16 Wauwawa kwa Kucharangwa Mapanga Usiku wa Manane-Musoma

Hata DRC hawajauwawa watu 30 ndani ya miezi miwili....japo hakuna amani.
 
.
Kwa Tarime, kuna tatizo, ila pia ni kweli gap kati ya wenye nacho na wasionacho imezidi kukuwa siku hadi siku, itafika wakati wasio nacho, watakata tamaa na kuamua kuwanyang'anya wenye nacho ili wagawane.

Kwanza natoa pole za dhai kwa wananchi wa Musoma waliopata msiba huu, huu ni msiba mkubwa.

Tatizo letu Tanzania ni kuwa badala ya kuangalia chanzo cha tatizo tunaangalia makoteo ya tatizo na kutafutia ufumbuzi. Tatizo kubwa ni tofauti ya wenye navyo na wasionavyo, vinginevyo matukio haya yasingekuwepo.

Mikoa mingine watu wako tolerant, level ya tolerance iko juu kidogo, wenzetu wa Musoma mungu kawabariki level iko low au imeexpire ndio maana wako balistic and sparky wakati wote.

Tusiombee hali hii ije mijini, hapo ndipo Dar Es Salaam itwaitwa Dar Es Balaa. Kinachotusaidia ni kuwa wajanja wa kalamu, mkishen town, udalali, semina na warsha kidogo basi tunasawazisha. Vinginevyo dormant volcan within us inaweza kuwa active wakati wowote.
 
Haka ka Mkoa ka Mara tuwape zawadi jirani zetu (as a sign of goodwill). Just kidding! Duh, jamaa wanahasira kiasi gani hadi kucharangana mapanga? Kesho tutasikia ukoo umelipiza kisasi
 
Oh Lord... si nilisikia wameagiza jeshi kuhamia kabisa huko!?

Mwanakijijijeshi ni panadol tu, hawajawahi kujiuliza maumivu yametokana na nini ili dawa madhubuti ipatikane. Jeshi haliwezi kuondoa njaa kwa wananchi hata kidogo na kanda za kipolisi vilevile sio solution.

The Government should go back to the drawing board, sit with he people and ask them what the problem is Tossi, Mwamyange etc can never be the solution.
 
Jamii ndiyo ilaumiwe kwa kuwekeana visasi visivyokwisha. Serikali itaweka jeshi katika kila kaya jamani ????

We bado upo ktk mila na desturi mwenzetu, watu wanalipa kodi sasa. Serikali ina wajibu wa kuwawekea watu Law and Order. Na si mijitu iamke usiku wa manane kuchukua machetes kwenda kuchinja wenzao.

Obviously kuna sababu kama aikua ujambazi, lakini sidhani hizo sababu zina wahusu au zina eleweka kwa watoto walio chinjwa kama wapo.Hau wahusika wote hapo.

Maswala haya ndio mna wapa watu excuse heti walikua na migogoro ya familia. Migogoro watu hawa chinjani bwana huu ni ushenzi. Ambao vyombo husika vikishindwa fanya kazi yake ujue kazi hawana. Hii hata si mbali hata nchi za africa zimeanza desturi hizi.

kwanza si ndio sehemu hizi wanaua albinos, hawa jamaa wanadhani killings is matter of having a machete only. Something has to be done kuna uzembe huko wa hali ya juu. Kuna migogoro ya kifamilia all over Africa lakini watu hawa chinjani especially the number of victims tunazo sikia.

Huu si mgogoro sasa hila ni vita.
 
,
Tena nadhani ni Tarime, sikumbuki vizuri ni Musoma wapi, kama ni Tarime, huyu DC, Frank Uhahula, kiongozi mstaafu wa Chipukizi nwa CCM akishirikiano na OCD, anachanganya siasa na uongozi kwa kuwachonganisha wana Tarime kuwa fujo zote, mauaji ya koo na wizi wa mifugo vinatokea kwa sababu wameichagua Chadema.

Kwenye kikao cha baraza la madiwani last week, walimfukuza kwenye kikao, wakazuiliwa na kanuni, ili walimpaka sana, na jamaa akajibu mapigo kwa lugha ya ubabe, kuwa yeye anafuata taratibu, sheria na kanuni.

Walimsifu Kamanda Tosi, kikosi chake ndicho angalau kinafanyan kazi bila kuchanganya na siasa.

Hiyo hapo nyeusi si kweli kabisa na ni ushabiki unaotakiwa kutopewa nafasi. Watu wenye mtazamo wa namna hii ama waandishi wa habari wa namna hii sijui tuwaite je?

Kaangalie historia yako upya? je mapigano hayo hayakuwepo hata wakati wa chama kimoja?
Angalia makabila ya huko utakuta na Kenya makabila hayo yapo , na tena kaangalie mapigano yaliyo mipakani ya kabila kati ya kenya na uganda, kati ya kenya na somalia kati ya kenya na sudani kati ya kenya na ethiopia. Na je huko nako wameichagua CHADEMA.?

Mimi nafikiri njia sahihi ni kuacha uzushi nafikiri itakuwa njia sahihi na nguzo mathubuti ya kuindoa ccm.
 
Tarime kuna nini? Naogopa hali hii inayoendelea kutokea Tarime isipozuiliwa na kukemewa kwa nguvu na kila mmoja wetu hizi chuki zinaweza kusambaa nchi nzima, ukizingatiwa hali ilivyo nchini walala hoi wengi wamelowa petrol wanahitaji njiti moja tu ya kiberiti kuanza kuteketezana kati walio nacho na wasio nacho!!
Hiyo wilaya iamishiwe Kenya,huku hapawafai kabisa!
 
Hiyo hapo nyeusi si kweli kabisa na ni ushabiki unaotakiwa kutopewa nafasi. Watu wenye mtazamo wa namna hii ama waandishi wa habari wa namna hii sijui tuwaite je?

Kaangalie historia yako upya? je mapigano hayo hayakuwepo hata wakati wa chama kimoja?
Angalia makabila ya huko utakuta na Kenya makabila hayo yapo , na tena kaangalie mapigano yaliyo mipakani ya kabila kati ya kenya na uganda, kati ya kenya na somalia kati ya kenya na sudani kati ya kenya na ethiopia. Na je huko nako wameichagua CHADEMA.?

Mimi nafikiri njia sahihi ni kuacha uzushi nafikiri itakuwa njia sahihi na nguzo mathubuti ya kuindoa ccm.

Yego Poti,

You are missing the point.

Suala la kuchaguliwa chadema sio maneno ya Pasco bali ni nukuu ya salam za mkuu wa wilaya ya tarime Frank Uhahula.Aliyasema maneno hayo akitoa salam siku ya maadhimisho ya miaka 33 ya ccm, na suala hilo liliibuliwa kwenye kikao cha baraza la madiwani.

Kwahiyo na wewe usitumie mahaba yako kwa ccm kutaka kutudanganya. Tunajua jinsi ccm mnavyotumia mwanya wa tofauti zilizopo kati ya koo za wakurya kujitafutia umaarufu wa bei nafuu. Tunajua mapigano ya tarime yangeweza kukomeshwa kama sio uchochezi unaoendelea kufanywa na na ccm. Kamanda massawe yuko busy kuchoma moto mashamba ya bangi lakini hafanyi lolote la maana kwa ajili ya kulinda usalama wa raia.Tunajua kuwa mmemleta massawe tarime ili kuwasaidia kuiba kura katika uchaguzi mkuu wa octber 2010 lakini jambo moja liko wazi, watu wa tarime watafanya uamuzi wao na kuhakikisha chaguo lao ndiye anakuwa muwakilishi wao.
Nsokili mosani!!!
 
unajua nadhani Jimbo la Nyamagana is becoming more tempting..
Ninakwenda huko inaonekana huyu Mmarekani i mean Masha hana jipya,kanda ya ziwa ndiko anakotoka lakini kanda ya ziwa ndiko kwenye kila aina ya mauaji anzia Maalbino, Bibi vikongwe,Mauaji ya koo ujambazi na uhujumu uchumi unaofanywa na wahindi pale Mwanza mjini.Imetosha kwa Masha ni wakati wa wazawa kuwatumikia wazawa.
 
Yego Poti,

You are missing the point.

Suala la kuchaguliwa chadema sio maneno ya Pasco bali ni nukuu ya salam za mkuu wa wilaya ya tarime Frank Uhahula.Aliyasema maneno hayo akitoa salam siku ya maadhimisho ya miaka 33 ya ccm, na suala hilo liliibuliwa kwenye kikao cha baraza la madiwani.

Kwahiyo na wewe usitumie mahaba yako kwa ccm kutaka kutudanganya. Tunajua jinsi ccm mnavyotumia mwanya wa tofauti zilizopo kati ya koo za wakurya kujitafutia umaarufu wa bei nafuu. Tunajua mapigano ya tarime yangeweza kukomeshwa kama sio uchochezi unaoendelea kufanywa na na ccm. Kamanda massawe yuko busy kuchoma moto mashamba ya bangi lakini hafanyi lolote la maana kwa ajili ya kulinda usalama wa raia.Tunajua kuwa mmemleta massawe tarime ili kuwasaidia kuiba kura katika uchaguzi mkuu wa octber 2010 lakini jambo moja liko wazi, watu wa tarime watafanya uamuzi wao na kuhakikisha chaguo lao ndiye anakuwa muwakilishi wao.
Nsokili mosani!!!

Tarime mapigano yako pale ni mapigano ya kihistoria na kitamaduni hayana uhusiano wowote na siasa. Ila CHADEMA ndo mnajitahidi kuyahusisha na siasa.

Japo kiswahili changu kipo chini ya kiwangu sielewi neno MAHABA unamaanisha nini maana ni tungo tata.

Na hata hivyo manyanga'u wakubwa watapiga sana matarambuta wanatamani manyanga'u wenzao waliokwisha ikamatilia nyama. Nao wanajaribu angalau kutafuta kijimfupa. Tatizo la manyanga'au wa pili wananjaa kubwaa.

Naionea huruma nchi ile kama itawekwa chini ya himaya ya manyang'au hawa wapili wenye njaa kali.
 
jamani taarifa ya habari imeniumiza roho nimebaki na mshangao wa kutokuamini kile kilichotokea ooooh my wanadamu tumekuwa wakatili kupita hata wanyama wakali,wahusika wachukuliwe hatua kali za kisheria ,mungu ziweke roho za marehemu pema peponi amen
 
Tatizo la ujambazi sio geni tangu walipokubali kuhujumu uchumi wa Tanzania na tatizo sio Masha peke yake tatizo ni Chama Cha Majambazi na serikali inayoongozwa na Jakaya Kikwete - kwishnei.
 
Tatizo la ujambazi sio geni tangu walipokubali kuhujumu uchumi wa Tanzania na tatizo sio Masha peke yake tatizo ni Chama Cha Majambazi na serikali inayoongozwa na Jakaya Kikwete - kwishnei.

Kaka haya mauaji hayahusiani kabisa na ujambazi ni ujinga na ushenzi wa binaadam wa mkoa wa Mara, maana haya mambo yanatokea huko tu na si mahala popote pale Tanzania, ingelikua kuna possibility ya kuuza mkoa basi MARA unatakiwa kuuzwa tena kwa mkopo kama Michael Owen.. MKOA WA MARA UNATIA AIBU SAAAAAAAAANA WATANZANIA, najuuta kuwa Mtanzania because of this region
 
Msingi wa amani katika jamii ni haki; na msingi wa kuishi kwa mapatano ni kujua kuwa kuna usawa. Wakati wowote kikundi chochote cha jamii ya watu kinapojiona kuwa aidha hakina haki au hakina usawa basi mara zote hakiwezi kuishi kwa amani. Hivyo utaona kuwa suluhisho la kweli la kuleta amani ya kweli ni kuleta haki na usawa wa kweli.

Sasa haki na usawa haviwezi kulazimishwa juu ya wote kwa kutumia nguvu. Hata hivyo uwepo wake unaweza kutengenezwa kwa kutumia nguvu. Sasa ningekuwa mimi ningefanya yafuatayo to pacify Tarime.. wanasema extraordinary situations demand extraordinary measures...
 
Kaka haya mauaji hayahusiani kabisa na ujambazi ni ujinga na ushenzi wa binaadam wa mkoa wa Mara, maana haya mambo yanatokea huko tu na si mahala popote pale Tanzania, ingelikua kuna possibility ya kuuza mkoa basi MARA unatakiwa kuuzwa tena kwa mkopo kama Michael Owen.. MKOA WA MARA UNATIA AIBU SAAAAAAAAANA WATANZANIA, najuuta kuwa Mtanzania because of this region

Acha kutukashifu.
 
Inasikitisha sana, inaumiza roho mno!...na polisi wanasema (watu wasio fahamika na wakti huo huo wanasema huenda ikawa mauaji ya kulipiza kisasi, kauli mbili zinazopingana!....

Mara nyingi kwa kuzingatia kuwa Mwalimu alitokea Mkoa huu wa Mara wenye kila aina ya vitendo visivyo vya kibinadamu, napata shaka sana kuamini kama kweli Mwalimu aliongoza hii nchi kwa mfumo uliosawa na alimuia iwe ya amani kwa misingi ya kuondoa kila aina ya vichocheo vya uhasama kama ukabila, udini, rangi, na Itikadi...Kama Mwalimu huyu tunayemuezni kwa kupenda amani aliweza kuwa "depoti" wahujumu uchumi na waliopinga maendeleo na kuleta chuki (makabaila, Makupe, Mabepari, Vingunge na Mabwenyenye), kwa nini hakufanya hivyo kwa kuwasambaza hawa watu wa kwake ili wakajichanganye na makabila mengine wajue ustaarabu wa kiutu?...

Hii amani aliyokuwa anaihubiri Mwalimu kwa mataifa mengine duniani ambayo haionekani katika eneo alilolazwa yeye mwenyewe imezimikia wapi?....Kama alituma majeshi kwenda kulinda amani nchi za wenzetu, kwa nini huko Mara hakukuwekwa kituo maalumu cha Ulinzi wa Amani na Kufundisha Ustaarabu kwa Watu wake ambao chuki na uhasama vipo kwenye damu?...

Na hata hivi sana, baada ya miaka 10 ya kifo cha "Mwenyeheri Julius Kambarage Nyerere," kwa nini wale wanaodai majukwaani "tunamuenzi Mwalimu" na kuanzisha mchakato wa kumtambua kuwa Mtakatifu, wameshindwaje kuwasaidia hawa watu wake wasichinjane kama Sungura juu ya ardhi aliyozikwa Mwalimu?....Hii ni makasudi na aibu kubwa kwa Taifa iwapo Mara ardhi ambayo mwasisi wa taifa hili linaamani mkubwa dunainai na wametoka pia Makamanda wa Jeshi letu la Wanachi la Ulinzi linaloheshimia pia dunian kwa ulinzi wa amani alktkumbe katika mihimili ya milango yao, mapigao yameshindwa kudhibitiwa...

Mungu Ibariki Tanzania, Wabariki Viongozi Wake....
 
Back
Top Bottom