commonmwananchi
JF-Expert Member
- Mar 12, 2011
- 3,377
- 1,952
wana JF,
Nikiwa mtanzania mwenye nia njema na nchi yangu,haya ni maoni yangu binafsi.nitakubali kupokea changamoto au maoni toka kwa mwana JF yoyote mwenye maoni tofauti na mimi,pia hata wahusika waheshimiwa wenyewe kama wamo humu.
Kulingana na hali halisi ya siasa za Rorya,nikizingatia kauli niliyowahi kumsikia mheshimiwa Lameck airo katika kituo cha televisheni ya ITV akisema (ilikuwa kipindi cha ahadi majimboni) hatagombea nafasi hiyo kwenye uchaguzi wa 2015.
Ni dhahiri kuwa Nafasi hiyo itakuwa wazi kwa CDM kulichukuwa,tukizingatia kuwa tuna kijana mzalendo wa kweli ambaye ni mzaliwa wa jimbo husika Mh Ezekiel wenje. Ambaye ameonyesha uwezo mkubwa katika medani za siasa nchini na uwakilishi wa kweli.
Katika jimbo la Nyamagana kumekuwa na tabia mazowea ya kutomrudisha mbunge mmoja katika nafasi hiyo kwa awamu mbili mfululizo,bali wana uwezo wa kukipa chama nafasi ya uwakilishi bungeni kwa vipindi kadhaa,lakini kwa mgombea mpya kwa kila awamu (historia imetuonyeshha mara zote katika chaguzi zilizotangulia )
Sijui ni kwa nini tabia hii imechukuwa nafasi,(hili nalo linahitaji mjadala kulijadili). kwa hali halisi bado CDM wana nafasi kubwa na ushawishi wa kutosha mpaka sasa.na ninaomba mungu hili liendelee kuwa hivyo. Hadi mwaka 2015.
Mwaka 2015 ifanyike reshufle na tumchukuwee kijana msomi mwihgine ambaye ni mheshimiwa Diwani wa Kata ya Igoma,Mh Adam chagulani awe mgombea wa Nyamagana.
Kitendo cha CDM kulichukuwa Jimbo la Rorya kitaimarisha chama katika ukanda wa Tarime na mkoa wa Mara kwa ujumla.na kutufanya tuweze kujitanua zaidi hadi serengeti na kwingineko katika kanda ya ziwa..
Naomba kuwakilisha kwa nia nzuri, lakini nikitarajia maoni mbalimbali kwa nia nzuri na kwa maslahi na ustawi wa taifa letu na vizazi vijavyo.
Nikiwa mtanzania mwenye nia njema na nchi yangu,haya ni maoni yangu binafsi.nitakubali kupokea changamoto au maoni toka kwa mwana JF yoyote mwenye maoni tofauti na mimi,pia hata wahusika waheshimiwa wenyewe kama wamo humu.
Kulingana na hali halisi ya siasa za Rorya,nikizingatia kauli niliyowahi kumsikia mheshimiwa Lameck airo katika kituo cha televisheni ya ITV akisema (ilikuwa kipindi cha ahadi majimboni) hatagombea nafasi hiyo kwenye uchaguzi wa 2015.
Ni dhahiri kuwa Nafasi hiyo itakuwa wazi kwa CDM kulichukuwa,tukizingatia kuwa tuna kijana mzalendo wa kweli ambaye ni mzaliwa wa jimbo husika Mh Ezekiel wenje. Ambaye ameonyesha uwezo mkubwa katika medani za siasa nchini na uwakilishi wa kweli.
Katika jimbo la Nyamagana kumekuwa na tabia mazowea ya kutomrudisha mbunge mmoja katika nafasi hiyo kwa awamu mbili mfululizo,bali wana uwezo wa kukipa chama nafasi ya uwakilishi bungeni kwa vipindi kadhaa,lakini kwa mgombea mpya kwa kila awamu (historia imetuonyeshha mara zote katika chaguzi zilizotangulia )
Sijui ni kwa nini tabia hii imechukuwa nafasi,(hili nalo linahitaji mjadala kulijadili). kwa hali halisi bado CDM wana nafasi kubwa na ushawishi wa kutosha mpaka sasa.na ninaomba mungu hili liendelee kuwa hivyo. Hadi mwaka 2015.
Mwaka 2015 ifanyike reshufle na tumchukuwee kijana msomi mwihgine ambaye ni mheshimiwa Diwani wa Kata ya Igoma,Mh Adam chagulani awe mgombea wa Nyamagana.
Kitendo cha CDM kulichukuwa Jimbo la Rorya kitaimarisha chama katika ukanda wa Tarime na mkoa wa Mara kwa ujumla.na kutufanya tuweze kujitanua zaidi hadi serengeti na kwingineko katika kanda ya ziwa..
Naomba kuwakilisha kwa nia nzuri, lakini nikitarajia maoni mbalimbali kwa nia nzuri na kwa maslahi na ustawi wa taifa letu na vizazi vijavyo.