2 Wafukuzwa kazi kwa Kudai Kuundwa chama cha Wafanyakazi Geita Gold

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
Wakati taifa bado linafuatilia habari za mgodi wa Barrick huko Tarime, habari nyingine ambazo zimepatikana zinadai kuwa viongozi 2 (mwenyekiti na Katibu) wa wafanyakazi kwenye mgodi wa Geita Gold huko Mkoani Geita wamefukuzwa kazi hapo jana huku wakipewa siku tatu kukata rufaa baadaya kuongoza maandamano ya kudai chama chao cha Wafanyakazi Migoni kisajiliwe kitu ambacho kinadaiwa kupingwa na menejjimenti kwa madai kuwa "idadi" ya wanachama haijatimia licha ya wafanyakazi hao kudai kuwa idadi imeshatimia ya kuweza kuundwa kwa chama cha kudai haki na maslahi ya wafanyakazi.



Upande wa menejimenti unadai kuwa wafanyakazi hao wamefukuzwa baadaya "kuwatukana" uongozi kwenye mabango yao ambayo yalitumika kudai chama chao cha wafanyakazi. Hadi hivi sasa imekuwa ngumu kwenye baadhi ya migodi kuunda vyama vya wafanyakazi wakati kwenye baadhi yao vyama hivyo vipo. Mgodi wa Kahama Mining unao chama cha wafanyakazi migodini (TAMICO).


Kuna mambo mengine ambayo yamo mikononi mwa vi-nzi na yataweletwa ili kuonesha harakati ambazo zinafanya kuzuia wafanyakazi kujiunga pamoja kupigania na kudai haki zao hasa huko migodini.




Fikra Pevu
 
Wakati taifa bado linafuatilia habari za mgodi wa Barrick huko Tarime, habari nyingine ambazo zimepatikana zinadai kuwa viongozi 2 (mwenyekiti na Katibu) wa wafanyakazi kwenye mgodi wa Geita Gold huko Mkoani Geita wamefukuzwa kazi hapo jana huku wakipewa siku tatu kukata rufaa baadaya kuongoza maandamano ya kudai chama chao cha Wafanyakazi Migoni kisajiliwe kitu ambacho kinadaiwa kupingwa na menejjimenti kwa madai kuwa "idadi" ya wanachama haijatimia licha ya wafanyakazi hao kudai kuwa idadi imeshatimia ya kuweza kuundwa kwa chama cha kudai haki na maslahi ya wafanyakazi.



Upande wa menejimenti unadai kuwa wafanyakazi hao wamefukuzwa baadaya "kuwatukana" uongozi kwenye mabango yao ambayo yalitumika kudai chama chao cha wafanyakazi. Hadi hivi sasa imekuwa ngumu kwenye baadhi ya migodi kuunda vyama vya wafanyakazi wakati kwenye baadhi yao vyama hivyo vipo. Mgodi wa Kahama Mining unao chama cha wafanyakazi migodini (TAMICO).


Kuna mambo mengine ambayo yamo mikononi mwa vi-nzi na yataweletwa ili kuonesha harakati ambazo zinafanya kuzuia wafanyakazi kujiunga pamoja kupigania na kudai haki zao hasa huko migodini.




Fikra Pevu

Pole sana Shigela..Kaza Buti
 
Wakati taifa bado linafuatilia habari za mgodi wa Barrick huko Tarime, habari nyingine ambazo zimepatikana zinadai kuwa viongozi 2 (mwenyekiti na Katibu) wa wafanyakazi kwenye mgodi wa Geita Gold huko Mkoani Geita wamefukuzwa kazi hapo jana huku wakipewa siku tatu kukata rufaa baadaya kuongoza maandamano ya kudai chama chao cha Wafanyakazi Migoni kisajiliwe kitu ambacho kinadaiwa kupingwa na menejjimenti kwa madai kuwa "idadi" ya wanachama haijatimia licha ya wafanyakazi hao kudai kuwa idadi imeshatimia ya kuweza kuundwa kwa chama cha kudai haki na maslahi ya wafanyakazi.



Upande wa menejimenti unadai kuwa wafanyakazi hao wamefukuzwa baadaya "kuwatukana" uongozi kwenye mabango yao ambayo yalitumika kudai chama chao cha wafanyakazi. Hadi hivi sasa imekuwa ngumu kwenye baadhi ya migodi kuunda vyama vya wafanyakazi wakati kwenye baadhi yao vyama hivyo vipo. Mgodi wa Kahama Mining unao chama cha wafanyakazi migodini (TAMICO).


Kuna mambo mengine ambayo yamo mikononi mwa vi-nzi na yataweletwa ili kuonesha harakati ambazo zinafanya kuzuia wafanyakazi kujiunga pamoja kupigania na kudai haki zao hasa huko migodini.




Fikra Pevu

Asante sana mkuu kwa taarifa.
Leo asubuhi nimemsikia Mwenyekiti wa TAMICO taifa akilalamikia suala hilo.

Sheria ya Ajira na Mahusiano kazini inaeleza wazi kuwa mfanyakazi hatakiwi kunyanyaswa wal kubaguliwa kwa sababu ya kujiunga na chama cha wafanyakazi kinachotambulika kitaifa.

Tatizo ninaloliona hapa ni kuwa waajiri wengi, hasa hawa wanaoitwa "wawekezaji" wanafanya hila za makusudi tena wakati mwingine kwa kushirikiana na "wazalendo".
Serikali iko wapi? kwani hii si case ya kwanza ya wafanyakazi kunyanyaswa.
 
Mh. Regia Mtema- Waziri kivuli wa Ajira na kazi.... hii yako komaa nayo mpaka kieleweke.
 
Ukoloni unarudi taratibu!
Kama hao jamaa wanajiamini, basi waweke hadharani mambo yote ya kishenzi ya hao waajiri, maana naamini mabango hayakuweza kueleza kila kitu!
Lakini utakuta baadhi ya oppressermen wa mgodi huo ni weusi wenzetu.
 
UMOJA NI NGUVU..UTENGANO NI UDHAIFU……Wathungu wanawachekechea hapa tuu…….Shigela maskini aliwatafutia mwanga wa dhahabu..utakuta weusi wenzake wamemgeuka na kusema yeye ndo kawashawishi lakini hawakushiriki kwa hiari yao…!! UMASKINI MTUPU TU UNATUDUNDA KA VITENESI…!!
 
Ninaamini kama watanzania hawawezi kukemea tabia hizi basi CHADEMA as chama cha wakombozi kichukuwe jukumu la kuweka wakili wa kujitolea ili watu hawa wapate haki zao. Nchi haiwezi kuendeshwa kiholela halafu wananchi tunyamaze kimya. Wakati wa kunyamaza kimya umeshapita. Tundu Lissu, wewe ni mbunge ambaye unafahamu zaidi matatizo yanayowakabili watanzania wenzetu huko migodini. Huu ni wakati muafaka kulishughulikia tatizo hilo. Kumbuka: Wabunge wa CHADEMA ni wabunge wa Taifa zima (hiyo ni kwa mujibu wa CHADEMA yenyewe).
Twende kazini huko migodini na sehemu zingine.
 
Mh. Regia Mtema- Waziri kivuli wa Ajira na kazi.... hii yako komaa nayo mpaka kieleweke.

tatizo haya madubwana BARRICK na GEITA yako very musculine in financial terms ndo maana serikali inalegea kama mbuzi vile anamfuata chatu...
 
Ninaamini kama watanzania hawawezi kukemea tabia hizi basi CHADEMA as chama cha wakombozi kichukuwe jukumu la kuweka wakili wa kujitolea ili watu hawa wapate haki zao. Nchi haiwezi kuendeshwa kiholela halafu wananchi tunyamaze kimya. Wakati wa kunyamaza kimya umeshapita. Tundu Lissu, wewe ni mbunge ambaye unafahamu zaidi matatizo yanayowakabili watanzania wenzetu huko migodini. Huu ni wakati muafaka kulishughulikia tatizo hilo. Kumbuka: Wabunge wa CHADEMA ni wabunge wa Taifa zima (hiyo ni kwa mujibu wa CHADEMA yenyewe).
Twende kazini huko migodini na sehemu zingine.

kalumbu twa mashiku ulipo gwa myitu...
 
Back
Top Bottom