1972 somalia ilisuluhisha mgogoro uliokuwepo kati ya tanzania na uganda

KELVIN GASPER

JF-Expert Member
Nov 1, 2010
1,066
454
Mwalimu nyerere wakati anaongea na wazee wa mkoa wa dar es salaam mwaka 1978 aliwaeleza kuwa serikali ya somalia ndio iliyosuluhisha mgogoro uliokuwepo kati ya tanzania na uganda. anaendelea kuwa hali ilikuwa ni tete kwani nchi zote mbili zilishasogeza majeshi hadi mpakani tayari kwa vita. ilifikiwa makubaliano kuwa majeshi pande zote mbili yarudishwe nyuma kilometa kumi kwa kila upande wa mpaka. Mwalimu Nyerere anadai kuwa wakuwahi hata siku moja kumpenda Idd Amini kwani nae alikuwa ni muuaji kama wazungu waliokuwa wanatawala zimbabwe na afrika kusini. Alishangazwa sana na baadhi ya viongozi wa afrika kumshabikia Amin eti kwa sababu tu aliwafukuza wahindi uganda. ilimkera sana kitendo cha viongozi wa afrika kumpa uenyekiti wa OAU Amin na Uganda kuwa mwenyeji wa kikao cha OAU kwa wakati huo.sikuamini kwani wengi tulio katika kikazi hiki tumeikuta somalia imeshaparaghanyika kumbe wenzenu enzi hizo walikuwa wako sawa hadi wanasuluhisha migogoro ya nchi majirani zao.
 
Pamoja na kuusoma uzi wako mara 2 bado sijakuelewa nani aliyekwambia vita ya kagera ilikua na mazungumzo? Maana jeshi la amin liliingia moja kwa moja na kushambulia kisha jkN ndo akatangaza vita rasmi unaposema kwamba somalia ilisema kila nchi irudishe majesh km 10 nyuma inamaana walikua pua kwa pua?
 
Pamoja na kuusoma uzi wako mara 2 bado sijakuelewa nani aliyekwambia vita ya kagera ilikua na mazungumzo? Maana jeshi la amin liliingia moja kwa moja na kushambulia kisha jkN ndo akatangaza vita rasmi unaposema kwamba somalia ilisema kila nchi irudishe majesh km 10 nyuma inamaana walikua pua kwa pua?

vita 1978. mgogoro ulianza miaka ya mwanzo ya sabini na hapo ndo somalia ilitusuluhisha.
 
Back
Top Bottom