Nadhani kuna tatizo kwa weledi wa viongozi wetu hasa katika suala zima la leadership. Kabla ya kukurupuka alitakiwa kujua utaratibu uliopo.
Fedha zilizotumika JICA au Serikali ya Japan ilishaamua zitatumikaje, hakuna namna ambayo matumizi hayo yangeweza kubadilishwa.
Hata kama wasingeeda...
It looks interesting good to know that, though sidhani kama kuna fomular maana mwingine anaweza kuwa na aibu wakati fulani au akiwa katika hali fulani na baada mfano anapopata bia mbili anakuwa na uwezo wa kuangalia machoni, kiunoni au shingoni n.k
Unajua tatizo kubwa ninaloona mimi ni kuwa bado Watanzania tumekuwa na maono ya kijamaa zaidi wakati Taifa lilishautupa ujamaa siku nyingi. Tukumbuke kuwa uedeshaji wa NHC kwa mfumo wa kiujamaa ulifikisha shirika katika hali mbaya sana. Leo Shirika limefufuka kwa kuwa limeedeshwa katika mfumo wa...
Waziri ni kiongozi wa Serikali na siyo mtu wa kawaida au mfanyabiashara, suala la kuzuiliwa kwake Bandari ya Tanga ni lazima kuangaliwe kwa umakini ili kuepusha chuki, viongozi wa Serikali wanautaratibu ambao unaruhusiwa kutumiwa kwenda kutembelea au kufanya ziara ya mafunzo au chochote katika...
Ni kweli tunapongeza ni hatua nzuri kwa uzalendo. Hata hivyo ni vyema tufanya tathmini ya kina kubaini kama hii njia sahihi au tunaenda kumkandamiza mlaji. Kwa sasa mahitaji ya sukari Tanzania ni kama 500k metric tonnes wakati uzalishaji wa ndani ni takriban 350k metric tonnes. Hii deficit...
Suala la ushirikina limekuwa likitumiwa na wengi sana kukwamisha maendeleo. Ninaamini kuanzisha biashara ikakwama ni kitu cha kawaida lakini wengi wakiona umeshindwa basi ndiyo kigezo cha kujaji hata wengine wanaotaka kuanzisha biashara. Utasikia utaweza wewe hapa hata fulani alishindwa.
Kwa ujumla hakuna bidhaa ambazo hazina uhitaji. Bidhaa zote zinauhitaji ndiyo maana zinaendelea kuingia nchi na kupata soko. Nakubalina na wewe kuwa kuna umuhimu wa kuangalia kupanda na kushuka kwa shillingi ikilinganishwa na fedha zenye nguvu duniani. Hili suala la kuangalia kwa upana zaidi...
Ingekuwa na maana zaidi kama ungeweka wasifu wao. Hao ni wale unaowajua wewe, kumbuka pia wengine watakuwa na majina au mapendekezo ya watu ambao wanaweza kuwa na weledi zaidi ya hao na hivyo kuwa wasifu wao upo wazi ili kutoa nafasi kwa wachangiaji kuchambua. Kama mchangiaji moja hapo juu...
Kimsingi Mawaziri wengi wanaofanya kama alivyofanya Mhe. Rais kushitukiza wamekosa ubunifu na kama ningekuwa mkuu wao naanza kuwa na mashaka na weledi wao. Serikali haiwezi kuendeshwa kwa style moja tu, halafu siyo lazima kama imetokea umepitia mahali uwe na waandishi wa habari. Baadhi ya...
Tusipo tafuta undani wa mauaji ya namna hii inaweza kutumaliza. maana leo kwake kesho kwangu mimi na wewe. Wakati mwingine kuna wananchi wanataarifa za vifo hivi kwa hiyo kama wapo wanaojua nini kipo nyuma ya pazia hili wasaidie polisi kwa vyovyote vile. serikali ya sasa ni sikivu watatusikia na...
Sidhani kama suala uaminifu ni dar tu, kwa sasa kupata mtu mwanifu Tanzania ni kazi ngumu hata awe ndugu, ninajua rafiki yangu yupo nje ya nchi yeye ametapeliwa na mke wake kabisa. Walikuwa wote nje akampa mke fedha kuja kujenga Tanzania yeye aendelee na kazi lakini ilikuwa ndiyo mwishi wa ndoa...
Matengenezo Mill.55, tujiulize hiyo gari ina miaka mingapi tangu imetengenezwa? imetembea KM ngapi mpaka wakati inapata ajali. Tukijua hayo tunaweza kumtuhumu kama ameibia serikali au la, maana suala siyo VX tu, je wakati huo ilikuwa na dhamani kiasi gani inakuwa halali kuitengeneza kwa kiasi...
Ninachoamini kuwa kuwa na kiranja mzuri hata wale wazembe watawajibika. Vile vile wezi nao wataweza kubainika kwa urahisi. Hakuna malaika binadamu ni binadamu tu, kwa hiyo tuwape muda na kumwomba Mungu awajalie maono ya utaifa kwanza
Huu ni mtazamo wako na nauheshimu. Hata hivyo naomba kuweka kumbukumbu sawa. Balozi Mahiga ambaye ameteuliwa kuwa Waziri wa Mambo ya Nje hakuwahi Balozi wa Rome, nadhani Balozi aliyehusika na hilo suala na kesi alishinda kuwa ilikuwa ni kashfa ya kutengenezwa ni Balozi Prof. Mahalu na siyo...
Sijaona ni wapi Serikali ya JPM imesema kuwa haitambui uwepo wa Mawaziri. Mawaziri watakuwepo kwa mujibu wa katiba. Hivi tungefurahi leo kusikia baada ya kuapishwa tu ateuwe baraza na mawaziri halafu kwa hizi kasheshe za bandari na TRA unasikia na waziri naye ameondoka kwa kuwa tu ufuatiliaji...
Kwa namna moja nakubaliana na uwezekano wa watu kutolewa kwa majungu na chuki kati maeneo ya kazi. Suala la vyeo watu wanaenda hadi kwa waganga sasa wakiona kuna nafasi ya kuharibia aliyejuu kwa matamanio ya kupanda bila kwenda kwa waganga unaweza kabisa kutumiwa mwanya huo. Hivyo ni muhimu sana...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.