4% ya mapato kwenda Zanzibar kama Hoja ya Muungano

20% inatoka kwenye mapato ya sehemu zipi????

Mapato ya TRA Zanzibar yanachukuliwa na serekali ya SMZ. Ila hayo mapato ya TRA Zanzibar hayazidi hata 20% ya stahiki ambayo SMT wanatakiwa kuilipa SMZ ya gawio la pato la Muungano. Na ndio mana SMZ wanadai hela zao.
 
Sasa hivi tunatawaliwa na wazanzibari,bara hatuna chetu, zamani tulikuwa tunasema Tanganyika imemeza Zanzibar,sasa hivi Zanzibar imemeza Tanganyika,hapo ndoo utamu wa muungano,kutesa kwa zam,mbuzi kamug'ata mchungaji,Tulikuwa na nyerere,mkapa na magufuli,Tulikuwa tunawaamini kusimamia maslahi ya bara lakini Sasa hivi hawapo,naogopa kusema sana lakini wazanzibari kwa Sasa hivi wanaweza kufanya salakasi yoyote wakuwazuwia simuoni.
Hiki ulichoandika hapa ni kituko, kwani Watanzania si ni wamoja? Hayo ni miongoni mwa makubaliano ambayo yapo kikatiba, Rais akitokea bara, Makamo wake atatokea visiwani na Rais akitokea visiwani Makamo wake atatokea bara.
Au ulitaka aje Mholanzi kuwa Rais wetu?
 
Na Tanganyika anakula cha TRA wakati uhalisia ni source ya mapato ya Muungano.
Tanganyika ni kupe wa Muungano na ndio
maana hataki utekelezaji wa akaunti ya pamoja anaogopa kuaibika (amejificha kwenye koti la Muungano)

Sent from my TECNO LC6 using JamiiForums mobile app

Kivipi ebu dadavua hoja yako.... Kwani kati ya Tanganyika na Zanzibar ipi yenye mapato makubwa?!!!
 
Kuna tatizo kwa Rais Samia

Inaonekana kwa kauli zake ni kama alikuwa na ''chuki' fulani na sasa anataka kutekeleza hoja za Wazanzibar na si kero za pande zote za muungano. Hili litamkwamisha sana kwasababu Watanganyika watakapochachamaa itakuwa tabu

1. Kama anataka pesa za 4% na nyingine , Rais Samia pia aeleze Mchango wa Zanzibar ni upi katika muungano?

2. Rais pia aimbie SMZ igharamie wazanzibar pale Bungeni na Wizara na taasisi za muungano kwasababu wanapata mgao wao.

3. Rais aweke wazi kipi cha muungano kipi sicho ili Watananyika nao wawe na fursa zao bila kuingiliwa

Rais Samia atambue ni Rais wa JMT si Mwakilishi wa Wazanzibar na kwamba Zanzibar wana Rais, nani atawaongelea Watanganyika?

Nimefuatilia kauli za Rais Samia ni kama vile amekuja kutekeleza hoja za Wazanzibar, hili litamsumbua sana hasa Watanganyika watakaposema 'enough is enough'. Yeye si Rais wa Zanzibar ni Rais kutoka Zanzibar

Rais Samia ana fursa ya kurudi katika Rasimu ya Warioba ili mambo ya muungano yawe wazi na Zanzibar ipate inachotaka. Tutaendelea kuidai Tanganyika ili nasi tuwe na nafasi ya kuamua masuala yetu

Kuna tatizo na Rais ashauriwe kwa kauli zinazoelekea kule kule tulipotoka '' Ni zamu yetu''

JokaKuu Mag3
Actually ni vyema tungejua mchango wa Zanzibar katika Muungano na vitu vya Muungano na visivyo vya Muungano . Ili ijulikane zipi ni secta za watanganyika tuu na zipi ni za wazanzibar tuu. Hii ni katiba mbovu na imepitwa na wakati.
 
yaani Zanzibar ni nguzo ya utalii Tz? wewe upo tz ya wapi? zanzibar ngi nguzo ya utalii kuliko ngorongoro, serengeti, mikumbi na mbuga zote hizi? akili yako umetupa wapi?
Zanzibar haina kitu chochote cha kuizidi Tanganyika. Wenyewe kwenye utalii ni zile beach hawana kitu kingine. Beaches Tanganyika zipo nyingi Sana kwahiyo ni kuboresha tuu . Mwambao wa bahari kuanzia Tanga mpaka Mtwara . Visiwa na mwambao wa maziwa yote vya na visiwa vyote vya bahari ya Hindi mfano mafia na vya ziwa Nyasa , Tanganyika na ziwa Victorian
 
Ni kweli ulichokiandika.
Kwa muundo huu wa muungano, Zanzibar ni koloni la Tanganyika, hivyo Tanganyika inawajibika kulipia gharama ya kulitunza koloni lake.

Upande wa pili utajiuliza ni kwa vipi Tanganyika inapata faida kwa kuikalia kimabavu Zanzibar? Jibu nitakupa hapa.
1. Sababu za kiusalama. Tanganyika haiwezi kuwa salama ikiwa Zanzibar itakuwa nchi huru. Watu wenye akili wameshanielewa........

2. Uchumi wa Tanganyika kibiashara unategemea sana bandari ya Dar na makusanyo ya kodi kwa bidhaa kutoka nje. Zanzibar ikiwa nchi huru, itakuwa na mamlaka ya kuwa na bandari huru kubwa, ushirika na Oman, China au nchi za mabeberu katika uwekezaji wa kibiashara kama kisiwa huru (mfano wa Dubai) na hapo itaua bandari ya Dar na makusanyo ya kodi kwa bidhaa za nje kwa Tanganyika.

Hizi blah blah za kutaka kujenga bandari Bagamoyo zitahamia ghafla Zanzibar siku chache tu baada ya Zanzibar kuja kuwa nchi huru.
Bandari ya Zanzibar haitaweza kuizidi bandari ya Dar es salaam kwasababu Zanzibar ni kisiwa kidogo Chenye population ndogo ya watu. Tanganyika kuna watu takribani 60 Million Vs 1million Zanzibar na kuna nchi ambazo ni landlocked zinaitegemea Tanganyika. Haitawezekana mzigo uende bandari ya Zanzibar ndio uje bandari ya Dar. Hapo umechemsha.
 
Bandari ya Zanzibar haitaweza kuizidi bandari ya Dar es salaam kwasababu Zanzibar ni kisiwa kidogo Chenye population ndogo ya watu. Tanganyika kuna watu takribani 60 Million Vs 1million Zanzibar na kuna nchi ambazo ni landlocked zinaitegemea Tanganyika. Haitawezekana mzigo uende bandari ya Zanzibar ndio uje bandari ya Dar. Hapo umechemsha.
ulitakiwa kusema, hata kama bandari ya zanzibar itakuwa huru still ni mizigo michache itabebwa pale kwa ndege kama itatakiwa kwenda landlocked countries za africa mashariki na sadc. kama mizigo hiyo itatakiwa kwenda huko lazima itatakiwa kupitia tena bandari ya dsm na itapigwa ushuru vilevile na itabebwa na malori au reli ya bongo vilevile. kwamaana hiyo, Bara ni mdau mkubwa sana wa uchumi wa Zanzibar na katu zenji wasijefikiri watafanikiwa wakijitenga na pengine kuwa adui wa bara. ni mawazo yao ambayo yapo kwenye makaratasi ila kwenye practice watakuja kujutia na hatutawapa nafasi hiyo tena kwasababu na sisi tutakuwa tumeonja utamu mpya.
 
Kuna hoja nimekuta watu wanaongea, ni kuhusu kile ambacho mama amesema waziri wa fedha akakae na mwenzake wajadili na kusuluhisha katika kero za muungano. Ninaupenda sana Muungano,ninauunga mkono. lakini, nilijiuliza kitu kimoja, mimi kama mtu wa bara sitaki tupigwe pia kama wazenji wasivyopenda kupigwa.

1. hivi Zanzibar inachangia kitu gani kwenye kwa Tz bara kinachowastahilisha tuwagawie hiyo asilimia? Bara inafaidika nini toka Zanzibar?

2. Mgao unaoongelewa ni wa misaada toka nje, au ni mapato ya nchi (pato la madini bara, TRA, navitu vyote vya bara)?

3. kama ni mapato ya nchi, kwani TRA haipo Zanzibar ya kikwaokwao?

4. proportion ya wingi wa watu + ukubwa wa eneo vinazingatiwaje wakati wa kugawa pato ya muungano?

5. kwanini marais waliopita walikuwa hawashughulikii hilo jambo, kulikuwa na kitu gani walichokiona? including one of them who was Zanzibari.

6. kwa anayeelewa, naomba anieleweshe hili jambo kwasababu kama vile tu zanji wasivyopenda kupigwa, mimi kama mtu wa bara pia sipendi na sikubali.

Naongea hivi kwasababu watu wanavyoongea mtaani wanaongea kama vile kwasababu mama ni mzanzibar basi wanaona wazanzibar wanaweza kupitisha vitu vingi sana ambavo vilikuwa havipiti kwa awamu za nyuma ambazo nyingi hazikushikwa na rais wa zanzibar.

MWISHO: siongei kwa ubaya, wala kwa unafiki, ila ninaongea kinachoongelewa mitaani. Ninamwamini mama atafanya makubwa. Ila naamini tunatakiwa kuwa na busara ya hali ya juu kwasababu kuna mambo tunaweza kufanya tukifikiri tunajenga muungano kumbe ndio tunauweka kwenye mazingira ya kubomoka kabisa.
Si mlisemaga kuwa watoto wa kike hujali sana wa nyumbani kwao au mi ndo sikuelewa sawasawa nini wajameni!?
 
ulitakiwa kusema, hata kama bandari ya zanzibar itakuwa huru still ni mizigo michache itabebwa pale kwa ndege kama itatakiwa kwenda landlocked countries za africa mashariki na sadc. kama mizigo hiyo itatakiwa kwenda huko lazima itatakiwa kupitia tena bandari ya dsm na itapigwa ushuru vilevile na itabebwa na malori au reli ya bongo vilevile. kwamaana hiyo, Bara ni mdau mkubwa sana wa uchumi wa Zanzibar na katu zenji wasijefikiri watafanikiwa wakijitenga na pengine kuwa adui wa bara. ni mawazo yao ambayo yapo kwenye makaratasi ila kwenye practice watakuja kujutia na hatutawapa nafasi hiyo tena kwasababu na sisi tutakuwa tumeonja utamu mpya.

Mkuu Zenj hawana mipango ya uadui na Bara, Zenj wanadai haki zao, Zenj wanadai uhuru wao. Sasa kudai haki zao na uhuru wao ni uadui ?
 
ulitakiwa kusema, hata kama bandari ya zanzibar itakuwa huru still ni mizigo michache itabebwa pale kwa ndege kama itatakiwa kwenda landlocked countries za africa mashariki na sadc. kama mizigo hiyo itatakiwa kwenda huko lazima itatakiwa kupitia tena bandari ya dsm na itapigwa ushuru vilevile na itabebwa na malori au reli ya bongo vilevile. kwamaana hiyo, Bara ni mdau mkubwa sana wa uchumi wa Zanzibar na katu zenji wasijefikiri watafanikiwa wakijitenga na pengine kuwa adui wa bara. ni mawazo yao ambayo yapo kwenye makaratasi ila kwenye practice watakuja kujutia na hatutawapa nafasi hiyo tena kwasababu na sisi tutakuwa tumeonja utamu mpya.

Mkuu unasahau tu kuwa Kuna Kenya na Msumbuji juu na chini ya bara. Tanganyika akisusa wenziwe watakula.
 
Bandari ya Zanzibar haitaweza kuizidi bandari ya Dar es salaam kwasababu Zanzibar ni kisiwa kidogo Chenye population ndogo ya watu. Tanganyika kuna watu takribani 60 Million Vs 1million Zanzibar na kuna nchi ambazo ni landlocked zinaitegemea Tanganyika. Haitawezekana mzigo uende bandari ya Zanzibar ndio uje bandari ya Dar. Hapo umechemsha.

Mkuu turufu ya Zanzbar kwenye sera za biashara ni free port na free zones, Hiyo watapiga bao tu kivyovyote.
 
Kivipi ebu dadavua hoja yako.... Kwani kati ya Tanganyika na Zanzibar ipi yenye mapato makubwa?!!!
Kwa mujibu wa article of Union Bandari, Customs, Income tax ni Mambo ya Muungano. Kwa maneno mengine ni mali ya Tanzania (si Tanganyika peke yake wala Zanzibar peke yake ni mali ya ushirika).
Kumbuka Muungano huu si wakila kitu,ni baadhi ya Mambo tu.
Hivyo basi yale mambo ambayo si ya ushirika (MUUNGANO), Kila upande ugharamie kivyake vyake isitumie Pato la Ushirika. Pato la Ushirika litumike kwa Mambo ya Ushirika tu mfano ulinzi, Mambo ya ndani, Elimu ya Juu n.k sio kwenye Afya, Kilimo wala barabara na kama hayo yasiyo ya Muungano.
Jibu la hili ni AKAUNTI YA PAMOJA.
Sijui nimeeleweka?
 
Mkuu turufu ya Zanzbar kwenye sera za biashara ni free port na free zones, Hiyo watapiga bao tu kivyovyote.
Bandari ya Zanzibar itawasaidia wazanzibar wao tuu. Haitatusaidia Tanganyika kwasababu Tanganyika ina mwambao mkubwa kuizidi Zanzibar ina strategic zones za kujeng bandari mpya nyingi zaidi from Tanga to Mtwara + mafia Island. wala bandari ya Zanzibar haitawasaidia other landlocked countries especially in Zambia, Malawi, Zimbabwe, Burundi, DRC, Uganda na Rwanda. Ni ngumu kusema mzigo especially raw materials ( especially Mazao, madini , mafuta) uje bandari za Tanganyika ndio ukachukue meli nyingine uende Zanzibar ndio uende western countries au Asia. Lakini pia ukiangalia mizigo ikitoka china au Asia au other western countries uende Kwanza Zanzibar ndio uje Tanganyika halafu uende other landlocked countries. Tanganyika ipo kwenye strategic location. Pia Zanzibar hayo mafuta yanayoongelea ni ndoto za Alinacha hamna kitu kila mwaka mafuta mafuta . Lakini hayachimbwi. Hata ukiangalia kwenye nchi zilizogundulika kuwa na Mafuta Zanzibar/ Tanzania Haipo. Utaona tuu kuna gesi iliyogunduliwa ipo Mtwara na sehemu zingine za Tanganyika na madini mbalimbali yaliyopo Tanganyika tuu. Huruma za Mwl Nyerere kuwasaidia ili Yule mkoloni( sultan) asiweze kurudi Zanzibar ndio ikabidi kuungana na Tanganyika. Sultan alikuja na kuikuta Zanzibar na watu weusi wanaishi akajimilikisha. Ilikuepo ni muhimu apinduliwe aende akatawale huko kwao Oman .
 
Bandari ya Zanzibar itawasaidia wazanzibar wao tuu. Haitatusaidia Tanganyika kwasababu Tanganyika ina mwambao mkubwa kuizidi Zanzibar ina strategic zones za kujeng bandari mpya nyingi zaidi from Tanga to Mtwara + mafia Island. wala bandari ya Zanzibar haitawasaidia other landlocked countries especially in Zambia, Malawi, Zimbabwe, Burundi, DRC, Uganda na Rwanda. Ni ngumu kusema mzigo especially raw materials ( especially Mazao, madini , mafuta) uje bandari za Tanganyika ndio ukachukue meli nyingine uende Zanzibar ndio uende western countries au Asia. Lakini pia ukiangalia mizigo ikitoka china au Asia au other western countries uende Kwanza Zanzibar ndio uje Tanganyika halafu uende other landlocked countries. Tanganyika ipo kwenye strategic location. Pia Zanzibar hayo mafuta yanayoongelea ni ndoto za Alinacha hamna kitu kila mwaka mafuta mafuta . Lakini hayachimbwi. Hata ukiangalia kwenye nchi zilizogundulika kuwa na Mafuta Zanzibar/ Tanzania Haipo. Utaona tuu kuna gesi iliyogunduliwa ipo Mtwara na sehemu zingine za Tanganyika na madini mbalimbali yaliyopo Tanganyika tuu. Huruma za Mwl Nyerere kuwasaidia ili Yule mkoloni( sultan) asiweze kurudi Zanzibar ndio ikabidi kuungana na Tanganyika. Sultan alikuja na kuikuta Zanzibar na watu weusi wanaishi akajimilikisha. Ilikuepo ni muhimu apinduliwe aende akatawale huko kwao Oman .

Mkuu Sultan si mkoloni, Sultan alikua ni Mzanzibari, Nyerere hajawasaidia wazanzibar, na ndio mana Anachukiwa sana Zanzibar. Tatizo kubwa lililokuepo Bara wanaizungumza Zanzibar from their own point of view, Na sio kwa point of view ya Wazanzibari wenyewe.

Unachotakiwa kufahamu, Zanzibar ikiwa huru Kariokoo inazikwa kwenye masuala ya Biashara. kuwa na mwambao mkubwa kwa Bara haiwezi kuiathiri Zanzibar kwenye sera zake za biashara.
 
Mkuu Sultan si mkoloni, Sultan alikua ni Mzanzibari, Nyerere hajawasaidia wazanzibar, na ndio mana Anachukiwa sana Zanzibar. Tatizo kubwa lililokuepo Bara wanaizungumza Zanzibar from their own point of view, Na sio kwa point of view ya Wazanzibari wenyewe.

Unachotakiwa kufahamu, Zanzibar ikiwa huru Kariokoo inazikwa kwenye masuala ya Biashara. kuwa na mwambao mkubwa kwa Bara haiwezi kuiathiri Zanzibar kwenye sera zake za biashara.
Sultan ni mkoloni wa Kwanza alieanzisha biashara ya utumwa Zanzibar. Kwani sultan alikuepo ni mtu mweusi au mtu mwenye asili ya Asia. Alipokuja mzungu alimtawala sultan na watu weusi Kwa pamoja. Sultan alitokea Oman . Sultan wa Oman wa sasa na Yule aliyepinduliwa Zanzibar ni mtu na mdogo wake. Asili Yao ni Oman Zanzibar walikuja tuu. Kwa taarifa yako Hadi maeneo ya mwambao wa kuanzia Mtwara mpaka Tanga ilikuepo ni miliki ya sultan. Hiyo yote iliitwa Zanzibar mzungu alikuja kupunguza mipaka ya Zanzibar je hii ilikuepo ni Mali yake au alijimilikisha tuu. Bila wapemba . Sasa kule Zanzibar wameondoka wamefuata circulation ya pesa inayopatikana Tanganyika. Kule Zanzibar hamna mizunguko wa pesa hata wakiondoka kule znz wataenda kufirisika kwasababu mizunguko upo Tanzania bara.
 
Sultan ni mkoloni wa Kwanza alieanzisha biashara ya utumwa Zanzibar. Kwani sultan alikuepo ni mtu mweusi au mtu mwenye asili ya Asia. Alipokuja mzungu alimtawala sultan na watu weusi Kwa pamoja. Sultan alitokea Oman . Sultan wa Oman wa sasa na Yule aliyepinduliwa Zanzibar ni mtu na mdogo wake. Asili Yao ni Oman Zanzibar walikuja tuu. Kwa taarifa yako Hadi maeneo ya mwambao wa kuanzia Mtwara mpaka Tanga ilikuepo ni miliki ya sultan. Hiyo yote iliitwa Zanzibar mzungu alikuja kupunguza mipaka ya Zanzibar je hii ilikuepo ni Mali yake au alijimilikisha tuu. Bila wapemba . Sasa kule Zanzibar wameondoka wamefuata circulation ya pesa inayopatikana Tanganyika. Kule Zanzibar hamna mizunguko wa pesa hata wakiondoka kule znz wataenda kufirisika kwasababu mizunguko upo Tanzania bara

Kuwa asili ya familia yake ilitokea Oman hakumfanyi yeye kuwa ni mkoloni. Hivi Vice President wa sasa wa TZ nae ni mkoloni? Mana asili yake ni Burundi.

Tatizo kubwa linalowasumbua wabara ni kuiangalia Zanzibar kwa misingi ya kibaguzi. Acha Ubaguzi ndugu
 
kimbunga kinachokuja ni ushahidi tosha kwamba bara ni muhimu sana kwa zanzibar, kwasababu kwa dunia ya leo kuishi kisiwani ni risk sana (angalia ufilipino na japan), huku bara tunawapa ardhi, na visiwa vingi vinapotea over time kila mwaka vinapungua ukubwa kidogokidogo. wanzazibari msitukane mamba wakati hamjavuka mto.
 
Kuna hoja nimekuta watu wanaongea, ni kuhusu kile ambacho mama amesema waziri wa fedha akakae na mwenzake wajadili na kusuluhisha katika kero za muungano. Ninaupenda sana Muungano,ninauunga mkono. lakini, nilijiuliza kitu kimoja, mimi kama mtu wa bara sitaki tupigwe pia kama wazenji wasivyopenda kupigwa.

1. hivi Zanzibar inachangia kitu gani kwenye kwa Tz bara kinachowastahilisha tuwagawie hiyo asilimia? Bara inafaidika nini toka Zanzibar?

2. Mgao unaoongelewa ni wa misaada toka nje, au ni mapato ya nchi (pato la madini bara, TRA, navitu vyote vya bara)?

3. kama ni mapato ya nchi, kwani TRA haipo Zanzibar ya kikwaokwao?

4. proportion ya wingi wa watu + ukubwa wa eneo vinazingatiwaje wakati wa kugawa pato ya muungano?

5. kwanini marais waliopita walikuwa hawashughulikii hilo jambo, kulikuwa na kitu gani walichokiona? including one of them who was Zanzibari.

6. kwa anayeelewa, naomba anieleweshe hili jambo kwasababu kama vile tu zanji wasivyopenda kupigwa, mimi kama mtu wa bara pia sipendi na sikubali.

Naongea hivi kwasababu watu wanavyoongea mtaani wanaongea kama vile kwasababu mama ni mzanzibar basi wanaona wazanzibar wanaweza kupitisha vitu vingi sana ambavo vilikuwa havipiti kwa awamu za nyuma ambazo nyingi hazikushikwa na rais wa zanzibar.

MWISHO: siongei kwa ubaya, wala kwa unafiki, ila ninaongea kinachoongelewa mitaani. Ninamwamini mama atafanya makubwa. Ila naamini tunatakiwa kuwa na busara ya hali ya juu kwasababu kuna mambo tunaweza kufanya tukifikiri tunajenga muungano kumbe ndio tunauweka kwenye mazingira ya kubomoka kabisa.
KAbisa kabisa. NA imepigiwa mstari kabla hata ya kumsahau Nabii na Mfalme wetu. Hili halikubaliki!
 
Back
Top Bottom