Bowie
JF-Expert Member
- Sep 17, 2016
- 4,372
- 6,078
Kwa kipindi cha mwaka mmoja wa utawala wa serikali ya awamu ya tano sina budi kumpongeza Rais John Pombe Magufuli kwa kazi kubwa aliyoyafanya katika kipindi cha mwaka mmoja. Katika uchaguzi wa mwaka 2015 Watanzani wengi walikuwa wamekataa tamaa na kuendelea kutawaliwa na Chama cha Mapinduzi kwasababu chama kilikoswa mwelekeo na kilivamiwa na viongozi wengi waliokuwa wakiweka maslahi yao ama maslahi ya biashara zao kwa kutumia jina la chama.
Toka aingie madarakani Rais Magufuli ameonyesha dhamira kubwa ya kutaka kuleta maendeleo na mabadiliko makubwa hapa nchini kwa kauli mbiu yake ya hapa kazi tu. Suala la ufisadi halikuwa linahusu chama cha mapinduzi pekee yake bali huyu mdudu UFISADI alikuwa pia katika vyama vya upinzani kwa mfano tumeona baadhi ya viongozi wa upinzani wakipanga kwenye nyumba za msajili bila kulipa kodi wengine wakihodhi mashamba makubwa bila kuyaendeleza wakati leo kuna Watanzania hawana hata sehemu za kuishi.
Katika kikao cha halmashuri kuu ya chama cha mapinduzi kilichofanyika majuzi Dar Mwenyekiti wa CCM John Magufuli alielezea mabadiliko makubwa anayotegemea kuyaleta ndani ya chama na nimekubaliana naye kwa asilimia 100 hayo Mabadiliko ni muhimu ili chama hicho kilichokuwa kimetekwa kirudi kwenye mkono wa wakulima na wafanyakazi na sio wafanyabiashara wachache. Tanzania si rahisi kupata kiongozi shupavu jasiri kama John Pombe Magufuli kwa maamuzi anayoyafanya.
Vyama vya upinzani vitafakari upya mikakati yao kwani kwasasa naona kama vinakosa mwelekeo kwani usitegemee leo nchi za Ulaya ndio zitaamua hatima ya siasa ya Tanzania, nchi hii ni nchi huru na hatima za siasa ya nchi hii itaamuliwa na watanzania wenyewe kupitia serikali iliyopo madarakani, kama kuna kasoro ni muhimu kwa viongozi wa upinzani kuonana na Rais Magufuli na kujadiliana naye jinsi ya kusukuma mbele gurudumu la maendeleo ya nchi hii mbele badala ya kutoa lugha za kejeli na kutishia maandamano.
Kwa kumalizia huu mtandao wa Jamii forums kuna baadhi ya wanachama hupenda kutumia lugha za matusi dhidi ya viongozi wa nchi hii akiwemo Mheshimiwa Rais Magufuli na kwa utamaduni wa kitanzania na wakiafrika ni jambo lisokubalika kabisa, mie binafsi nampa pole mwanzilishi wa mtandao kwa matatizo yaliyompata na mwenyezi Mungu atamuondelea matatizo hayo ila ndugu yangu hakikisha mtandao huu unatumika kuleta majadiliano mazuri kwa faida ya nchi hii sio matusi na lugha za kejeli.
Mwisho namtakia Rais Magufuli, familia yake pamoja na viongozi wake wote heri ya krismasi na Mwaka mpya.
Toka aingie madarakani Rais Magufuli ameonyesha dhamira kubwa ya kutaka kuleta maendeleo na mabadiliko makubwa hapa nchini kwa kauli mbiu yake ya hapa kazi tu. Suala la ufisadi halikuwa linahusu chama cha mapinduzi pekee yake bali huyu mdudu UFISADI alikuwa pia katika vyama vya upinzani kwa mfano tumeona baadhi ya viongozi wa upinzani wakipanga kwenye nyumba za msajili bila kulipa kodi wengine wakihodhi mashamba makubwa bila kuyaendeleza wakati leo kuna Watanzania hawana hata sehemu za kuishi.
Katika kikao cha halmashuri kuu ya chama cha mapinduzi kilichofanyika majuzi Dar Mwenyekiti wa CCM John Magufuli alielezea mabadiliko makubwa anayotegemea kuyaleta ndani ya chama na nimekubaliana naye kwa asilimia 100 hayo Mabadiliko ni muhimu ili chama hicho kilichokuwa kimetekwa kirudi kwenye mkono wa wakulima na wafanyakazi na sio wafanyabiashara wachache. Tanzania si rahisi kupata kiongozi shupavu jasiri kama John Pombe Magufuli kwa maamuzi anayoyafanya.
Vyama vya upinzani vitafakari upya mikakati yao kwani kwasasa naona kama vinakosa mwelekeo kwani usitegemee leo nchi za Ulaya ndio zitaamua hatima ya siasa ya Tanzania, nchi hii ni nchi huru na hatima za siasa ya nchi hii itaamuliwa na watanzania wenyewe kupitia serikali iliyopo madarakani, kama kuna kasoro ni muhimu kwa viongozi wa upinzani kuonana na Rais Magufuli na kujadiliana naye jinsi ya kusukuma mbele gurudumu la maendeleo ya nchi hii mbele badala ya kutoa lugha za kejeli na kutishia maandamano.
Kwa kumalizia huu mtandao wa Jamii forums kuna baadhi ya wanachama hupenda kutumia lugha za matusi dhidi ya viongozi wa nchi hii akiwemo Mheshimiwa Rais Magufuli na kwa utamaduni wa kitanzania na wakiafrika ni jambo lisokubalika kabisa, mie binafsi nampa pole mwanzilishi wa mtandao kwa matatizo yaliyompata na mwenyezi Mungu atamuondelea matatizo hayo ila ndugu yangu hakikisha mtandao huu unatumika kuleta majadiliano mazuri kwa faida ya nchi hii sio matusi na lugha za kejeli.
Mwisho namtakia Rais Magufuli, familia yake pamoja na viongozi wake wote heri ya krismasi na Mwaka mpya.