaua lakini komando mmoja aliyekuwa kwenye rand Rover za msafara aliwamalizia kwa kutumia bunduki kubwa isiyotoa sauti.

Wakiwa wameingia kwenye jengo lililokuwa linawafuga mateka hawa makomando walipaza sauti kutumia Vipaza sauti wakisema kwa Kingereza na Kiebrania kuwa “KAA CHINI, KAA CHINI” sisi ni wanajeshi wa Israel , kijana wa Kiyahudi wa miaka 19 alijaribu kusimama na alipigwa risasi kwa kudhaniwa kuwa alikuwa mtekaji. Pia mzee wa miaka 52 aliuwawa kimakosa baada ya kujeruhiwa na risasi ya jeshi la nchi yake, pia mateka mmoja mwenye asili ya Urusi aliuuliwa kwa risasi ya watekaji.

Wakiwa wanaendelea na oparesheni hii makamanda wa kiyahudi waliwauliza mateka kwa kiebrania walipo watekaji wengine na waliwaonyesha kwa vidole kuwa watekaji hao wamejificha kwenye chumba kinachofuata, makomandoo walikibomoa chumba hicho kwa magruneti kabla ya kuingia ndani na kuwamiminia risasi watekaji hao wa Kipalestina.

Kipindi wakiendelea a zoezi hilo la uokozi ndege vita tatu aina ya C-130 zilitua uwanjani hapo ili kutoa ulinzi wa anga ikiwa pia na kuzilinda ndege za jeshi la israel zikiwa zinajaza mafuta uwanjani hapo, oparesheni ya kuwaokoa mateka pia ilienenda sambamba na kuziharibu ndege za jeshi la Uganda zilizokuwepo uwanjani hapo.

Wakiwa wanaendelea kuwapakia mateka kwenye ndege zao wanaeshi wa Uganda waliendelea kurusha risasi, wanajeshi hawa wa Uganda wakiwa wanarusha risasi kutoka mnara wa kuongozea ndege walifanikiwa kuwajeruhi makomando watano na kumuua Kiongozi mmoja wa oparesheni Luteni Kanali Yonathan Netanyahu, makomando wa Israel walirusha RPG (wanaojua dhana za kijeshi RPG siyo jina geni kwao) na kuuharibu kabisa mnara huo wa kuongozea ndege, kulingana na mmoja wa vijana wa Idd Amin askari aliyempiga risasi Yonathan Netanyahu aliuliwa katika majibizano hayo ya risasi.

Zoezi hili lilichukuwa dakika 53 pekee japo lilipangwa kuchukua dakika 90. Katika oparesheni hii jumla ya wanajeshi 45 wa Uganda waliuliwa, mateka wote wanane waliuliwa, komando mmoja wa Israel alikufa, pia makomando 5 kujeruhiwa, ndge vita 11 za jeshi la Uganda aina ya Mig-17s na Mig-21 zilliharibiwa, pia kati ya mateka 106 mateka 3 waliuwawa kama nilivyoelezea mwanzoni pia na mateka mmoja kikongwe wa miaka 75 alisahaulika Uganda kikongwe huyu alichukiliwa nakupelekwa hospitali ya taifa ya Uganda-Mulago ambapo aliuliwa na wanajeshi wa Uganda kesho yake akiwa kitandani .

Ni hayo tu kwa leo, sina mengi ya kueleza juu ya oparesheni hii ila hayo kiduchu ninaamini yamekufanya uipate picha juu ya kile kilichotokea miaka 40 iliyopita. Ninaweza nikawa sijaandika kwa mtiririko mzuri ila nadhani hoja yangu imefika na imeeleweka.

Unaweza wasiliana nami kupitia +255653737353 (WhatsApp) au nyambeya@yahoo.com

OPERESHENI ENTEBE/OPERESHENI THUNDERBOLT

Tukio moja la dharura ambalo lilitokea mnamo juni 27 1976, wakati Yitzhak Hofi akiwa ndio kwanza amepokea kijiti cha ukurugenzi wa MOSSAD, ilikuwa ni dharura iliyohitaji suluhu kwa ustadi mkubwa, pamoja na bahati. Vijana mchanganyiko wenye asili ya kiarabu na wengine kijerumani waliteka ndege ya shirika la ndege la ufaransa, Air France Airbus 300. Ndege ilianzia Tel Aviv hadi Athens – Ugiriki, ambapo watekaji waliingia wakijifanya abiria wa kawaida kwa ajii ya safari ya kuelekea Paris, Ufaransa. Kwa kuwa safari ilianzia Tel Aviv, abiria wengi kati ya 248 waliokuwamo walikuwa waisrael.

Watekaji walijitambulisha kama mawakala wa ukombozi wa Palestina,(PLO) kisha wakatoa amri kwa rubani kurusha ndege hadi Entebe, Uganda ambapo dikteta jeuri na katili Idd Amin Dada alikuwa akitawala, naye alikubaliana na kitendo hicho na kuwapokea na kuwahifadhi watekaji. Masharti ya watekaji yalikuwa kuachiwa huru kwa wafungwa 40 wa kipalestina waliofungwa katika jela za Israel, pamoja na wafungwa 13 katika nchi zingine.

Abiria wa ki-israeli pamoja na wayahudi na wahudumu wa ndege waliokuwa waisrael, jumla wakiwa zaidi ya 100 walitenganishwa, kisha abiria waliobaki wapatao 148, raia wa nchi zingine waliachiwa huru pamoja na rubani, wakarudishwa Paris, Ufaransa.

Huko Paris, abiria wale wa nchi zingine walipofika walihojia na mawakala wa intelijensia wa Ufaransa na Israel. Wana-intelijensia walijifunza kadiri ilivyowezekana kuhusu watekaji na mahali walipohifadhiwa wayahudi na raia wengine wa Israel.

Wakati huo, Israel tayari ilikuwa na uhusiano wa siri na utawala wa Jomo Kenyatta wa Kenya. Uhusiano huo ulitengenezwa kwa makubaliano na jasusi David Kimche ambaye alitumia mwanya wa urafiki wa Jomo Kenyatta na mkulima wa kizungu mwenye asili ya Scotland, Bruce McKenzie. Mkulima huyo, Bruce Mckenzie alikuwa mzungu pekee kwenye baraza la Kenyatta, huku akitumiwa na shirika la intelijensia la Israel, MOSSAD. David Kimche aliyefanikisha urafiki huo anatajwa pia kutoa msaada kwa waasi waliopindua serikali ya kisultan ya Zanzibar, mnamo Januari 12 1964.

Kazi yake ya kuzugia katika misheni zake za barani Afrika ilikuwa ‘kujifanya’ mwandishi wa habari wa kiingereza.
Basi kwa ya urafiki huo, Mossad kwa haraka walifika Kenya na kupatiwa msaada wa ndege ya mtu binfasi wa kenya ambayo waliittumia kupita juu ya anga la Entebe na kuchukua picha za maeneo ya mji huo ili kujua pa kuingilia na pa kutokea.

Wiki moja baadae, julai 4 1976, makomandoo wenye sare za kijeshi wa Israel, kikosi maalumu kilichoitwa sayeret Matkal (Scouting Generals) walitekeleza misheni ya kuwakomboa mateka kwa utulivu, ustadi mkubwa na kasi ya ajabu.
Ndege 2 kubwa za mizigo zilitua uwanjani kisha makomandoo 100 wa kiisrael walishuka wakiwa na magari yenye rangi za jeshi la Uganda kisha kuelekea eneo walipo watekaji. Wakati watekaji wakiduwaa na magari yale wakijua ni asjari wa Uganda, walistukia risasi zikimiminwa mfullulizo.

Ndipo majibishano ya risasi yalipoanza huku michezo ya kutafutana na kujificha ikiendelea. Baada ya dakika 90, mateka waliokolewa. Watekaji wote 7 walikufa, askari 45 wa Idd Amin waliuawa na wengi kujeruhiwa. Mateka wanne walipoteza maisha, makomandoo wanne wa Sayeret Matkal walijeruhiwa na mmoja, aliyekuwa kiongozi wa kikosi hiko, Yonathan (Yoni) Netanyau, alifariki kwenye tukio hilo. Ilikuwa ni desturi katika vikundi vyote vya kijeshi na kiintelijensia vya Israel, kwamba kiongozi anakuwa mstari wa mbele katika misheni za hatari, kwanza kwa ajili ya kuwapa nguvu wengine na pia ni namna yao ya kuenzi utamaduni ulio katika simulizi zao za kale.

Yonathan Netanyau alikuwa kaka wa Benjamin (Bibi) Netanyau, waziri mkuu wa sasa wa Israel. Waisrael hawakuwahi kuwa na furaha kubwa kuliko usiku ule wakati ndege za kijeshi zikitua kuwarudisha ndugu zao. Wanadamu wengi, marafiki na maadui walitamani kuwa waisrael usiku ule. Dunia iliitamani Israel kwa kukataa matakwa ya watekaji na kuwaokoa raia wake waliokuwa mateka katika ardhi ya mbali.

Sehemu ya Kitabu; Spies Against Armageddon, by Dan Raviv.
Imetafasiriwa na Christopher Cyrilo.
 
Last edited by a moderator:
Operation Entebbe was a counter-terrorist hostage-rescue mission carried out by commandos of the Israel Defense Forces (IDF) at Entebbe Airport in Uganda on 4 July 1976. A week earlier, on 27 June, an Air France plane with 248 passengers was hijacked, by members of the Popular Front for the Liberation of Palestine and the German Revolutionary Cells, and flown to Entebbe, the main airport of Uganda. The local government supported the hijackers and dictator Idi Amin personally welcomed them. Sasa hapo ndipo kilinuka baada ya israel kutuma makomandoo wao kuja kupiga moja ya greatest hostage rescue in the history. Hii hapa documentary inayoelezea bayana nini kilichojiri katika operation hiyo: <b style="color: rgb(37, 37, 37); font-family: sans-serif; line-height: 19.1875px;">


Impressive and very interesting! These guys are very intelligent!
 
Last edited by a moderator:
The documentary is not saying anything about the mastermind of the whole plan the brave commander Yonatan
Netanyau!
220px-Yoni-candid.jpg
He was the genius of the whole plan. Unfortunately he was killed by a Ugandan sniper who was also killed during the last minutes of the rescue mission!!The whole story is here Lt. Col. Jonathan (Yoni) Netanyahu official memorial web site - The Entebbe Rescue (Jonathan Operation) - Page 2
Operation Entebbe was a counter-terrorist hostage-rescue mission carried out by commandos of the Israel Defense Forces (IDF) at Entebbe Airport in Uganda on 4 July 1976. A week earlier, on 27 June, an Air France plane with 248 passengers was hijacked, by members of the Popular Front for the Liberation of Palestine and the German Revolutionary Cells, and flown to Entebbe, the main airport of Uganda. The local government supported the hijackers and dictator Idi Amin personally welcomed them. Sasa hapo ndipo kilinuka baada ya israel kutuma makomandoo wao kuja kupiga moja ya greatest hostage rescue in the history. Hii hapa documentary inayoelezea bayana nini kilichojiri katika operation hiyo:
 
Last edited by a moderator:
Yeah hii mission ilikuwa ya ukweli sana. Hivi wamarekani washawahi kutekewa ndege wakaenda okoa hostages nchi yoyote? Au waishia kutengeneza movies tu za missions kama hizi?
 
Donluchesse kuna watu unawaumiza sana kwa kuwaonyesha uwezo wa Taifa la Kiyahudi wao wanataka uwasifie Al Shabbab, Osama, Hamas, nk. Ila ukweli utabaki hivyo kua The State of Israel will keep knocking their unrealistic wishes to ashes.

I second you bro!! Long live the State of Israel! The blessed one!!
 
Back
Top Bottom