5TH Anniversary!!!!!!

CharmingLady

JF-Expert Member
Apr 16, 2012
18,250
12,868
Good morning Ladies under Gentlemen (Sosi: Idd Amin)

Natumaini hamjamboni nyote hapa jukwaani, kwa wale wagonjwa nawaombea kwa Mwenyezi Mungu awaponye…….

Napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunifikisha miaka mitano (5) nikiwa hapa kwa Mkoloni, si jambo rahisi kufikisha miaka mitano, kuna ambao walipata redundancy, kuna ambao waliacha kwa mapenzi yao na kuna ambao walitangulia mbele za haki. Ila mimi bado nipo, ni jambo la kushukuru kwa kweli.


Pili napenda kumshukuru Mama yangu mzazi kwa kunitia moyo, asikwambie mtu katika kazi kuna changamoto nyingi sana, isingekuwa mama yangu aisee ningeacha kazi na kurudi Ushagoo kulima. “I LOVE YOU MUMMY” Kama mjuavyo Majungu, wivu, fitina na kijicho ni “Unkwepable” katika kazi. Hivyo basi nilipitia katika kipindi kigumu sana katika hii kazi. Kuna Mtumishi mmoja wa Shetani alitaka kuniharibia, ila kwa mkono ulio hodari wa Mwenyezi Mungu alishindwa na nawaambia yale mabaya yote alikuwa kuwa akinifanyia yalimrudia. Mungu ni mwema na nimeuona mkono wake jamani……….


Tatu napenda kuwashukuru WANAJAMIIFORUM woooote kwa kunitia moyo kwa namna moja ama nyingine, nimekuwa nikisoma post za watu waliopitia changamoto zinazofanana na zangu na jinsi gani wamekuwa wakizikabili. Mmekuwa msaada kwangu kimawazo, pia hata katika kupunguza stress hasa jukwaa la picha na Jokes. Huwa nafarijika sana kwa kupita majukwaa hayo ili kupunguza stress za kazi. Daddy angu watu8 na Mzee Mtambuzi hamkuwa nyuma kunitia moyo, hakika mawazo na ushauri wenu umenijenga sana. Mbarikiwe saaaaaaaana, mnaweza msijue ni kwa namna gani mmenifanya nimekuwa strong katika kazi ila napenda kuwaambia ushauri wenu ni mkubwa sana na sitawasahau.

Mwisho napenda mjumuike name katika kuadhimisha miaka mitano (5) hapa kwa mkoloni….

Humbled……

CL
 
Last edited by a moderator:
images


images


images


To charminglady......
 
Last edited by a moderator:
Wacha mineno mengi.. we taja lokesheni zitakakopigiwa Ndyofu..
Happy 5th Annivessary, Mi mwenzio ndo natarajia kutimiza mwaka mmoja hapo January. Sijui na hapa watanitimua kama hizo sehemu zingine 18 na ushee nilikopitia.
 
Wacha mineno mengi.. we taja lokesheni zitakakopigiwa Ndyofu..
Happy 5th Annivessary, Mi mwenzio ndo natarajia kutimiza mwaka mmoja hapo January. Sijui na hapa watanitimua kama hizo sehemu zingine 18 na ushee nilikopitia.

Ndyofu muhimu aisee.... Thnx much Baba V

Level 8 patahusika saaaaanaaaa!!!!
 
Last edited by a moderator:
Hongera sana charminglady kwa kweli unastahili pongezi kwa kumudu kukabiliana na changamoto za ajira na kusonga mbele.
Kwa miaka mitano tayari umeshapata uzoefu mkubwa hivyo hata ukisema unabadilisha kazi, huo uzoefu utakusaidia. Labda tu ningependa kukushauri kwamba sasa inabidi uongeze kidogo daraja lako la taaluma baada ya kupata uzoefu wa miaka mitano ili uwe kwenye nafasi nzuri ya kupanda kwenye nafasi nyingine ya juu zaidi.

Naamini utakuwa umenielewa...........
 
Last edited by a moderator:
Hongera sana charminglady kwa kweli unastahili pongezi kwa kumudu kukabiliana na changamoto za ajira na kusonga mbele.
Kwa miaka mitano tayari umeshapata uzoefu mkubwa hivyo hata ukisema unabadilisha kazi, huo uzoefu utakusaidia. Labda tu ningependa kukushauri kwamba sasa inabidi uongeze kidogo daraja lako la taaluma baada ya kupata uzoefu wa miaka mitano ili uwe kwenye nafasi nzuri ya kupanda kwenye nafasi nyingine ya juu zaidi.

Naamini utakuwa umenielewa...........

Nashukuru sana Baba Ngina.... labda kwa vile sijataja upande wa mafanikio. Nimefanikiwa kuinvest na kuongeza Asset kadha wa kadha kupitia kazi.... Pamoja na mafanikio ya kiuchumi, sikuwa nyuma upande wa Taaluma. Nimefanikiwa kuongeza madaraja kadhaa upande wa Taaluma kitu ambacho pia namshukuru Mungu. Na sitabweteka kufika hapo nitaendelea mwakani panapo Majaaliwa ya Mwenyezi Mungu...

Asante kwa kuwa beba kwa beba nami!!!
 
Last edited by a moderator:
Hongera sana charminglady kwa kufikisha umri huo ukiwa kwenye ajira
Hongera pia kwa mafaniko ---- pia kitaaluma na kimaisha na ongeza sana juhudi na Mungu akutangulie
Ndyofu zinahusika sana level 8 na rock bottom pale though Fusion panabamba sana Nicas Mtei alinikataza nisije mwanza eti nitaonana na wewe
Msalimie sana watu8
 
Last edited by a moderator:
Nashukuru sana Baba Ngina.... labda kwa vile sijataja upande wa mafanikio. Nimefanikiwa kuinvest na kuongeza Asset kadha wa kadha kupitia kazi.... Pamoja na mafanikio ya kiuchumi, sikuwa nyuma upande wa Taaluma. Nimefanikiwa kuongeza madaraja kadhaa upande wa Taaluma kitu ambacho pia namshukuru Mungu. Na sitabweteka kufika hapo nitaendelea mwakani panapo Majaaliwa ya Mwenyezi Mungu...

Asante kwa kuwa beba kwa beba nami!!!

Haya, chapchap sana tuma nusu bei nikuóngezeemo nawe uendeshamo ka IST.
 
8 Reactions
Reply
Back
Top Bottom