Mimi ni shabiki kwelikweli wa soka. Natamani timu yangu ishinde kila mechi na kila kombe. Lakini pia mimi ni muumini wa haki. Napenda sheria, kanuni na taratibu zifuatwe. Napenda nidhamu ya mchezo idumishwe. Kama timu yangu ikishinda, nafurahi ikishinda kwa haki.
Lakini mashabiki wengi...
Simba Sports Club a.k.a wahenga inashuka leo kukabiliana na kikosi Azam kwenye uwanja wa Azam huko Chamazi. Simba inashuka kwa mara ya kwanza kwenye uwanja huu kuikabili Azam huku kila timu ikiwa na ubora na nguvu ktk maeneo tofauti tofauti.
Simba, ni dhahiri ndio wanaopewa nafasi kubwa...
Ndugu zangu, kama mnavyofahamu mimi ni mfuatiliaji mwenye uchungu na mpira wetu wa Bongo na nilionyesha kutoridhishwa kwa kiwango kikubwa na hali ya utawala usio bora kutoka TFF ya Jamal Malinzi. Mimi ni muumini wa dhana ya utawala bora na kwa kiwango kikubwa eneo hili ndilo lililomwangusha...
Wadau, leo ni hukumu ya kikosi cha Taifa Stars dhidi ya Amavubi a.k.a. Nyigu kutoka Kigali. Ni mchezo wa pili baada ya kukutana wiki iliyopita na kushuhudia timu hizi zikigawana pointi kwa kutoka sare ya kufungana goli moja moja, jijini Mwanza.
Katika mchezo uliopita kikosi hiki cha Salum...
Mshambualiaji wa Timu ya Nkana FC ya Nchini Zambia ambaye pia ni Miongoni mwa wachezaji wanaowindwa na Mabingwa wa Azam Federation Cup, Simba SC Walter Bwalya amejitokeza na kutoa ufafanuzi kuhusu Uraia wake.
Bwalya ambaye uraia wake Bado unawachanganya wengi Kwa kuwa amezaliwa na Mama Mkongo...
Salum Mayanga ni kocha ambaye amekonga mioyo ya Watanzania kwa muda mfupi kutokana na kuunda Taifa Stars mpya ya vijana wadogo wenye vipaji vikubwa na ari ya kucheza soka. Amebadilisha mfumo kutoka ule wa kubutuabutua hadi kuweka mpira chini kwa pasi nyingi na kucheza kwa kushambulia zaidi...
Leo ni siku ambayo nimemwona Samatta akiwa ametoka uwanjani kwa hasira kubwa baada ya mechi kati ya Taifa Stars na Lesotho. Pamoja na yeye kucheza vizuri na kujitoa kwa 100%, anahisi juhidi zake zilipaswa kuzawadiwa na pointi 3 muhimu kutoka kwa kibonde Lesotho.
Lakini haikuwa hivyo, wachezaji...
Baada ya kutumia karibu majuma matatu hivi tukijadili vituko vya soka letu vinavyochangiwa kwa kiasi kikubwa na usimamizi dhaifu wa soka na ushabiki usio na tija wa wafuasi wa timu hizi kubwa na kongwe zaidi nchini, leo tujaribu kuja kivingine ili kuinua soka la nchi hii.
Simba na Yanga ni timu...
1.Hii ni TFF pekee iliyotukumbusha kuwa bado
kuna viini vya ukabila nchi hii ambapo viongozi wakuu wa chombo hiki pamoja na asilimia kubwa ya wadau wengine ni wahaya.
Sitaki kuamini kuwa hii ni bahati mbaya na kimsingi ni kinyume cha misingi ya utawala bora hata kama wateuliwa wana vigezo
2...
Kanuni ilishawekwa tangu ligi inaanza kuwa mchezaji mwenye kadi 3 atasimama kucheza mchezo unaofuata. Na pia mchezaji mwenye kadi nyekundu ya moja kwa moja anakosa michezo 3 inayofuatia, na yule mwenye kadi nyekundu isiyo ya moja kwa moja anakosa mechi 2
Mkemi na anayoiita Kamati ya Utendaji ya...
Kuelekea 'big match' ya michuano ya kombe la mapinduzi katika hatua ya nusu fainali itakayofanyika kesho Jumanne Januari 10, 2017, uchambuzi huu unaonesha kuwa itakuwa ni ngumu sana Yanga kuepuka kupigo kutoka kwa mtani wake wa jadi Simba.
Hadi majira ya usiku wa saa nne na nusu, kama mambo...
Mengi yamezungumzwa na wachambuzi wa soka kuhusiana na matukio na matokeo ya mchezo wa Simba na Yanga Jumamosi iliyopita. Mojawapo ya tukio lililovuta hisia ni utovu wa nidhamu aliouonyesha nahodha wa Simba Jonas Mkude dhidi ya mwamuzi Martin Saanya na kupelekea kuzawadiwa kadi nyekundu mapema...
Katika somo la ujasiriamali, kuna dhana maarufu ya kugeuza changamoto kuwa fursa ya kujiletea maendeleo. Inashauriwa kuwa wakati wengine wakiendelea kulalamika na mazingira magumu au yanayowakwaza katika kutimiza malengo yao, mjasiriamali halisi hutumia mazingira hayo hayo na changamoto zake na...
Utawala wa Jamal Malinzi umekuwa ukipokea shutuma nyingi kutoka pande mbalimbali za wadau wa soka. Mimi pia ni mmoja wa wakosoaji wake. Watu wengi tumekuwa tukihoji uwezo wake kiuongozi, uadilifu na umakini wake na wasaidizi wake katika shughuli ya usimamizi wa mchezo huu pendwa kuliko yote hapa...
Jinsi sakata la mchezaji wa zamani wa Simba Hassan Ramadhan Kessy kujiunga na Yanga lilivyoshughulikiwa na inayoitwa Kamati ya Sheria na Haki za wachezaji inaonyesha ni namna gani safari ya Tanzania kuondoa ubabaishaji michezoni ilivyo ngumu na hivyo kutishia mustakabali wa maendeleo ya mchezo...
Nimepokea kwa mshangao taarifa ya kusudio la kukodishwa kwa klabu ya Yanga kwa M/ kiti wake Yusufu Manji, uamuzi ambao umepitishwa kwa kauli moja na mkutano mkuu leo hii tarehe 6 Agosti 2016. Kwa umri wangu huu wa utu uzima wa kati sijawahi kusikia mfumo wa namna hii kwa uendeshaji wa klabu ya...
Katika hali isiyokuwa ya kawaida, katibu mkuu wa TFF amemjia juu Jerry Muro mkuu wa kitengo cha habari cha Yanga kuwa ni mbumbumbu na mtu asiyejua mambo ndio maana yeye peke yake kati ya viongozi wa Yanga ndio anaendelea kupiga kelele kuhusiana na mechi za Yanga.
Hii si kawaida kwa Mwesigwa...
The Central Bank of Kenya (CBK) has cleared the acquisition of a 51 per cent stake in the shareholding of Oriental Commercial Bank.
It was licensed to operate in Kenya in 1991, and was ranked 37th in terms of market share as at 31 December 2015, with nine branches.
Bank M of Tanzania was...
In 2013, three countries; Kenya, Rwanda and Uganda devised the so called coalition of the willing outside the traditional East African Community to fast-track regional integration especially on aspects of monetary union, political federation, grand infrastructural developments, etc.. When asked...
Hakuna kipindi kizuri ambapo Simba na Yanga zinakutana kama sasa ambapo macho na masikio ya wapenzi wa soka la Tanzania, Afrika Mashariki na Kati yataelekezwa katika dimba la Taifa kuanzia majira ya saa 10 jioni kushuhudia timu hizi kongwe nchini zikiwania uongozi wa ligi na vilevile kujiweka...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.