Kwa majibu haya, inawezekana una ugonjwa wa kisukari na hiyo ganzi ni madhara ya kuwa na kisukari kwa muda mrefu bila kutibiwa. Nakushauri ufike kituo cha kutolea huduma za afya na kupata matibabu na ushauri wa kitaalamu.
Tuhuma hizi ni nzito. Tutafuatilia kubaini ukweli wake na kuchukua hatua. Lengo la Serikali ni kuhakikisha zinatolewa kwa uadilifu na kwa kuzingatia maadili ya taaluma katika sekta ya afya.
Mwenye maelezo mahsusi ambayo yanaweza kutusaidia kwenye ufuatiliaji huu asisite kuwasiliana nasi.
Dkt...
Sahihi kabisa. Hata walio chini ya miaka 50 wanahitaji kuzingatia misingi ya lishe, kufanya mazoezi, kupunguza matumizi ya vileo na kupima afya zao mara kwa mara.
TAARIFA
Jana tarehe 18 Septemba 2017, Mbunge wa Kigamboni Dkt Faustine Ndugulile (Mb) akiambatana na Naibu Waziri wa Wizara ya Nishati na Madini Dkt Medard Kalemani (Mb) walifanya ziara ya kukagua miradi ya umeme inayolisha Dar Es Salaam na hususan Kigamboni.
Ziara hii ilijumuisha Kamishna wa...
Kuna juhudi zinaendelea za kutaka kukarabati barabara za Kisota kwa ushirikiano kati ya wakazi wa Kisota ba Halmashauri.
Kama ni mkazi wa eneo na hauko kwenye mtandao wa wakazi wa Kisota. Ni-inbox jina na namba yako ili uweze kuunganishwa na kupata taarifa ya kinachoendelea.
Barabara ya Kibada-Mwasonga ipo kwenye mpango wa kujengwa kwa kiwango cha lami. Kwa mwaka ujao wa fedha upembuzi yakinifu unaendelea.
Natambua kuwa barabara hii imeharibika sana katika kipindi hiki cha mvua. Tayari nimeshawajulisha Tanroads kuikagua na kuchukua hatua za dharura. Matenngenezo...
Nakushukuru kwa kunitia moyo. Natambua changamoto ya kukatika umeme mara kwa mara Kigamboni. Hii inasababishwa na mambo kadhaa ikiwa ni pamoja:
1. Mahitaji ya umeme Kigamboni ni 20MW lakini tunapata 8MW.
2. Laini tunayopata Kigamboni inaanzia Kipawa na inahudumia pia Mbagala, Mkuranga na maeneo...
Kigamboni ni Halmashauri Mpya. Tunarajia ucheleweshaji na urasimu utoaji wa vibali kutokuwepo.
Kama ulipeleka maombi yako Temeke na haujapata kibali, bado ninaweza kukusaidia. Wasiliana nami.
Nashukuru Ndugu Nyabhingi kwa maoni yako. Kimsingi, michoro kwa ajili ya kipande kilichobaki imekamilika. Tunatarajia kazi kuanza muda wowote.
Suala la tozo pamoja na ufanisi wa huduma pale darajani ninaendelea kulifuatilia. Kumekuwa na kutupiana mpira kati ya NSSF, Wizara ya Ujenzi na SUMATRA...
Nawashukuru kwa michango yenu. Kwa sasa hakuna mipango yoyote ya kuwa na ruti za daladala toka darajani hadi maeneo mbali mbali ya Kigamboni. Ila ninaamini huko mbele ya safari itabidi tuangalie ruti za kutoka maeneo mbali mbali kuja Kigamboni kupitia darajani, mfano, Mbagala-Kigamboni...
Ndugu Francis Da Don hebu fafanua hiyo ruti unayopendekeza ili niweze kufuatilia.
Najua kuna daladala zinatoka Feri kupitia Mjimwema kwenda Kongowe au unaongelea kutoka darajani kwenda Mjimwema?
Dkt Faustine Ndugulile-Mbunge Kigamboni
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.