Lazima kutakuwa na shida mahali fulani. Wakati Ikulu ilitoa taarifa kwamba Uingereza walitoa pesa kuchangia maafa hayo, lakini Waziri Mkuu akisoma hotuba bungeni juzi alisema kwamba Uingereza waliahidi kutoa Shilingi 6 bilioni. Ipi ni kweli sasa, walitoa au waliahidi?
Kwa taarifa yako hata walio asisi CHADEMA walitoka CCM. Hakuna jambo la ajabu hapo. Mpinzani mzuri ni yule anaye mfahamu vizuri adui yake. Sumaye anaifahamu vizuri CCM ndio maana wana hofu.
Ukweli ubaki kuwa ukweli hata kama unauma. Prof. yuko sahihi, mlaji wa mwisho (end user) ndio mlipaji wa VAT. Ktk hili tukubali kwamba watumiaji wa huduma za kibenki ndio tunabeba mzigo.
Tumefikia pabaya sana kama kuwaona wagonjwa nako tunaingiza siasa na u-chama. Nadhani Magufuli hakwenda kumwona Sumaye kwasababu yeye ni CCM bali alienda kumwona kama watu wengine walivyoenda kumwona. Ni upendo tu kwa watu wengine.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.