JF Kuwa Chama Tishio Cha Siasa?

Jamiiforums Kugeuzwa Chama?

  • Yawezekana

    Votes: 44 71.0%
  • Haiwezekani

    Votes: 19 30.6%

  • Total voters
    62
  • Poll closed .

Sura-ya-Kwanza

JF-Expert Member
Nov 17, 2007
566
10
Duku duku zinazoenakana ndani ya Jamboforums (JamiiForums) ni kwamba itaweza kuwa Chama cha Upinzani 2010!

Wachunguzi wamebaini kwamba wanachama machachari wa Upinzani na hata Chama tawala wameona kiunganishi hichi ambamo wanaweza kuweka bayana yanayowagusa Wananchi na kuchambua kwa uwazi ni kigezo kizuri cha kuendesha shughuli za bunge!

Mpaka naenda mtamboni huu ni uzushi tuu lakini Yawezekana?.
 
Wanamageuzi wa karne ya ishirini na moja wameona kutumia njia hii ya mawasiliano sio tu kutawasogesha karibu na wananchi bali wanaweza Kuwaelimisha na hata kuwahamasisha Wananchi katika kujijumuisha katika majidiliano ambayo kwa namna moja au nyingine zinaleta changamoto sio tu kwa Wananchi na waandishi wa habari bali serikali au chama kilicho tukutu kwa wakati!:rolleyes:

Kwa mantiki hii... Sio siri kuona chombo kama cha, JF kinageuzwa kama chombo cha siasa, katika karne ya 22

Mfumo uliyojitokeza JF sio simulizi! Mijadala, Hoja, Maandiko, Udaku,[sijaona ngonjera hapa] Kwi !!! Wakubwa na vioja vyao, Kwa namna moja au nyingine ni mambo mbadao, lakini bado ni Simulizi ya miandiko ,mijadala na hoja za mambo mbadao ambayo inategemewa kuwa vigezo,nguzo na hata mielekeo ya wanaharakati wa JF katika muundo wa miongozo ya karne ya 22!
Siasa endelevu ya karne ya 22 ndio teke-linalo-fuata! nafikiri, hii ni; Sababu moja yapo, itakayoweza kuleta maadhimio ya ukumbi huu kama ni kweli- itaunda Chama!

Sitasita kuweka viongozi wenye kuunda chama hichi kwa nyanja zao kama itanibidi!

Kada-Mpinzani: Stop snuggling!,kalaga bao u-ubete uhulu
Mwanakijiji:Una hoja hapo!
Mtoto wa mkulima:Utaendelea kulima au? lete mdahalo!
YAWEZEKANA!
 
Kweli Invisible, week end imeanza ingawa inaanza vibaya!

Watu wanoona kama Sura ya kwanza and company ambaye naamini si junior member bali amejisajili ili kutoa dukuduku lake (na huu ni uoga) ni bora watulie kuliko kujaribu kui-undergrade JF kwa maslahi yao.
 
Kwa kadri ninavyochukia dhana na mifumo ya vyama vya siasa na siasa zenyewe (kama zilivyo na zinavyoendeshwa Bongo), naanza kukusanya virago vyangu kuondoka humu kama kweli jambo hili litaonesha dalili zozote kudhihirika hapo baadae!!!
Wikisha njema!
 
Kweli Invisible, week end imeanza ingawa inaanza vibaya!

Watu wanoona kama Sura ya kwanza and company ambaye naamini si junior member bali amejisajili ili kutoa dukuduku lake (na huu ni uoga) ni bora watulie kuliko kujaribu kui-undergrade JF kwa maslahi yao.
Company yangu ni ya walala hoi! Sina lolote la kui-undergrade JF(sina formula)!
Ngao: Mimi nafikiri wewe ndio muoga wa kuwepo kwenye Jahazi kama kweli itatokea. "What happens is not as important as how you react to what happens.!!"
Na Ibrah-Kuna baadhi za thread ambamo tunaona wale wanaojuana kutupiana madongo badala ya kukata Hoja! Kuuliza kama Jamboforum Kugeuzwa kuwa chama ina madhara gani? Naafikiri kama nilisoma vizuri maadhimio ya J.F ni kuleta changamoto na kuona kama yanaweza kufanyiwa mabadiliko,uchunguzi,uhakiki na Kwk... Na hii Where we Dare Talk Openly itakuwa na maana gani kama wana JF hataweza kuuliza hili JF? Naamini wamo watu wengi tu watukutu wa Tanzania na Nchi nyingine ambao wameshafika hapa na kutoa dukuduku zao! Zingine mbaya tu kama kumsema vibaya Raisi wa nchi!
Je Hili ili "kui-undergrade" JF?
Weekend Njema tu!
 
Kwa kadri ninavyochukia dhana na mifumo ya vyama vya siasa na siasa zenyewe (kama zilivyo na zinavyoendeshwa Bongo), naanza kukusanya virago vyangu kuondoka humu kama kweli jambo hili litaonesha dalili zozote kudhihirika hapo baadae!!!
Wikisha njema!

Duuh, hivi 'weekend' ndiyo 'wikisha' siku hizi, hii itakuwa poa sana kama inakubalika... lol

SteveD.
 
Kuuliza Si Ujinga Hata Kidogo
Umefanya Vizuri Kumbuka Uoga Si Mbinu Ya Mapambano Japo Wasukuma Wanasema Kaya Ya Ng`hoba Nayo Kaya(nyumba Ya Mwoga Nayo Nyumba)
Ng`wananogu
 
Yangu Macho...exhilarating

*"Shukrani za pekee na pongezi ziwaendee waandishi wa habari na vyombo vyao walioweka maslahi binafsi pembeni na kupiga kelele kwa nguvu zao zote kuhusu mwenendo uliokuwa hauridhishi wa mchakato wa zabuni ya umeme wa dharura."

*"Vilevile shukrani zetu ziende kwa Watanzania na watu wote wenye nia njema na nchi hii waliotuunga mkono kwa kutupa taarifa mbalimbali, maoni kwa njia ya barua pepe, simu n.k."


JamboForums...Reckon with!
Detest your Adversaries and rekindle!
*:source Issamichuzi
 
Best iwe njia ya kuvisafisha na kujenga Institutions zingine kwa kuweka mambo wazi na kurecruit wachapa kazi.

Sidhani nchi inahitaji vyama vingine vya siasa. Afadhali hivyo vilivyopo vifanyiwe mageuzi mle mle ndani kazi nzuri zifanyike. Mpo hapo?

Kazi ya sasa ya BoT, Richmond, Kiwira, Madini - plus hawa wote walio culprits more presure is needed so that they face full force of the law - ili iwe fundisho. Jambo forum can play crucial role kuyaanika hayo na akina Mwakyembe wayaone na tuone sasa kama Sita atasema tena "emails zisizojulikana" aliposema kukejeli ile email ya kwanza iliosomwa bungeni...

Hivyo waugwana - JF isiende kuwa chama cha siasa, italoose focus. Ila kidemokrasia kama watu wanataka huwezi zuia - hivyo basi JF iwe kama platform ya kuzaa hizo groups au vyama. Lakini narudi ushauri wangu ni kuwa isiwe chama cha siasa.
 
Best iwe njia ya kuvisafisha na kujenga Institutions zingine kwa kuweka mambo wazi na kurecruit wachapa kazi. ....Sidhani nchi inahitaji vyama vingine vya siasa. Afadhali hivyo vilivyopo vifanyiwe mageuzi mle mle ndani kazi nzuri zifanyike. Mpo hapo?
.......Lakini narudi ushauri wangu ni kuwa isiwe chama cha siasa.

Taasisi Za siku mkuu na pia nimefurahi "kukuona", nadhani bado tunakuhitaji ili uwe unashusha nondo zako hapa kwani zinahitajika sana.

Ulivyosema ni kweli vyama vya siasa tunavyo vingi, ila JF ni vyema itumike kama chachizo kwa vyama vilivyopo. Na ikiwezekana iundwe taasisi isiyo ya kiserikali ambayo itakemea rushwa, ubadhirifu na ufisadi bila kufungamana na chama chechote kile, iwe CCM, Chadema, TLP, NCCR nk.
 
Yangu Macho...exhilarating

*"Shukrani za pekee na pongezi ziwaendee waandishi wa habari na vyombo vyao walioweka maslahi binafsi pembeni na kupiga kelele kwa nguvu zao zote kuhusu mwenendo uliokuwa hauridhishi wa mchakato wa zabuni ya umeme wa dharura."

*"Vilevile shukrani zetu ziende kwa Watanzania na watu wote wenye nia njema na nchi hii waliotuunga mkono kwa kutupa taarifa mbalimbali, maoni kwa njia ya barua pepe, simu n.k."


JamboForums...Reckon with!
Detest your Adversaries and rekindle!
*:source Issamichuzi


Sio vibaya nikaji-kuoti hapa...

Detest your Adversaries and rekindle!
 
Tumesikitishwa Sana . . . .
Tumenyanyaswa Sana . . .
Tumeonewa Sana . . . .

Hakuna wa kututetea kikamilifu ndani ya Chama Tawala . . . .
Upinzani nao bado unasua sua na hauna mwelekeo wa kushika hatamu . . . .

Sasa kwa hiari yetu tumeamua kuanzisha Chama Cha Kisiasa, kitakachoshika Madaraka ya Kuongoza Serikali Mwaka 2015 . . .

Rev. Kishoka . . . . tunaomba uanze kuandika rasimu ya katiba kisha tuletee hapa jamvini tuipitie . . . .

Mwanakijiji . . . . anza kutayarisha rasimu ya Ilani ya Uchaguzi

Kuhani . . . . Anza kuchambua chambua weaknesses za vyama vyote vya Kisiasa . . . .

Wana JF Wooote . . . . Tuanze kujiandaa kufanya kweli . . . . .

Tunahitaji mchango wa kila mwana JF ni nini hasa tufanye ili tufanikiwe kuunda Serikali Mwaka 2015 . . . . .
 
Tumesikitishwa Sana . . . .
Tumenyanyaswa Sana . . .
Tumeonewa Sana . . . .

Hakuna wa kututetea kikamilifu ndani ya Chama Tawala . . . .
Upinzani nao bado unasua sua na hauna mwelekeo wa kushika hatamu . . . .

Sasa kwa hiari yetu tumeamua kuanzisha Chama Cha Kisiasa, kitakachoshika Madaraka ya Kuongoza Serikali Mwaka 2015 . . .

Rev. Kishoka . . . . tunaomba uanze kuandika rasimu ya katiba kisha tuletee hapa jamvini tuipitie . . . .

Mwanakijiji . . . . anza kutayarisha rasimu ya Ilani ya Uchaguzi

Kuhani . . . . Anza kuchambua chambua weaknesses za vyama vyote vya Kisiasa . . . .

Wana JF Wooote . . . . Tuanze kujiandaa kufanya kweli . . . . .

Tunahitaji mchango wa kila mwana JF ni nini hasa tufanye ili tufanikiwe kuunda Serikali Mwaka 2015 . . . . .

Mmmh...! Wasi wasi wangu ni mmoja tu... Hicho chama kama hakitakuwa na UDINI basi Mwisho wa Dunia umefika...! Yaani itakuwa imebaki siku moja dunia Kuangamia...!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom