Mbunge wa Musoma kuwasha moto kuhusu milki ya mgodi wa Buhemba

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,006
Niliwahi kusikia kwamba Kigoda alipokuwa Waziri katika sirikali ya Mkapa alikuwa akipita nchi mbali mbali za magharibi kutafuta makampuni ya uchimbaji wa dhahabu yaingie mkataba na yeye na Mkapa wa kuchimba dhahabu katika "mgodi wao wa dhahabu". Isije ikawa huu wa Buhemba ndio mgodi "wao"

Posted Date::4/12/2008
Mbunge wa Musoma kuwasha moto kuhusu milki ya mgodi wa Buhemba
* CAG akiri, asema si mgodi wa serikali
* Waziri Ngeleja asema apatiwe muda

Na Mkinga Mkinga
Mwananchi

SUALA la umiliki wa mgodi wa dhahabu wa Buhemba mkoani Mara, limechukua sura mpya, baada ya Mbunge wa Musoma vijijini, Nimrod Mkono kuamua kupeleka bungeni hoja binafsi kupata maelezo ya kina, kuhusu nani anayemiliki mgodi huo.

Akizungumza na Mwananchi Jumapili katika mahojiano maalum, Mkono alisema atahitaji kupata maelezo yanayojitosheleza hasa baada ya kuonekana, serikali si mmiliki wa mgodi wa Buhemba kutokana na maelezo ya Mdhibiti Mkuu na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG), na msajili wa asasi za serikali.

Mkono alisema amekuwa akiipeleka hoja hiyo bungeni mara kadhaa, lakini imekuwa ikikosa mtu wa kutoa ufafanuzi wa nani mmiliki wa mgodi huo, ambao ulikuwa chini ya Kampuni ya Meremeta, kampuni ambayo imekuwa ikipigiwa kelele na wapinzani katika masuala ya ufisadi.

Majuzi hapa wakati wa mkutano wa asasi zote, CAG ameulizwa kuhusu Buhemba, akasema hajapata taarifa zozote za mgodi huo wala hajawahi kupitia hesabu zake, na wala hajui kama ni mgodi wa serikali, alisema Mkono.

Mbunge huyo alisema kwa kipindi kirefu sasa kumekuwa na utata wa umiliki wa mgodi huo wa Buhemba, huku taarifa za awali zikionyesha kuwa mgodi huo ulikuwa unamilikiwa na Kampuni ya Meremeta, ambayo inamilikiwa na serikali.

Wananchi pamoja na mimi tumekuwa tukiambiwa kuwa mgodi huo ni wa serikali, lakini kwa mujibu wa CAG, pamoja na msajili wa asasi za umma walisema, kampuni hiyo haimo katika orodha ya makampuni ya asasi za umma kama ilivyokuwa inasemekana, alisema Mkono.

Ninachotaka kusema ni kwamba hapa lengo sio majungu, ila kama Mbunge wa Musoma Vijijini ambako mgodi huo upo anahitaji kujua, ili wananchi wangu pia niwafahamishe kuhusu umiliki halali wa mgodi huo, alisema Mkono.

Alisema utata huo wa umiliki wa mgodi wa Buhemba, umezidi kuwa mkubwa ambapo sio yeye wala wananchi ambao walifahamishwa kuwa mgodi huo ulikuwa unamilikiwa na nani.

Mkono aliongeza kuwa, kitendo cha kuchimba madini ya dhahabu yaliyokuwa yanapatikana katika mgodi huo, kwa kutumia jina la serikali, ni sawa na kuisaliti nchi na kuiba maliasili zake.

Mbunge huyo wa Musoma Vijijini alisema, mabilioni ya fedha yametumika katika kuimarisha mgodi huo, hata baada ya kuanza uzalishaji wa dhahabu si serikali wala wananchi ambao wamefaidika na uchimbaji madini huo.

Mabilioni ya shilingi hapa yametafunwa, huu ni ufisadi, maana kama hizo za EPA zimeundiwa task force committee kwa nini hapa pia pasiundiwe tume, alisema Mkono.

Kwa mujibu wa mbunge huyo inakadiriwa kuwa zaidi ya Sh 180 bilioni zimetafunwa kupitia mgodi huo, fedha ambazo zingeweza kuwafaidisha wananchi katika mambo mengine ya maendeleo.

Alisema kinachoendelea kushangaza wananchi wa jimbo lake ni kwamba, mpaka sasa askari wa jeshi la polisi bado wanaendelea kulinda katika eneo hilo la Mgodi wa Buhemba, wakati imefahamika kwamba serikali si mmiliki wa mgodi huo.

Katika hatua nyingine, Mkono alisema amefikisha malalamiko yake katika Tume ya Rais ya kupitia upya mikataba ya madini iliyoko chini ya Jaji mstaafu Mark Bomani na kwamba sasa anasubiri utekelezaji.

Wakati kamati ya Rais inayoshughulikia madini ilipotembelea mgodi huo, niliwaambia masuala kadhaa yenye utata hapo Buhemba, bila shaka watayafikisha kunakohusika, alisema mbunge huyo.

Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Heasbu za Serikali, Ludovick Utouh, alipoulizwa na Mwananchi Jumapili jana, alisema ni kweli kwamba katika orodha ya makampuni ya umma 158, kampuni iliyotajwa kumiliki mgodi huo si miongoni mwa makapuni ya umma.

Ninachokifahamu na nilichomueleza Mbunge wa Musoma vijijini, Nimrod Mkono ni kwamba katika orodha ya makampuni 158, ninayoyakagua hilo halimo, alisema CAG.

CAG alitaka maswali zaidi yaelekezwe kwa msajili aliyeko hazina, kwa madai kuwa anaweza kuwa na majibu mazuri zaidi ya hilo, na kwamba yeye ndiye mwenye mamlaka na asasi za serikali.

Naye Waziri wa Nishati na Madini, Wiliam Ngeleja alipotakiwa kutoa ufafanuzi wake jana na msimamo wa serikali katika utata uliogubika mgodi wa Buhemba alisema jambo hilo linahitaji takwimu zaidi.

Jambo hili linahitaji takwimu zaidi halafu mimi sipo ofisini, tafadhali hebu wasilianeni na Kamishna wa Madini, atakuwa anafahamu zaidi, alisema waziri Ngeleja.

Aliongeza kuwa suala hilo linahitaji kujiandaa zaidi na kwamba yeye atamuagiza kamishna huyo wa madini atoe ufafanuzi kwa gazeti hili.

Suala la utata wa mgodi wa Buhemba limedumu kwa muda mrefu sasa, takribani miaka mitano, na kwamba mwishoni mwa mwaka jana wapinzani waliinyoshea kidole serikali kuhusu umiliki wake wa mgodi huo.

Mgongano huo pia, ulisababisha Mbunge wa Musoma vijijini, Nimrod Mkono kukataa kupokea kiasi cha sh 200 milioni kama mrabaha kwa wilaya hiyo, kwa madai kuwa haikuwa inaendana na kile kinachovunwa katika ardhi hiyo. Juhudi za Kumtafuta Kamisha wa Madini jana hazikuzaa matunda.
 
Niliwahi kusikia kwamba Kigoda alipokuwa Waziri katika sirikali ya Mkapa alikuwa akipita nchi mbali mbali za magharibi kutafuta makampuni ya uchimbaji wa dhahabu yaingie mkataba na yeye na Mkapa wa kuchimba dhahabu katika "mgodi wao wa dhahabu". Isije ikawa huu wa Buhemba ndio mgodi "wao"

Posted Date::4/12/2008
Mbunge wa Musoma kuwasha moto kuhusu milki ya mgodi wa Buhemba
* CAG akiri, asema si mgodi wa serikali
* Waziri Ngeleja asema apatiwe muda

Na Mkinga Mkinga
Mwananchi



SUALA la umiliki wa mgodi wa dhahabu wa Buhemba mkoani Mara, limechukua sura mpya, baada ya Mbunge wa Musoma vijijini, Nimrod Mkono kuamua kupeleka bungeni hoja binafsi kupata maelezo ya kina, kuhusu nani anayemiliki mgodi huo.

Akizungumza na Mwananchi Jumapili katika mahojiano maalum, Mkono alisema atahitaji kupata maelezo yanayojitosheleza hasa baada ya kuonekana, serikali si mmiliki wa mgodi wa Buhemba kutokana na maelezo ya Mdhibiti Mkuu na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG), na msajili wa asasi za serikali.

Mkono alisema amekuwa akiipeleka hoja hiyo bungeni mara kadhaa, lakini imekuwa ikikosa mtu wa kutoa ufafanuzi wa nani mmiliki wa mgodi huo, ambao ulikuwa chini ya Kampuni ya Meremeta, kampuni ambayo imekuwa ikipigiwa kelele na wapinzani katika masuala ya ufisadi.

Majuzi hapa wakati wa mkutano wa asasi zote, CAG ameulizwa kuhusu Buhemba, akasema hajapata taarifa zozote za mgodi huo wala hajawahi kupitia hesabu zake, na wala hajui kama ni mgodi wa serikali, alisema Mkono.

Mbunge huyo alisema kwa kipindi kirefu sasa kumekuwa na utata wa umiliki wa mgodi huo wa Buhemba, huku taarifa za awali zikionyesha kuwa mgodi huo ulikuwa unamilikiwa na Kampuni ya Meremeta, ambayo inamilikiwa na serikali.

Wananchi pamoja na mimi tumekuwa tukiambiwa kuwa mgodi huo ni wa serikali, lakini kwa mujibu wa CAG, pamoja na msajili wa asasi za umma walisema, kampuni hiyo haimo katika orodha ya makampuni ya asasi za umma kama ilivyokuwa inasemekana, alisema Mkono.

Ninachotaka kusema ni kwamba hapa lengo sio majungu, ila kama Mbunge wa Musoma Vijijini ambako mgodi huo upo anahitaji kujua, ili wananchi wangu pia niwafahamishe kuhusu umiliki halali wa mgodi huo, alisema Mkono.

Alisema utata huo wa umiliki wa mgodi wa Buhemba, umezidi kuwa mkubwa ambapo sio yeye wala wananchi ambao walifahamishwa kuwa mgodi huo ulikuwa unamilikiwa na nani.

Mkono aliongeza kuwa, kitendo cha kuchimba madini ya dhahabu yaliyokuwa yanapatikana katika mgodi huo, kwa kutumia jina la serikali, ni sawa na kuisaliti nchi na kuiba maliasili zake.

Mbunge huyo wa Musoma Vijijini alisema, mabilioni ya fedha yametumika katika kuimarisha mgodi huo, hata baada ya kuanza uzalishaji wa dhahabu si serikali wala wananchi ambao wamefaidika na uchimbaji madini huo.

Mabilioni ya shilingi hapa yametafunwa, huu ni ufisadi, maana kama hizo za EPA zimeundiwa task force committee kwa nini hapa pia pasiundiwe tume, alisema Mkono.

Kwa mujibu wa mbunge huyo inakadiriwa kuwa zaidi ya Sh 180 bilioni zimetafunwa kupitia mgodi huo, fedha ambazo zingeweza kuwafaidisha wananchi katika mambo mengine ya maendeleo.

Alisema kinachoendelea kushangaza wananchi wa jimbo lake ni kwamba, mpaka sasa askari wa jeshi la polisi bado wanaendelea kulinda katika eneo hilo la Mgodi wa Buhemba, wakati imefahamika kwamba serikali si mmiliki wa mgodi huo.

Katika hatua nyingine, Mkono alisema amefikisha malalamiko yake katika Tume ya Rais ya kupitia upya mikataba ya madini iliyoko chini ya Jaji mstaafu Mark Bomani na kwamba sasa anasubiri utekelezaji.

Wakati kamati ya Rais inayoshughulikia madini ilipotembelea mgodi huo, niliwaambia masuala kadhaa yenye utata hapo Buhemba, bila shaka watayafikisha kunakohusika, alisema mbunge huyo.

Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Heasbu za Serikali, Ludovick Utouh, alipoulizwa na Mwananchi Jumapili jana, alisema ni kweli kwamba katika orodha ya makampuni ya umma 158, kampuni iliyotajwa kumiliki mgodi huo si miongoni mwa makapuni ya umma.

Ninachokifahamu na nilichomueleza Mbunge wa Musoma vijijini, Nimrod Mkono ni kwamba katika orodha ya makampuni 158, ninayoyakagua hilo halimo, alisema CAG.

CAG alitaka maswali zaidi yaelekezwe kwa msajili aliyeko hazina, kwa madai kuwa anaweza kuwa na majibu mazuri zaidi ya hilo, na kwamba yeye ndiye mwenye mamlaka na asasi za serikali.

Naye Waziri wa Nishati na Madini, Wiliam Ngeleja alipotakiwa kutoa ufafanuzi wake jana na msimamo wa serikali katika utata uliogubika mgodi wa Buhemba alisema jambo hilo linahitaji takwimu zaidi.

Jambo hili linahitaji takwimu zaidi halafu mimi sipo ofisini, tafadhali hebu wasilianeni na Kamishna wa Madini, atakuwa anafahamu zaidi, alisema waziri Ngeleja.

Aliongeza kuwa suala hilo linahitaji kujiandaa zaidi na kwamba yeye atamuagiza kamishna huyo wa madini atoe ufafanuzi kwa gazeti hili.

Suala la utata wa mgodi wa Buhemba limedumu kwa muda mrefu sasa, takribani miaka mitano, na kwamba mwishoni mwa mwaka jana wapinzani waliinyoshea kidole serikali kuhusu umiliki wake wa mgodi huo.

Mgongano huo pia, ulisababisha Mbunge wa Musoma vijijini, Nimrod Mkono kukataa kupokea kiasi cha sh 200 milioni kama mrabaha kwa wilaya hiyo, kwa madai kuwa haikuwa inaendana na kile kinachovunwa katika ardhi hiyo. Juhudi za Kumtafuta Kamisha wa Madini jana hazikuzaa matunda.


Hivi Mukono anaunganishwa wapi vile na Ufisadi ? Ni migodi ama BoT ?Je anaweza kufanya haya anayo yasema ama anasema ili tusikie yupo ? Maana CCM bwana . Hivi Masha na ile kesi yake dhidi ya gazeti moja nchini imesha fuguliwa ? Kama ndiyo mbele ya Jaji nani ama kesi namba ngapi ? Inasikilizwa lini ?
 
mimi nafikiri kuna wenye nchi na serikali ambao serikali na utawala uliopo hauwezi kuwagusa wala kuwanyooshea kidole.mafisadi
 
Huyu Mkono anajaribu kujikosha tu mbele ya wapiga kura wake ili a divert attention kutoka kwenye kashfa za ufisadi alizohusishwa nazo. Kama angekuwa na busara angesubiri ripoti ya Kamati ya Madini kwanza.
 
Huyu Mkono anajaribu kujikosha tu mbele ya wapiga kura wake ili a divert attention kutoka kwenye kashfa za ufisadi alizohusishwa nazo. Kama angekuwa na busara angesubiri ripoti ya Kamati ya Madini kwanza.

Kana ka Nsungu kansungu Mwelu, huyu bado yuko kwenye kundi la mafisadi baada ya kulipwa bilioni nane na BoT ambazo hadi hii leo haijulikani zilikuwa zinahusiana na kazi gani aliyoifanya pale BoT. Wakati huo huo tumwache atufumbue macho kuhusiana na ufisadi mwingine pale Buhemba ambapo Watanzania tulikuwa tunajua ni mgodi wa SIRI KALI kumbe sivyo! Wajanja wachache walishajimilikisha! Je, ni nani aliyehusika katika kuwamilikisha mgodi huu? Ni nani hao wanaomiliki mgodi huu, na wanaumiliki tangu lini? Je wizara ya madini ilikuwa inafahamu kwamba mgodi huu si wa siri kali? Kama jibu ni ndio, kwanini wizara iliamua kukaa kimya? Je ni migodi mingine mingapi ya dhahabu au madini mengine yeyote Tanzania ambayo haimilikiwi na SIRI KALI wakati Watanzania tunadhani ni ya siri kali?
 
richimod aina mwenyewe,
EPA aina mwenyewe,
buhemba aina mwenyewe,
Gorofa lilioanguka pale changombe alikuwa na mwenyewe,
Dawoson aina mwenyewe,

Hapa nakumbukia shamba la babu.
 
Mkisha vunja miiko hakuna kurudi nyuma.

Mkono gandamiza mkono wako hapo hapo mpaka uchungu na uatamu vichanganikane huku wewe mwenyewe ukisubiri kikombe cha maovu yako.
 
hili treni linaenda kwa kasi sana na kila mwenye akili timamu bora adandie hata kama ni lile behewa la mwisho; muda si mrefu mtasikia Rostam naye anabomu la kulipua!

Mafisadi wanapojaribu kujisafisha kwa kuwanyoshea mikono mafisadi wengine, basi ufisadi wao ndio humulikwa zaidi. Nimrodulikuwa wapi siku hizi zote?
 
Nimrod ananikumbusha ile hadithi ya kwetu.
Natega mtego wangu wa kwale, namnasa kwale alonona, mwenyewe namnyonyoa na kumwosha vizuri kisha nimweka mbaniko kwenye mti na kumchoma.

Akiwa karibu kuiva mbwa wangu aja amla mzima mzima kwa paffu moja.

Kwa hasira nachukua rundo la majani makavu na kuufungia mkia wa mbwa nayamwagia mafuta ya taa na kuyawasha moto ili nimkomeshe mbwa kwa wizi wake.

Mbwa anatimua mbio na kujitoma kwenye shamba la mpunga uliokomaa kwa ukali na uchungu wa moto.

Mpunga unashika moto,Shamba langu na ya majirani yote yanateketea.

Kwale namkosa na mpunga shambani naukosa huku nikizua uhasama mzito na majonzi kutoka kwa majirani zangu.

Akili nyingine zina ujinga mwingi ndani.
 
:) :) Madela-wa-Madilu, ahsante kwa hadithi... i'm luvin it, quite authentic.... lol
 
hili treni linaenda kwa kasi sana na kila mwenye akili timamu bora adandie hata kama ni lile behewa la mwisho; muda si mrefu mtasikia Rostam naye anabomu la kulipua!

Mafisadi wanapojaribu kujisafisha kwa kuwanyoshea mikono mafisadi wengine, basi ufisadi wao ndio humulikwa zaidi. Nimrodulikuwa wapi siku hizi zote?

Itakuwa safi sana kama Rostam akiamua ama kuitisha kikao na waandishi wa habari na kuwapa data zote za aliyotaka kuyasema ndani ya Bunge au akaandika na kuyatuma kwenye magazeti, Radio na TV za bongo. Hapo ndio itakuwa mwanzo wa mwisho wa CCM kama tunavyoijua.

Haingii akilini eti Sitta kamnyima ruhusa ya kuongea bungeni ili kulinda hadhi ya CCM, what about crebility of our beloved country....Ooops! I forgot that mafisadi they are always more concerned about the credibility of Chama Cha Mafisadi as compared to credibility of Tanzania.
 
Rostam hana data asiwadanganye mtu; data humwaga JF kwanza...huko Bungeni wanapata mwisho wake tu; kama anazo na anaamini zinaweza kumsafisha anajua pa kuzipeleka.
 
Nimrod anajitayarisha na EPA report!! Lazma afe na mtu!! Jamani watetezz wa CCM ningewashauri muwatose viongozi wenu na muunde CCM-Z (Zalendo)..break out now before its too late..kuna wengine hata hela za ufisadi bado hamjanusa na chama kinavunjika..ji sevuni mapema!!
 
Rostam hana ubavu wa kukaa mbele ya waandishi wa habari kwa sababu mambo anayotakiwa kuyatolea ufafanuzi ni mengi na mazito mno kuliko utetezi alionao
 
Madela-wa-Madilu, shabash!!!! Kula tano Mkuu manake umegusa panapo penye Mkuu..... Leave alone ile ya kumwondoa Mzee wa Tarabushi kama Lawyers wa BOT.....

Watatajana wote hawa wakuu na mwishoni lazima kidole kitabakia kwa mmoja swali ni yupi!!! Huyo ndiye tutaanza naye kisha tuwarudie wao!!
 
Nimrod ananikumbusha ile hadithi ya kwetu.
Natega mtego wangu wa kwale, namnasa kwale alonona, mwenyewe namnyonyoa na kumwosha vizuri kisha nimweka mbaniko kwenye mti na kumchoma.

Akiwa karibu kuiva mbwa wangu aja amla mzima mzima kwa paffu moja.

Kwa hasira nachukua rundo la majani makavu na kuufungia mkia wa mbwa nayamwagia mafuta ya taa na kuyawasha moto ili nimkomeshe mbwa kwa wizi wake.

Mbwa anatimua mbio na kujitoma kwenye shamba la mpunga uliokomaa kwa ukali na uchungu wa moto.

Mpunga unashika moto,Shamba langu na ya majirani yote yanateketea.

Kwale namkosa na mpunga shambani naukosa huku nikizua uhasama mzito na majonzi kutoka kwa majirani zangu.

Akili nyingine zina ujinga mwingi ndani.


Madiluuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu hakika you have made my Sunday noon.Nimecheka hata jamaa kwenye cafe kanitolea macho na kuomba maji ya kunywa .Asante sana kwa maneno na mfano huu mzito .
 
Itakuwa safi sana kama Rostam akiamua ama kuitisha kikao na waandishi wa habari na kuwapa data zote za aliyotaka kuyasema ndani ya Bunge au akaandika na kuyatuma kwenye magazeti, Radio na TV za bongo. Hapo ndio itakuwa mwanzo wa mwisho wa CCM kama tunavyoijua.

Haingii akilini eti Sitta kamnyima ruhusa ya kuongea bungeni ili kulinda hadhi ya CCM, what about crebility of our beloved country....Ooops! I forgot that mafisadi they are always more concerned about the credibility of Chama Cha Mafisadi as compared to credibility of Tanzania.

The last few weeks kama si days we all said kwamba JK na CCM yao kwao Tanzania si ya kwanza bali ni ya pili baada ya CCM yao na labda madaraka then Tanzania .They have proved it again .Nashangaa double standard za Sitta ikifikia kwenye CCM yake .Wale mliopinga majuzi mko wapi ?
 
Waungwana huyo Mkono aliyesema atawasha moto Bungeni kuhusiana na umiliki wa mgodi wa Buhemba mbona hatujamsikia?
 
Back
Top Bottom