2016 US Elections - Exlusive discussion thread

Kuna watu wanaamini tokea mwanzo alikuwa ni pandikizi la Hillary ili bi mkubwa awe na mteremko.

We mwenyewe hebu jiulize tu...mgombea gani wa urais tena wa taifa bora zaidi na la muhimu zaidi duniani ana behave namna ile?

Mtu anakejeli walemavu...anashinda kwenye social media hadi usiku wa manane...anakashifu kila mtu hadi marais wa zamani wa chama chake....

Huyo ni mtu aliye serious kweli? Ni mtu anayetaka kuchaguliwa kuongoza Marekani kweli?

Binafsi siamini kama ni pandikizi. Huwa siko mtu wa conspiracy theories.

Lakini tabia za Trump kwa kweli zinashangaza.

Na mimi tokea hata kabla hajatangaza kugombea nilishasema kuwa jamaa hayuko serious kabisa.

Trump hautaki urais
 
Kuna watu wanaamini tokea mwanzo alikuwa ni pandikizi la Hillary ili bi mkubwa awe na mteremko.

We mwenyewe hebu jiulize tu...mgombea gani wa urais tena wa taifa bora zaidi na la muhimu zaidi duniani ana behave namna ile?

Mtu anakejeli walemavu...anashinda kwenye social media hadi usiku wa manane...anakashifu kila mtu hadi marais wa zamani wa chama chake....

Huyo ni mtu aliye serious kweli? Ni mtu anayetaka kuchaguliwa kuongoza Marekani kweli?

Binafsi siamini kama ni pandikizi. Huwa siko mtu wa conspiracy theories.

Lakini tabia za Trump kwa kweli zinashangaza.

Na mimi tokea hata kabla hajatangaza kugombea nilishasema kuwa jamaa hayuko serious kabisa.
Hayuko serious, pamoja na mapungufu yake angejipanga vizuri Hillary asingenusa SH.

Lakini pengine yeye anaona udhaifu wake ndiyo nguvu yake!!
 
  • Thanks
Reactions: kui
I've said it way back, I'll say it again: The next President of the United States is Hillary Clinton.

She's the better devil.

This Orange Guy will soon be forgotten in a couple of months.
 
Hayuko serious, pamoja na mapungufu yake angejipanga vizuri Hillary asingenusa SH.

Lakini pengine yeye anaona udhaifu wake ndiyo nguvu yake!!

Pia, Bill Clinton na Donald Trump wote ndo walewale tu.

Tofauti yao ni kwamba, mmoja yupo on tape akiongea vile ilhali mwingine mpaka hivi sasa hakuna recording yoyote ile inayothibitisha tuhuma juu yake.

Tofauti ingine ni kwamba Bill walau anajua namna ya ku behave hadharani.

Ila kimsingi wote wawili ni ma predators na perverts.
 
Haya...WikiLeaks nao wametoa transcripts za hotuba za Hillary ambazo zinathibitisha unafiki na uongo wake.

Lakini huwezi kulinganisha unafiki na huo uongo wa Hillary na tabia za Trump.

Kweli mwaka huu Wamarekani wameula wa chuya!

Yaani katika watu zaidi ya milioni 300 hawa ndo wagombea wawili walioweza kuchaguliwa kugombea urais na vyama vyao?

Ndo maana naamini yeyote kati yao atakayeshinda huu uchaguzi [binafsi naamini Hillary atashinda] atakuwa one term president.
 
Haya...WikiLeaks nao wametoa transcripts za hotuba za Hillary ambazo zinathibitisha unafiki na uongo wake.

Lakini huwezi kulinganisha unafiki na huo uongo wa Hillary na tabia za Trump.

Kweli mwaka huu Wamarekani wameula wa chuya!

Yaani katika watu zaidi ya milioni 300 hawa ndo wagombea wawili walioweza kuchaguliwa kugombea urais na vyama vyao?

Ndo maana naamini yeyote kati yao atakayeshinda huu uchaguzi [binafsi naamini Hillary atashinda] atakuwa one term president.

The bad and the ugly!
Yaani uko sahihi hommie
Bora hii matchup ingekuwa Jeb vs Corry Booker
Olympus could fall
 
Hillary ana mapungufu but at least people have an idea of what to expect from her, unlike her unpredictable opponent.

Hakuna binadamu asiye na mapungufu na kwa mwanasiasa kubadili msimamo si dhambi. Mwaka 2012 Hilary Clinton aliongoza kama mwana mama aliyeheshimika zaidi duniani hadi siku alipotangaza kugombania Urais.

Kama kawaida Republicans wakamvalia njuga Kama walivyofanya na wanavyoendelea kufanya kwa Obama. Hakuna hatua aliyochukua Obama wasiipinge hata Kama mwanzoni waliunga mkono.

Mapungufu ya Clinton huwezi kuyaweka mizani moja na mhuni Trump hata kama humpendi Vipi huyo mama. Uchaguzi wa Marekani safari hii ni kama kumsukuma mlevi (Trump)
 
Pia, Bill Clinton na Donald Trump wote ndo walewale tu.

Tofauti yao ni kwamba, mmoja yupo on tape akiongea vile ilhali mwingine mpaka hivi sasa hakuna recording yoyote ile inayothibitisha tuhuma juu yake.

Tofauti ingine ni kwamba Bill walau anajua namna ya ku behave hadharani.

Ila kimsingi wote wawili ni ma predators na perverts.

Nilikuwa sijui kama Bill Clinton anagombea urais mwaka huu.
 
Haya...WikiLeaks nao wametoa transcripts za hotuba za Hillary ambazo zinathibitisha unafiki na uongo wake.

Lakini huwezi kulinganisha unafiki na huo uongo wa Hillary na tabia za Trump.

Kweli mwaka huu Wamarekani wameula wa chuya!

Yaani katika watu zaidi ya milioni 300 hawa ndo wagombea wawili walioweza kuchaguliwa kugombea urais na vyama vyao?

Ndo maana naamini yeyote kati yao atakayeshinda huu uchaguzi [binafsi naamini Hillary atashinda] atakuwa one term president.

Hakuna cha ajabu WikiLeaks zaidi ya propaganda za The DeplorableNews (FoxNews).
 
Hakuna binadamu asiye na mapungufu na kwa mwanasiasa kubadili msimamo si dhambi. Mwaka 2012 Hilary Clinton aliongoza kama mwana mama aliyeheshimika zaidi duniani hadi siku alipotangaza kugombania Urais.

Kama kawaida Republicans wakamvalia njuga Kama walivyofanya na wanavyoendelea kufanya kwa Obama. Hakuna hatua aliyochukua Obama wasiipinge hata Kama mwanzoni waliunga mkono.

Mapungufu ya Clinton huwezi kuyaweka mizani moja na mhuni Trump hata kama humpendi Vipi huyo mama. Uchaguzi wa Marekani safari hii ni kama kumsukuma mlevi (Trump)


Nailed it!, na hapo red ni everything.
 
Nilikuwa sijui kama Bill Clinton anagombea urais mwaka huu.

Na, chakushangaza Trump hata kamtaja kwenye apology statement yake, sijui Bill wa nini zaidi ya kupunguza uzito wa message yake ambayo ni most important for him in the middle of this storm.

Na kesho kwenye debate I bet he's going to yell Bill Clinton most part of it.
 
Na, chakushangaza Trump hata kamtaja kwenye apology statement yake, sijui Bill wa nini zaidi ya kupunguza uzito wa message yake ambayo ni most important for him in the middle of this storm.

Na kesho kwenye debate I bet he's going to yell Bill Clinton most part of it.

Jamaa ni kubwa jinga. Ni sawa na mtoto unamuuliza kwanini umetukana halafu anasema mbona John ametukana?
 
  • Thanks
Reactions: kui
Back
Top Bottom