2 Yrs CCM Makatibu Wakuu 3, CHADEMA safu ileile

mwemanga

Senior Member
Oct 22, 2012
120
31
Wana Jf napenda kutowa hoja hii kuwa DK.slaa ni katibu mkuu bora kuliko makatbu wakuu wote wa vyama vya siasa nchi tanzania. tathimini hii nimeifanya mimi mwenyewe kutokana na namna anavyo fanya kazi za chama.

Niliwahi kufanya kazi na katbu mkuu wa NCCR mageuzi wakati ule ndugu. Mabere Malando mwaka 1994 mpaka 1997 niliwahi kufanya kazi na katbu mkuu wa CUF Chama cha wananchi ndugu. Maalim Seif sharif hamadi mwaka 1998 mpaka 2007 na ninafanya kazi na dk.slaa tokea mwaka 2008 mpaka leo hii nikiwa mtendaji katka ngazi za chini za uongozi kata,jimbo na wilaya nimegundua kuna tofauti kubwa sana kati ya Dk.Slaa na makatibu wezake.

1. dk.slaa anapo fanya ukaguzi wa chama anapo kuja ktk ngazi yako ya uongozi ana kagua Uhalali wa wajumbe.

2.anasoma mihutasari ya vikao vyenu kisha ana jenga hoja kupitia alicho soma.

3. hata akiwepo ofisini ana towa matamko kwa watendaji. hali hii haipo kwa makatibu wengine wa vyama vingine utakuta wao wanapo kagua chama huwa wanasomewa risala basi kisha wao hawakagui chochote.
 
Wana Jf napenda kutowa hoja hii kuwa DK.slaa ni katibu mkuu bora kuliko makatbu wakuu wote wa vyama vya siasa nchi tanzania. tathimini hii nimeifanya mimi mwenyewe kutokana na namna anavyo fanya kazi za chama. niliwahi kufanya kazi na katbu mkuu wa NCCR mageuzi wakati ule ndugu. mabere malando mwaka 1994 mpaka 1997 niliwahi kufanya kazi na katbu mkuu wa CUF Chama cha wananchi ndugu. maalim seif sharif hamadi mwaka 1998 mpaka 2007 na ninafanya kazi na dk.slaa tokea mwaka 2008 mpaka leo hii nikiwa mtendaji katka ngazi za chini za uongozi kata,jimbo na wilaya nimegundua kuna tofauti kubwa sana kati ya dk.slaa na makatibu wezake. 1. dk.slaa anapo fanya ukaguzi wa chama anapo kuja ktk ngazi yako ya uongozi ana kagua Uhalali wa wajumbe. 2.anasoma mihutasari ya vikao vyenu kisha ana jenga hoja kupitia alicho soma. 3. hata akiwepo ofisini ana towa matamko kwa watendaji. hali hii haipo kwa makatibu wengine wa vyama vingine utakuta wao wanapo kagua chama huwa wanasomewa risala basi kisha wao hawakagui chochote.

Nilitupa kadi yangu ya CCM kutokana na uzalendo alonao huyu mzee. Nashindwa kuelewa majitu mengine yanayosambaza picha zao za uchi kwa wanawake kupitia mitandao kujiita makada wa CCM huku wakikimbia familia zao. Hawa watatusaidia nini wakati hawawezi kuzisaidia familia zao. Mengine wauwaji wa Faru na Tembo ndio makatibu wetu wakuu? Hapana sikubaliano nao. Naomba Mungu 2015 ifike Kinana na kundi lote la CCM waende segerea.
 
Nilitupa kadi yangu ya CCM kutokana na uzalendo alonao huyu mzee. Nashindwa kuelewa majitu mengine yanayosambaza picha zao za uchi kwa wanawake kupitia mitandao kujiita makada wa CCM huku wakikimbia familia zao. Hawa watatusaidia nini wakati hawawezi kuzisaidia familia zao. Mengine wauwaji wa Faru na Tembo ndio makatibu wetu wakuu? Hapana sikubaliano nao. Naomba Mungu 2015 ifike Kinana na kundi lote la CCM waende segerea.
Tembo a.k.a ndovu wanafanyiwa kitu kinaitwa organised crime, na imezidi kuwa organised baada ya majangili kuwa organised vema kwenye mifumo ya kiutawala na udhalimu.
 
images
images

Rais Kikwete na Rais wa zamani Tanzania awamu liliyomtangulia Kikwete Benjamini Mkapa

images
images
images
Yusuf Makamba, Mukama, na Kinana
Makatibu Wakuu CCM tangu uchaguzi Mkuu uliopita

Mawimbi ya Chadema yameweza kuipiga meli ya CCM ndani tangu Uchaguzi Mkuu uliopita kwa miaka miwili na kusababisha kubadilisha manahodha wa meli watatu ndani ya muda huu mfupi.

Nahodha wa awali Kanali Yusuf Makamba aka mgosi wa kaya, ilionekana akipumzisha itakuwa dawa kwa kumkabidhi unahodha mzee wa kiwango cha kutuliza nerves, huku uvuvuzela wa Chama kukabidhiwa Nape. Moto ulioanza wakati ule ambao Mwenyekiti wao aliuasisi kwa lugha yenye lafudhi ya kisiasa ya kuvuana magamba na wengine kupewa siku 90 huku Nape akivimbishia mishipa usoni kuzunguka nchi nzima kana kwamba mizizi ya fitina imeshakatwa, ikaanza kupooza kama ugali ulisubiria walaji bila kujitokeza na kubakia hoja hiyo kubaki kiporo kisichoweza kuliwa tena bali ni kutupwa na hivyo kuonekana tatizo Nahodha aliduwazwa kwa kuingizwa mkenge tu bila kujua mfumo wa system inayoendesha kwenye meli hiyo.

Mukama anapojaribu kusogeza kiti vizuri kwenye usukani mara inaonekana ujuzi wake wa kuongoza meli hiyo hana na hivyo bora kuirudisha kwa wanajeshi kama walizoea misukosuko katika shughulizao kama alivyokuwa mgosi wa kaya, kwa kumkabidhi Sijui Luten au kanali Kinana. Hawakumkawiza kwani wajuaji wameshaanza choko choko chombo cha usafiri majini ambacho Kinana ni miliki kupata kashfa ya kukutwa na nyara za Taifa huko Hon Kong tuhuma ambayo ameikanusha bila vielelezo vya mmiliki wa nyara hizo. Kwani anapokosekana mmuliki wa mali katika chombo cha usafirishaji, mmiliki moja kwa moja ndiye mhusika.

Manahodha watatu wamebadilishana offisi kuu ya Katibu Mkuu CCM tangu kampeni za uchaguzi mkuu uliopita ndani ya miezi 27. Hii ni dalili tosha Chadema imeitikisa CCM kwa kiwango kisicho cha kwaida kwani si jambo la kawaida nafasi hizo zibadilishwe mara kwa mara ukitilia maanani wengine hata uzoefu wa ofisi tu ulikuwa bado.

Je, CCM wanatambua kaya madadiliko nchini inayoendeshwa na upinzani wa CCM tangu uchaguzi mkuu uliopita? Upinzani ungali vyama vya msimu kama Kikwete alivyotamka katika kampeni za uchaguzi mkuu uliopita?

Dr-Wilbroad-Slaa1.jpg
Mbowetalk(3).jpg

Uongozi wa Juu Chadema haujayumba ila unazidi kuimarika licha ya jitihada kubwa za CCM kufanya kila kinachowezekana kuyumbisha lakini wamesimama imara.
 
Inavyoonekana ni jitihada nyingi za serikali ya CCM kufanya mambo mengi kwa njia ya zimamoto ili kuwaonyesha wapiga kura kwamba ahadi nyingi za kuboresha hali ya uchumi inastawi.

CCM kwa sasa nao wanapanda majukwaani kujitetea kwa njia ya hoja mbalimbali huku wakati huohuo wale wanasiasa wasio na ujuzi wanaojiita wajumbe wa NEC kama Hussein Bashe na Nape Nnauye wakiwa wanazidi kukididimiza chama hicho kwenye eneo la propaganda.

Ndio maana wamemrudisha mashine ya propaganda mzee Kinana afanye vitu vyake. Lakini huyu nae historia yake inajulikana na juzi pale Arusha akaongea mambo yasiyoeleweka kuhusu viwanda kwamba zinatafutwa njia ya kuviinua wakati yeye alikuwepo enzi hizo kiwanda cha matairi cha General Tyre kilipokufa huku kikijiona.

Ni CCM ndio ilianzisha viwanda na kwasababu ya kuwa na mchanganyiko wa mafisadi na wale wanaoona mbali ni CCM hiyohiyo ikaviua viwanda hivyo.

Pia ni CCM hiyohiyo iliyoua mashirika yote ya umma kwa kisingizio cha kufanya ubinafsishaji na wanachama wake wengi tu wakiongozwa na mwenyekiti wao wakajizolea mali nyingi za serikali tena kwa bei poa.

CCM inatawaliwa na rushwa na ufisadi na hata katika mkutano wake mkuu mambo hayo mawili yalitawala kiasi cha watu wa aina ya Bashe kutembeatembea ukumbini wakipiga kampeni za chinichini juu ya mjumbe fulani kutoka kusini asipite.

Na hata kama watabadilisha sekretarieti yake hata mara 20 bado doa lipo palepale la CCM kukumbatia Rushwa na Ufisadi, na kushindwa kwa chama hiki hapo uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, ambao wapiga kura kwa maadili kabisa watakwenda kupigia kura mageuzi ya kisiasa nchini mwetu kwamba kuwepo na chama mbadala ambacho kitaleta utaratibu mpya wa uendeshaji nchi.
 
CS;

Najua nitapigwa madongo. Lakini kwa sisi tusio na vyama vya siasa tunaweza kuchambua vingine. CCM alitoa ahadi kuwa akishinda atafanya hivi na vile. Na vilevile ndio mwenye kuwa na bajeti ya nchi na kuifanyia mipango ya utekelezaji. Hivyo akiboronga mtaji wake wa kisiasa unapungua kwa kiasi kikubwa.

Kwa upande mwingine. CDM kazi yake ni kuonyesha wapi watawala wanakosea au wanaonea. CDM are activists. The real test of characters will come when we, the people, give CDM power.
 
Na bado mpaka 2015 makatibu wanaweza kufika hata 5, hiki chama hakina wachezaji wa akiba wote ni majeruhi na wengine wana kadi nyekundu hawawezi rudi uwanjani mpaka 2015 sababu ya makundi, hiki chama kina laana ila waliomo ndani yake hawajui ama wanajua ila wamelalia masikio kwa utamu wa madaraka na hela za kifisadi ila 2015 wengi presha zitawalaza kitandani.
 
Na bado mpaka 2015 makatibu wanaweza kufika hata 5, hiki chama hakina wachezaji wa akiba wote ni majeruhi na wengine wana kadi nyekundu hawawezi rudi uwanjani mpaka 2015 sababu ya makundi, hiki chama kina laana ila waliomo ndani yake hawajui ama wanajua ila wamelalia masikio kwa utamu wa madaraka na hela za kifisadi ila 2015 wengi presha zitawalaza kitandani.

Duh! Umenivunja mbavu, hahaha! Yaani timu imejaa majeruhi na wenye red card, kwa sasa ni kujaribu kuwaingiza uwanjani wale wenye yellow card. Jamaa JF ni great thinker haswaaa! Wenye Yellow card ni hawa akina Kinana nadhani, maana kashfaya meli yake kushikwa na pembe za ndovu nchi za mashariki ya mbali huko ni kizungumti.



 
CCM wanachofanya ni kama mazingaombwe ili kuhadaa wananchi kwamba wanafanya mabadiliko yatakayoleta matumaini kwa wananchi.. kumbe wote ni vibaka watupu! Kila wanapobadili uongozi ndivyo wanavozidi kuongeza Uchafu zaidi ya ule wa mwanzo!!
 
CCM wanachofanya ni kama mazingaombwe ili kuhadaa wananchi kwamba wanafanya mabadiliko yatakayoleta matumaini kwa wananchi.. kumbe wote ni vibaka watupu! Kila wanapobadili uongozi ndivyo wanavozidi kuongeza Uchafu zaidi ya ule wa mwanzo!!

Afadhali Yusufu na Mukama hawakuwa na matakataka ya pekee kama huyu Kinana, naona patachimbika, mbona wapo wengi wazuri tu kwa nini wang'ang'aniwe wenye yellow card?
 
UKIONA UNAJENGA NYUMBA NA IKIFIKIA UMEPAUWA NA KUONA IMEPATA NYUFA DAWA SI KUTINDUA UFA BALI NI KUBOMOA NYUMBA NA KUJENGA MSINGI MPYA,CCM MSINGI WAKE UMEDHOOFU,NI LAZIMA UBOMOLEWE,vinginevyo wataingia hasara mara maengeneer watakapo amuru kuvunjwa kwa jengo[CCM],KUBOMOLEWA KWA KUHATARISHA MAISHA YA WAKAAZI WAKE.
 
ukiona umemtongoza mwanamke na akakubali ukapeleka mahari yakakubaliwa ukafunga ndoa baada ya muda ukaanza kuzunguka huku na kule ukimtongoza kana kwamba hujafunga nae ndoa jua wewe ni khanisi na hufai kuwa na ndoa na huyo mama na ana haki ya kutafuta mwanamme mwingine.ndoa ikishafungwa mambo yote yanaishia ndani na nje watu wanashuhudia matokeo na huna haja ya kutangaza.

ccm kuzunguka mikoani na kutangaza mara oo tutawafukuza mwakala wa korosho,oo tutafufua viwanda,oo atakayepatikana kwa rushwa hatutasita kumfukuza.
madaraka mmeshapewa tendeni kazi kunakontena la katibu wa chama chenu china kalileteni na yeye mumfikishe mahakamani na wananchi wataona mko serously kwenye kazi. acheni longolongo.
 
makatibu.
dr slaa.........smg.

kinana............

maalim seif.........mshale.

nccr............kombeo.

udp................manati.
 
Ngoja waje wale watoto wa mafisadi wanaokesha humu JF kulinda maslahi ya familia zao kama Ritz uone watakavyo anza kuongelea ndoa yake utafikiri aliwachumbia akawatosa
 
Last edited by a moderator:
Katibu mkuu bora kwa kuvunja ndoa za watu,kutelekeza familia na kumiliki viwanda vya kutengeneza uongo.
 
Back
Top Bottom