Sajenti
JF-Expert Member
- Apr 24, 2008
- 3,651
- 412
Habari hii nimeisikia leo asubuhi BBC kuwa katika wilaya ya Tarime mkoani Mara kuna wasichana na watoto wa kike 5,000 wakisubiri kufanyiwa tohara a.k.a kukeketwa katika mwezi huu wa Desemba. Kwa mujibu wa mtu mmoja aliyekuwa akihojiwa kuwa tukio hilo ni sherehe kubwa inayofurahiwa na wenyeji wa eneo hilo kiasi kwamba ilifikia hatua kulikuwa na msafara wa magari yakielekea huko kunako "site" na watumiaji wengine wa barabara likiwemo gari la polisi kusimama pembeni kupisha msafara huo???
Hivi hata kama ndio kudumisha mila kwa maoni yangu hiki kitendo si cha kiungwana hata kidogo ukizingatia madhara mbali mbali anayopata msichana wakati na baada ya kutahiriwa achilia mbali kukosa radha halisi anapofanya mapenzi....
Hivi hata kama ndio kudumisha mila kwa maoni yangu hiki kitendo si cha kiungwana hata kidogo ukizingatia madhara mbali mbali anayopata msichana wakati na baada ya kutahiriwa achilia mbali kukosa radha halisi anapofanya mapenzi....