Ndiyo lazima ajenge bond kati ya aliye tumboni na aliyepo,na kuendelea kunyonyesha ni njia mojawapo ya kubond, watu hapa wanamshauri aache kunyonyesha eti asikae nae karibu sijuhi ni mawazo ya wapi haya
Yani nashangaa wanashindwa kutumia akili ya kawaida kabisa kufikri ,eti akili ya mazingira na mazoea, yani sijuhi nini ila Taifa letu kwa kiwango kikubwa lina watu wanaokumbatia ujinga.
Napenda kujibu kwa fact,hebu na wewe tupe fact ya mtaani kwako huko kubemendwa kuna kuwaje,na hayo maziwa mnayosema yanakuwa yamechafuka ,yanachafukaje labda.
Yani wewe utakuwa na matatizo siyo bure kabisa,hebu nenda katafute chanzo cha allergies ni nini,na kuna allergy mbalimbali zinazosababishwa na vitu mbalimbali,nenda basi hata Google upate nadharia mbalimbali kuhusu kipi bora formula au maziwa ya ng'ombe au uliza hata dr yoyote akuambie...
Penda kujifunza unapokoselewa,Nenda kaulize kama kuna dr atakeyekushauri kutumia maziwa ya ng'ombe kwa mtoto mdogo,na kama hujui maziwa ya formula yanatengenezwaje nenda kajifunze kabla ya kubisha.
Juzi kati hapa Drs wameelezea jinsi maziwa ya ng'ombe yanavyoleta allergy especially kwa watoto...
Aisee maziwa ya ng'ombe yasiyotiwa maji? Content ya maziwa ya ng'ombe aliyoandaliwa ndama ,mtoto ndiyo ayanywe hivyohivyo? Ni bora formula kuliko maziwa ya ng'ombe kwa mtoto mdogo maziwa ya ng'ombe yanasababisha allergy tena ni mtoto mdogo ambaye kinga ya mwili bado ni ndogo.
Hamna hicho kitu kinachoitwa kubemenda, Anatakiwe aendelee kunyonyesha na azingatie kula lishe kamili na supplement ya vitamin na Zinc,atafute unga wa mbegu za maboga ili kuongeza kiwango cha maziwa ,
Makalekale hata Mimi huwa nawasafishia wanangu,unajua huu usasa yani mtu hajuhi chochote ,kwa tunaobahatika kupata elimu ya wazee Wa zamani ukimwambia mtu anabisha ,wanafikiri watu Wa zamani walikuwa wanaenda kwa specialist.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.