2 Cabinet Ministers differ on dress code

Waheshimiwa, mbona hamsemi kwenye ofisi gani ya serikali, Tanzania na hata Ulaya mmeona mtu amevaa bikini? Condoleeza Rice ambaye inawezekana ndiye mwanamke mwenye nguvu kuliko wote anavaa nguo ambazo wenzetu mtaziita mini(zinaishia juu ya magoti) lakini kwa wengi ni nguo za staha. Hakuna mtu anayeweza kudai kuwa uvaaji wake wa nguo hizo na boots za nguvu zikisisitiza uanamke wake zinampunguzia heshima na ufanisi wake. Eddy, chuo kikuu ni mahali ambapo wanafunzi wanatakiwa wa'test' mipaka ya authority. Mimi binafsi ninapomuona mwanafunzi wa chuo kikuu amevaa suti na tai naingiwa na wasiwasi. Pale ni mahali ambapo non-conformity ndio wajibu. hii inaendana na mpaka mavazi. Mwanafunzi wa Chuo Kikuu akiingia uchi darasani sitamshangaa maana pengine kuna kitu anachotaka kuieleza jamii. Chuo kikuu ni mahali pa fukuto la mawazo. Kamwe usipachanganye na ofisi za serikali. Katika matatizo yote tuliyonayo leo tumapoteza muda wote huu kuangalia jambo ambalo hata halipo( hakuna mtu aliyeweza kutoa mfano wa ofisi ya serikali wanakovaa bikini au pajama)? Kuzungumzia hili ni kama kusimama jukwaani na kusema kuwa kuanzia leo unakataza kunywa pombe katika ofisi za serikali. Kama hii code(ambayo mimi naona ni ya kipuuzi) ipo angeikazia badala ya kuileta katika public realm.


Mchundo:

Dunia imebadilika sana. Utafiti unaonyesha kuwa watoto marekani wanapenda chips zilizo kwenye packet zenye label ya MacDonald kuliko zilizowekwa kwenye sahani japokuwa mpishi ni mmoja na radha ni sawa.

Nimebadilisha kazi zaidi ya mara tatu na kila sehemu ninapewa manual ya dress code.
 
Watanzania hatuna utamaduni wa dressing code. Kwenye mazishi unaona wasela wanazuka na jezi na track suit. Hata kama unachapa kazi vizuri lakini ukashindwa kujiwakilisha mwenyewe, utashindwa vibaya vibaya katika maisha.

Bin Maryam.
Mimi nakazania pale pale. Kwenye ofisi gani ya serikali umeona watu wamezuka na jezi na track suit? Tupeni mifano ya ofisi za serikali maana huyu mama alikuwa anazungumzia hizo na si kwenye mazishi au chuo kikuu!
 
Ahsante bin Maryam...ongeza na hiii....Birayani iliachwa wazi inang'ongwa na kugandiwa na NZI wa chooni na MUHOGO wa kuchemshwa uliofunikwa KAWA....UTAKULA UPI???
 
Chips za McDonald zinaitwa junk food na si chakula cha staha. Dress code iwepo na wafanyakazi wapewe. Ninachopinga ni huku kutangaza hadharani kama vile kwenye maofisi yote ya serikali yamejaa mini, vichupi na sidiria. sasa wengine wanataka ndevu na sura za kilevi(sio kuwa mlevi) na vyenyewe vipigwe marufuku. Huu ni utaratibu wa ndani, Chief Secretary angesambaza standing orders kwenye kila ofisi kuhusu hili bila kutunguiza hata wale ambao hatuma. Mbona maagizo kibao kuhusu nani anaruhusiwa kwa ndege daraja la kwanza, matumizi ya magari ya serikali n.k. na wanayafungia macho? Huko ulaya kuna code na zinategemea unafanya wapi. Huwezi kuwaambia vijana wa Google ati lazima wavae suti! Hayo waachie wale wa wall street. Waulize hao wakuu, kama hizi sheria zilikuwepo, waliishawafahamisha wafanyakazi wao kuhusu hili na wakapingwa? Tuna mambo ya maana zaidi ya kufanya kuliko hili.
 
Bin Maryam.
Mimi nakazania pale pale. Kwenye ofisi gani ya serikali umeona watu wamezuka na jezi na track suit? Tupeni mifano ya ofisi za serikali maana huyu mama alikuwa anazungumzia hizo na si kwenye mazishi au chuo kikuu!

Mchundo:

Mifano nitakayotoa imepitwa na wakati kwa sababu bongo nimeondoka kipindi.

Lakini nakumbuka kabla bunge alijatilia mkazo wa dress code kuna waheshimiwa walikuwa wanazuka na T-shirt, Jeans, training shoes. Waandishi wa habari ndio kabisa.
 
Ahsante bin Maryam...ongeza na hiii....Birayani iliachwa wazi inang'ongwa na kugandiwa na NZI wa chooni na MUHOGO wa kuchemshwa uliofunikwa KAWA....UTAKULA UPI???

Aliyekuambia umekaribishwa kula nani? Typical male chauvinism!
 
Lakini nakumbuka kabla bunge alijatilia mkazo wa dress code kuna waheshimiwa walikuwa wanazuka na T-shirt, Jeans, training shoes. Waandishi wa habari ndio kabisa.

Wabunge si wafanyakazi wa serikali. Pamoja na hao waandishi!
 
Chips za McDonald zinaitwa junk food na si chakula cha staha. Dress code iwepo na wafanyakazi wapewe. Ninachopinga ni huku kutangaza hadharani kama vile kwenye maofisi yote ya serikali yamejaa mini, vichupi na sidiria. sasa wengine wanataka ndevu na sura za kilevi(sio kuwa mlevi) na vyenyewe vipigwe marufuku. Huu ni utaratibu wa ndani, Chief Secretary angesambaza standing orders kwenye kila ofisi kuhusu hili bila kutunguiza hata wale ambao hatuma. Mbona maagizo kibao kuhusu nani anaruhusiwa kwa ndege daraja la kwanza, matumizi ya magari ya serikali n.k. na wanayafungia macho? Huko ulaya kuna code na zinategemea unafanya wapi. Huwezi kuwaambia vijana wa Google ati lazima wavae suti! Hayo waachie wale wa wall street. Waulize hao wakuu, kama hizi sheria zilikuwepo, waliishawafahamisha wafanyakazi wao kuhusu hili na wakapingwa? Tuna mambo ya maana zaidi ya kufanya kuliko hili.

Mfano wa Chips za McDonald ni packaging. Na dress code ni packaging. Muhimu wake huko katika kujiwakilisha.
 
Wabunge si wafanyakazi wa serikali. Pamoja na hao waandishi!

Wewe umesomea uhandisi au sayansi nini? Maana watu wa fani hizi wanataka majibu sahihi kama vile tupo kwenye sayansi project.

Huu ni ukumbi wa siasa na unachotakiwa ni kuwa vague na ku-spin points. Ndio maana katika hotuba yake ya mwaka mpya mnataka hotuba za JK zijibu masuala ya BOT kama vile anazungumza na wana JF, wakati yeye anazungumza na waliopigia kura ambao hata akaunti ya benki hawana na hawajui kuwa kuna kitu kinaitwa BOT.
 
Mfano wa Chips za McDonald ni packaging. Na dress code ni packaging. Muhimu wake huko katika kujiwakilisha.

Chips za Mcdonald ni marketing issue, wao wanauza lifestyle ambayo iko targeted kwa segment fulani ya jamii. Dress code si packaging. Dress code inalenga kumwezesha anayevaa atimize wajibu wake ipasavyo. Ndiyo maana hauwezi kudai fundi mchundo avae tai wakati yeye ni mtu wa magrisi. Na wale wanaotoa huduma kwa wateja wanapaswa wavae nguo ambazo zitawafanya wateja kuwa na imani nao ikiwa ni pamoja na kuamini kuwa zile nguo hazitakuwa kizuizi kwake kutoa huduma. Kwa mfano, aje fundi bomba nyumbani kwako Masaki kutoka Area 4 Ostabei, amefunga ushungi na amevaa baibui utaamini kweli ataweza kuzibua choo? Au utamwamini zaidi akiwa amevaa jeans na training shoes? Vilevile ukimkuta sekretari amevaa bikini utapoteza imani.Hawa wote ni wafanyakazi wa serikali. Kama kawaida katika kutafuta cheap popularity tume rahisisha sana ishu. Tatizo hili si kubwa kama ambavyo mtu unavyoweza kudhani kutokana na matamshi ya Mheshimiwa waziri.
 
Wewe umesomea uhandisi au sayansi nini? Maana watu wa fani hizi wanataka majibu sahihi kama vile tupo kwenye sayansi project.

Touche, Bin Maryam. Mimi Fundi tuu mkuu. Samahani bado sijachangia thread yako, nitafanya hivyo hivi karibuni. Ngoja basi niwaachie wanasiasa wapambane maana spin siwezi!
 

Chips za Mcdonald ni marketing issue, wao wanauza lifestyle ambayo iko targeted kwa segment fulani ya jamii. Dress code si packaging. Dress code inalenga kumwezesha anayevaa atimize wajibu wake ipasavyo. Ndiyo maan hauwezi kudai fundi mchundo avae tai wakati yeye ni mtu wa magrisi. Na wale wanaotoa huduma kwa wateja wanapaswa wavae nguo ambazo zitawafanya wateja kuwa na imani nao ikiwa ni pamoja na kuamini kuwa zile nguo hazitakuwa kizuizi kwake kutoa huduma. Kwa mfano, aje fundi bomba nyumbani kwako Masaki kutoka Area 4 Ostabei, amefunga ushungi na amevaa baibui utaamini kweli ataweza kuzibua choo? Au utamwamini zaidi akiwa maevaa jeans na training shoes? Vilevile ukimkuta sekretari amevaa bikini utapoteza imani.Hawa wote ni wafanyakazi wa serikali. Kama kawaida katika kutafuta cheap popularity tume rahisisha sana ishu. Tatizo hili si kubwa kama ambavyo mtu unavyoweza kudhani kutokana na matamshi ya Mheshimiwa waziri.

Kama kuna norms zinaonyesha dress code basi aliyesema hana makosa yoyote kwa sababu anarudia vile vilivyoandikwa. Kama anachosema ni uzushi basi atakuwa anachemsha.

Na yule anayesema kinachotakiwa ni ufanisi anachemsha big time kwa sababu hatujawahi kuwa wafanisi.
 
Touche, Bin Maryam. Mimi Fundi tuu mkuu. Samahani bado sijachangia thread yako, nitafanya hivyo hivi karibuni. Ngoja basi niwaachie wanasiasa wapambane maana spin siwezi!

Mimi mchundo pia lakini hata ku-repair switch ni lazima niite fundi.
 
Na yule anayesema kinachotakiwa ni ufanisi anachemsha big time kwa sababu hatujawahi kuwa wafanisi.

Na ndiyo unataka tuwekeze kwenye nuclear? Hututakii mema.

Mimi mchundo pia lakini hata ku-repair switch ni lazima niite fundi.

Huyo fundi anakuja amevaa baibui?
 
Back
Top Bottom