2010 elections: JF tunasupport WAZEE au VIJANA?

mzaramo

JF-Expert Member
Sep 4, 2006
6,371
5,174
I think its about time tukaamua kama chombo kwenye uchaguzi wa 2010 tunasupport Vijana au wazeee

by Vijana simaanishi akina calibr ya akina Lawrence Masha (alishapata nafasi na alishindwa na si Kijana anymore) balli ninamaanisha Vijana ambao wako UNDER 36 yrs regardless of chama kipi wanakiwakilisha

In otherwords tunaendelea na BACK TO THE SAME au NEW BLOOD

lakini its about time tukaamua tuko upande upi.
 
Mimi nasapoti mtu mwenye nia ya kweli ya kuongoza, muadilifu, asiye fisadi, mwenye mtazamo na uwezo wa kuleta positive changes, capacity builder na sifa zote za kiongozi bora

sijali umri, kabila au dini!!!

NAWAKILISHA
 
I think its about time tukaamua kama chombo kwenye uchaguzi wa 2010 tunasupport Vijana au wazeee

by Vijana simaanishi akina calibr ya akina Lawrence Masha (alishapata nafasi na alishindwa na si Kijana anymore) balli ninamaanisha Vijana ambao wako UNDER 36 yrs regardless of chama kipi wanakiwakilisha

In otherwords tunaendelea na BACK TO THE SAME au NEW BLOOD

lakini its about time tukaamua tuko upande upi.


Chombo gani unaongelea? JF au kitu kingine? Na unataka ku-support vijana ili iweje? Kwa namna gani? Tuweke sawa basi ili twende pamoja.
 
Mimi nasapoti mtu mwenye nia ya kweli ya kuongoza, muadilifu, asiye fisadi, mwenye mtazamo na uwezo wa kuleta positive changes, capacity builder na sifa zote za kiongozi bora

sijali umri, kabila au dini!!!

NAWAKILISHA

back to the same
 
I think its about time tukaamua kama chombo kwenye uchaguzi wa 2010 tunasupport Vijana au wazeee.

Haitawezekana kuamua kama CHOMBO. Hii si demokrasia.

Harafu, achana na mawazo potofu - kwamba umchague kiongozi wako kwa kigezo cha umri wake.

Kiongozi bora atapimwa kwa kauli zake, sera zake, past background yake na ikiwezekana amedeliver nini huko nyuma. Mzee au Kijana si hoja ya msingi
 
JF ni ya wananchi wote,vijana kwa wazee,wanawake kwa wanaume,wenye ulemavu na wasio na ulemavu,maskini na matajiri,maarufu na wasio maarufu ,wenye dini na wasio na dini,waislaum na wakristo hivyo sidhani kama ni sahihi kwa JF kama taasisi kusapoti au kutosapoti kundi lolote...
 
Haitawezekana kuamua kama CHOMBO. Hii si demokrasia.

Harafu, achana na mawazo potofu
- kwamba umchague kiongozi wako kwa kigezo cha umri wake.

Kiongozi bora atapimwa kwa kauli zake, sera zake, past background yake na ikiwezekana amedeliver nini huko nyuma. Mzee au Kijana si hoja ya msingi

JF ni ya wananchi wote,vijana kwa wazee,wanawake kwa wanaume,wenye ulemavu na wasio na ulemavu,maskini na matajiri,maarufu na wasio maarufu ,wenye dini na wasio na dini,waislaum na wakristo hivyo sidhani kama ni sahihi kwa JF kama taasisi kusapoti au kutosapoti kundi lolote...
1994-Anna-Semamba-Makind.jpg
Kingunge%20%201.jpg


the above personalities must be very Proud of you...i guess ule msemo wa CHANGE WE CAN BELIEVE IN does not resonate na watu kama nyinyi...

Hawa wazee wamekuwa wakitutawala for over 40 years and what have we got? well you know what it is...kweli mtu kashindwa kuleta changes in the 20th Century anajipya la kutuletea in the 21st Century?

Might sound extreme lakini you know what wapewe hizo nafasi akina Mnyika na wenzie waende lakini Im tired of the MAKINDAS and KINGUNGES wa tangu enzi za Nabii Nuhu!!
 
It is irrelevant kuangalia umri kwenye uongozi.......however, ukiangalia vizee vilivyopo CCM na kwingineko ni hivyo hivyo vime-support ubaradhuli unaoendelea.........inatia hasira sana

Tufikie mahala tuwaambie wazi viongozi wetu yale mapungufu yao bila kujali umri wala nini......
 
Hawa wazee wamekuwa wakitutawala for over 40 years and what have we got? well you know what it is...kweli mtu kashindwa kuleta changes in the 20th Century anajipya la kutuletea in the 21st Century?

Might sound extreme lakini you know what wapewe hizo nafasi akina Mnyika na wenzie waende lakini Im tired of the MAKINDAS and KINGUNGES wa tangu enzi za Nabii Nuhu!!

Then kumbe si suala la UMRI wao, bali ni kwamba hawajadeliver kitu in 40 years!

Kwa hiyo akina Mnyika wapewe tuuu kwa kuwa ni VIJANA? Labda una maana kwamba TUWAJARIBU vijana nao tuone kama wataweza. Tumefikia hatua sasa hatuna matumaini na ni jambo la kujaribisha jaribisha tu
 
Tunachotakiwa si kuangalia nani tuangalie ni kitu gani ame delier kwenye uongozi wake nafikiri hapa tatizo si umri ila umri nao wakati mwingine huendana na mazoea hatutaki kiongozi anayeongoza kwa mazoea

Tunataka anayeongoza kwa ubunifu kama tunaona labda huyu ubunifu wake umefifia kutokana na uzee basi hatufai lakini kama ubunifu wake bado una msaada tutam support

Ingawa pia wakati mwingine yeye anatakiwa atumie busara hata kama bado u kiongozi mzuri na umetumikia taifa kwa muda mrefu say 30-40 yrs ni vizuri akapumzika kwa hiari na ukawa mshauri wa wengine si kusubiri hadi ukataliwe kwenye kura za maoni.
 
Acheni mambo ya 'vijana' versus 'wazee'. Hamjui utu uzima ni dawa? Mfano hai ni pale Mzee Malecela alipoleta historia katika kumuweka sawa Sofia Simba. Vijana hawakuweza kufanya hesabu za haraka na huenda hawakujua nini kilijiri huko nyuma ili kuweza ku-crash muswada wa Sofia!

Jingine, suala zima la Sofia Simba kupeleka muswada tata kiasi hicho bungeni haliingii akilini. Hivi miswada hii kabla ya kupelewa Bungeni huwa haipitii kwenye Baraza la Mawaziri?
 
WAZEE VIJANA YALEYALE TU MBONA TUNA MAWAZIRI VIJANA MASHA NA WENZAKE wamezidi kutuangusha tu
 
Then kumbe si suala la UMRI wao, bali ni kwamba hawajadeliver kitu in 40 years!

Kwa hiyo akina Mnyika wapewe tuuu kwa kuwa ni VIJANA? Labda una maana kwamba TUWAJARIBU vijana nao tuone kama wataweza. Tumefikia hatua sasa hatuna matumaini na ni jambo la kujaribisha jaribisha tu
Uongozi sio suala la kubahatisha na naamini ndio mambo yanayotusumbua sasa kama nchi. Mtu ambaye ki asili ni kiongozi kipaji chake hakijifichi, na hivyo haipaswi tubahatishe au tumpe mtu kwa kigezo cha ujana au umri wake. Cha msingi tuwe wakweli tumchague mtu ambaye tunaamini atatufikisha pale tunapo patarajia kutokana na mtazamo wake, upeo wake katika kuchambua mambo na hasa kiongozi mzuri ni yule ambaye anafahamu matatizo yetu kama taifa.

Na cha mwisho ni kwamba kwa kuwa hakuna binadamu mkamilifu kama kiongozi ana nafasi yake kitika hili hivyo awe msikivu, asiwe haambiliki.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom