4% ya mapato kwenda Zanzibar kama Hoja ya Muungano

Kama ni mzigo, mbona hamuutuwi basi? Wazanzibari wenyewe hatutaki Muungano, na ukivunjika itatangazwa kuwa ni siku ya uhuru ile 1964 itasahauliwa.

Tanganyika na mali zote mlizokuwa nazo lakini mnashindwa kusonga mbele. Ishu sio kuwa na mali, ishu ni je mnajua kutumia izo mali? jibu ni kuwa hamujui.
Sio hawajui tu Bali hata uwezo wa kujua hawana.
 
Ni kweli ulichokiandika.
Kwa muundo huu wa muungano, Zanzibar ni koloni la Tanganyika, hivyo Tanganyika inawajibika kulipia gharama ya kulitunza koloni lake.

Upande wa pili utajiuliza ni kwa vipi Tanganyika inapata faida kwa kuikalia kimabavu Zanzibar? Jibu nitakupa hapa.
1. Sababu za kiusalama. Tanganyika haiwezi kuwa salama ikiwa Zanzibar itakuwa nchi huru. Watu wenye akili wameshanielewa........

2. Uchumi wa Tanganyika kibiashara unategemea sana bandari ya Dar na makusanyo ya kodi kwa bidhaa kutoka nje. Zanzibar ikiwa nchi huru, itakuwa na mamlaka ya kuwa na bandari huru kubwa, ushirika na Oman, China au nchi za mabeberu katika uwekezaji wa kibiashara kama kisiwa huru (mfano wa Dubai) na hapo itaua bandari ya Dar na makusanyo ya kodi kwa bidhaa za nje kwa Tanganyika.

Hizi blah blah za kutaka kujenga bandari Bagamoyo zitahamia ghafla Zanzibar siku chache tu baada ya Zanzibar kuja kuwa nchi huru.

Hiyo sababu namba 1 ilikuwa enzi hizo za cold war si dunia ya leo mtu yuko pentagoni na laptop na kikombe cha capocino anakuletea kombora ukiwa chooni kwako.

Hata Uganda ilikuwa tishio la amani kwa Tanzania kumbuka walifanyiwa nini? Hadi leo tunalipwa fadhila ya bomba la mafuta.
 
Kama ni mzigo, mbona hamuutuwi basi? Wazanzibari wenyewe hatutaki Muungano, na ukivunjika itatangazwa kuwa ni siku ya uhuru ile 1964 itasahauliwa.

Tanganyika na mali zote mlizokuwa nazo lakini mnashindwa kusonga mbele. Ishu sio kuwa na mali, ishu ni je mnajua kutumia izo mali? jibu ni kuwa hamujui.
Wanaibiana wenyewe kwa wenyewe mkuu.

Wamezoea wizi
 
Huu Muungano ni mzigo Kwa Tanganyika Kwa 100% . Kifo cha JPM kimeturudisha nyuma miaka kimaendeleo. JPM Bora angemchaguaga Hussein Mwinyi kuwa vice president wa Tanzania. Kwenye katiba ibadilishwe na iseme akifa rais basi prime minister ndio awe rais. Hapa Tanganyika tunavuja Jasho kwaajili ya kuwanufaisha wazanzibar. Huu ni Muungano mbovu kuwahi kutokea duniani
Huu muungano sisi watanganyika ndo tunaonekana kutawaliwa
 
Wewe unaambiwa Zanzibar wamechangia zaidi ya 60% mchango wa kuanzishwa BOT halafu unasema 4% zanzibar kwa nini wakati Zanzibar ata 50% bado Tanganyika itakuwa wanaionea Zanzibar.,

Halafu Tanganyika wanajisahau sana kwenye hili wanaangalia idadi ya watu wakati Tanganyika walipoungana na zanzibar waliungana kama nchi na nchi.
Wala hawajisahau. Wanajifanya wehu tu
 
Kwahiyo na hili deni letu la taifa la 71tr wao pia wanachangia asilimia ngapi?..au tunagawana nusu kwa nusu.

Kimsingi huu muungano ni pasua kichwa..vizenji tegemezi zaidi ya chawa..bado vinataka pasu huu ni upuuzi.

Leo hii vi zenji vikija huku ni free kwa kila jambo..ila mbara aakienda huko ubaguzi kuanzia akishuka bandarini..mara kitambulisho cha ukaazi..ni ushezi tu...harafu tunajiita watanzania etu tuna muungano.

#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwahiyo na hili deni letu la taifa la 71tr wao pia wanachangia asilimia ngapi?..au tunagawana nusu kwa nusu.
Wazanzibari watakuwa na wajibu wa kuchangia if and only if hilo deni limegharamia mambo ya muungano.
 
Acha uongo, tra ukusanye mapato znz alaf yote yaachwe znz basi itakua tra yenu ya kikundi cha majambazi
Mwambie simtajii siku, lakini siku hiyo ikifika ndani ya kila mwezi, mzigo wa hela unakuwa na Escort unasafirishwa kutoka Zanzibar kupelekwa Airport na kupelekwa Benki Kuu.
 
Naona wengi hawaelewi huu Muungano ulivyo. Muungano si kila kitu cha Serikali kiko kwenye Muungano bali ni makubaliano ya baadhi ya mambo. Kwa uelewa tuyataje hayo mambo hapa
 
TAtizo linakuja wengi hawaelewi kabisa uhalisia wa mambo. wanakwenda kimihemko tu
Yes ila kuna baadhi wanaelewa. Kuna mambo ya muungano na ambayo si ya muungano na kuna kitu kinaitwa akaunti ya pamoja ya fedha ambapo ndio kunatakiwa kuwekwa mapato ya muungano na baada ya matumizi bakaa ndio inapaswa kugawanywa kwa 4.5% kwa visiwani na 95.5% bara
 
Yes ila kuna baadhi wanaelewa. Kuna mambo ya muungano na ambayo si ya muungano na kuna kitu kinaitwa akaunti ya pamoja ya fedha ambapo ndio kunatakiwa kuwekwa mapato ya muungano na baada ya matumizi bakaa ndio inapaswa kugawanywa kwa 4.5% kwa visiwani na 95.5% bara
Hii akaunti bado haijaanzishwa na ndio vice alipewa agizo la kwenda kuanzisha. Inabidi tuyaelewe haya mambo kabla ya kuwa na jazba na kukashifiana. Haya mambo yalipaswa kufundishwa kwenye somo au topiki ya uraia
 
Kuna tatizo kwa Rais Samia

Inaonekana kwa kauli zake ni kama alikuwa na ''chuki' fulani na sasa anataka kutekeleza hoja za Wazanzibar na si kero za pande zote za muungano. Hili litamkwamisha sana kwasababu Watanganyika watakapochachamaa itakuwa tabu

1. Kama anataka pesa za 4% na nyingine , Rais Samia pia aeleze Mchango wa Zanzibar ni upi katika muungano?

2. Rais pia aimbie SMZ igharamie wazanzibar pale Bungeni na Wizara na taasisi za muungano kwasababu wanapata mgao wao.

3. Rais aweke wazi kipi cha muungano kipi sicho ili Watananyika nao wawe na fursa zao bila kuingiliwa

Rais Samia atambue ni Rais wa JMT si Mwakilishi wa Wazanzibar na kwamba Zanzibar wana Rais, nani atawaongelea Watanganyika?

Nimefuatilia kauli za Rais Samia ni kama vile amekuja kutekeleza hoja za Wazanzibar, hili litamsumbua sana hasa Watanganyika watakaposema 'enough is enough'. Yeye si Rais wa Zanzibar ni Rais kutoka Zanzibar

Rais Samia ana fursa ya kurudi katika Rasimu ya Warioba ili mambo ya muungano yawe wazi na Zanzibar ipate inachotaka. Tutaendelea kuidai Tanganyika ili nasi tuwe na nafasi ya kuamua masuala yetu

Kuna tatizo na Rais ashauriwe kwa kauli zinazoelekea kule kule tulipotoka '' Ni zamu yetu''

JokaKuu Mag3
Mkuu wewe ni mtu umejijengea heshima humu jukwaani, si vizuri kuiharibu mwenyewe. Usiendeshwe na ushabiki.

Angalia heshima aliyojijengea Pascal Mayalla na halafu akaiharibu.

1. Rais Mama Samia sio jukumu lake kueleza mchango wa Zanzibar kwenye Muungano ila ni jukumu lake kuhakikisha kila jamii inapata haki yake inayostahili.

2. Rais Mama Samia anajua kwamba wabunge wote wa Zanzibar waliopo bungeni ni Wabunge wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambapo Zanzibar ni Mshirika. Ikisha kuwa tu jambo linalohusu jina Tanzania basi watanganyika wajue kwamba humo kuna haki za Wazanzibari na wala Wazanzibari hawafanyiwi ihsani. Hili ni muhimu lijulikane wala msijitie hamnazo.

3. Si kazi ya Rais Mama Samia Suluhu Hassan kuweka wazi kipi cha muungano na kipi si cha muungano, mkataba upo na Serikali ya Muungano haijataka kuuweka wazi, anachokisimamia mama Samia ni kuhakikisha mkataba unatekelezwa.

4. Rais Mama Samia Suluhu Hassan anajua kwamba yeye ni Rais na Amir jeshi mkuu wa JMT na anapotenda anatenda kwa kuzingatia hilo. Nongwa imekuja tu baada ya yeye kuagiza hili suala lishughulikiwe????

Rais Mama Samia Suluhu Hassan amekuja kutekeleza hoja na kutenda haki kwa Watanzania. Hatosumbuliwa na chochote na hao Watanganyika hawatosema enough is enough kamwe kwa sababu wamekuwa wakiinyonya Zanzibar for years. Besides there is nothing bad for Tanganyikans to say so when it comes about the union.

Ni imani yetu Rais wetu kipenzi Mama yetu Samia Suluhu Hassan atarudisha mchakato wa katiba mpya kwa maslahi ya Tanzania kwa ujumla ili kila upande washirika wa Muungano wapate wanachostahili. Angalizo: Watanganyika kamwe hajawahi kuidai Tanganyika yao kwahiyo hakuna suala la "tutaendelea kuidai"

Once again, umejijengea heshima hapa jukwaani kwahiyo ni bora kuilinda.
 
Umedadavua vizuri mkuu, je wabunge kutoka Zanzibar wanafanya nini Dodoma nisaidie tujue faida zao kwa bara.
Wabunge kutoka Zanzibar wapo pale kujadili mambo yote ya kibunge yanayohusu Muungano.
Wapo kwa ajili ya kuwawakilisha Wazanzibari kwenye Muungano
 
1. Rais Mama Samia sio jukumu lake kueleza mchango wa Zanzibar kwenye Muungano ila ni jukumu lake kuhakikisha kila jamii inapata haki yake inayostahili.
Hapana si kweli! kama tutakubaliana nawe basi useme kuwa ni wajibu wake kusimamia uwajibikaji wa pande zote mbili katika muungano. Haiwezekani kusimamia haki ya mapato bila kusimamia haki ya mchango na madeni.
Hapa ndipo penye tatizo, kwamba, muungano si kapu la kutoa! ni kapu la kuweka pia
2. Rais Mama Samia anajua kwamba wabunge wote wa Zanzibar waliopo bungeni ni Wabunge wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambapo Zanzibar ni Mshirika. Ikisha kuwa tu jambo linalohusu jina Tanzania basi watanganyika wajue kwamba humo kuna haki za Wazanzibari na wala Wazanzibari hawafanyiwi ihsani. Hili ni muhimu lijulikane wala msijitie hamnazo.
Hao wabunge wanakuja Dodoma kwa gharama za SMZ au za JMT ambayo ni Tanganyika? Hapa uelewe muungano ni kuwajibika si jina. Huwezi kuongelea haki bila kuongelea haki ya kuchangia na haki ya kulipa madeni.
Wazanzibar wanafanyiwa hisani kwasababu pale Bungeni wanajadili TAMISEMI , Wizara ya Afya, Elimu, Mifugo, maji na mawasiliano kwa sababu gani. Ni hisani kwasababu mchango wa Zanzibar upo wapi ukiachilia jina?
3. Si kazi ya Rais Mama Samia Suluhu Hassan kuweka wazi kipi cha muungano na kipi si cha muungano, mkataba upo na Serikali ya Muungano haijataka kuuweka wazi, anachokisimamia mama Samia ni kuhakikisha mkataba unatekelezwa.
Mkataba upi ambao umesema haujawekwa wazi?
4. Rais Mama Samia Suluhu Hassan anajua kwamba yeye ni Rais na Amir jeshi mkuu wa JMT na anapotenda anatenda kwa kuzingatia hilo. Nongwa imekuja tu baada ya yeye kuagiza hili suala lishughulikiwe????
Hapana! suala la muungano ni la kitaasisi na lishughulikiwe kitaasisi. Suala la muungano si kero za Wazanzibar ni matatizo yanayohusu Tanganyika pia ndani ya muungano hasa kubeba gharama peke yake
Rais Mama Samia Suluhu Hassan amekuja kutekeleza hoja na kutenda haki kwa Watanzania.
Tunamuombea kwa mwenyezi mung amfanyie wepesi na kumuonyesha njia
Hatosumbuliwa na chochote na hao Watanganyika hawatosema enough is enough kamwe kwa sababu wamekuwa wakiinyonya Zanzibar for years. Besides there is nothing bad for Tanganyikans to say so when it comes about the union.
Sijui una maana gani maana kwangu mimi kiingereza kinanisumbua kidogo
Ni imani yetu Rais wetu kipenzi Mama yetu Samia Suluhu Hassan atarudisha mchakato wa katiba mpya kwa maslahi ya Tanzania kwa ujumla ili kila upande washirika wa Muungano wapate wanachostahili.
Hasa na kila mshirika abebe majukumu yake na ya muungano. Ushirika uwe wa kubebana si kubebwa
Angalizo: Watanganyika kamwe hajawahi kuidai Tanganyika yao kwahiyo hakuna suala la "tutaendelea kuidai"
OK! unakumbuka G55
 
Back
Top Bottom