Mawazo yako ni sahihi kabisa lakini, je kwa njia hii tutajenga taifa la kitanzania au ndiyo tunaanza kujenga taifa la vitaifa vidogo vidogo? Je busara na mahitaji ya akina Nyerere ya kutaka kujenga taifa moja imara yamepitwa na wakati? Ni vigumu kujenga taifa katika bara la Afrika. Wanaotaka...
Mawazo yako ni sahihi kabisa lakini, je kwa njia hii tutajenga taifa la kitanzania au ndiyo tunaanza kujenga taifa la vitaifa vidogo vidogo? Je busara na mahitaji ya akina Nyerere ya kutaka kujenga taifa moja imara yamepitwa na wakati? Ni vigumu kujenga taifa katika bara la Afrika. Wanaotaka...
Tafsiri yako haitendi haki wala kwa mbunga huyo au kwa wananchi wale. Tatizo ni ubovu wa barabara. Hata kama una gari la namna gani kule halifiki. Hakuna barabara. Labda ungeshauri anunue helikopta. Vijiji vya kando kando ya Ziwa vinazungukwa na milima na miamba, hivyo ni vigumu kutengeza au...
Katika nchi kama ya kwetu ambayo ujenzi wake uliishia kwenye msingi ambao tunaubomoa, hakuna chama cha siasa kilicho bora. Ili kuwa na kikundi kinachojiita cha siasa, inabidi uwe na taifa linalojitambua na kujielewa. Taifa linalofahamu wapi limetoka na wapi linaenda. Taifa la namna hiyo linakuwa...
Kuna maneno na mazungumzo mengi na marefu juu ya kurudishwa mahakama ya Kadhi. Na kila linapozungumzwa jambo hilo linafananishwa na dini za kikristo.
Kwa wale tunaojua historia ya mahakama ya kadhi, tunajua kwamba ziliidhinishwa hapa nchini na utawala wa Waingreza pale walipoweka mfumo wa...
Naona unaota ndoto za mchana au unataka kuchekesha baraza? Hivi kweli kwa siasa za uchumia tumbo za nchi yetu, mtu akurupuke toka nje ya mtandao aje aingie jikoni na awe ndiyo mlaji mkuu na mtengeneza ulaji! Haiwezekani kabisa.
Ebu tujifunze kujenga hoja! Hata kama sikubaliani na yanayojadiliwa, hauwezi kujenga hoja ya ubadilifu wa fedha za umma hata kama ni kidogo namna gani, kwa msingi eti wengine wameiba nyingi zaidi. Hii ni hoja mbovu na haifuati misingi ya kimantiki ya ujengaji hoja.
Nimefurahia sana tafakuri yako. lakini, Najiuliza,hivi kweli msanii na mwana taaluma siasa za kikwetu zinamfaa?Nawatazama akina Profesa Anna Tibaijuka na Muhongo, wangetoa michango mikubwa zaidi kwa nchi yetu kama wangebaki na taaluma zao kuliko kuingia kwenye siasa za moja kwa moja. Ndivyo...
sakata zima linatokana na udhaifu wa sheria zetu na muundo wa utawala wa nchi yetu. Wananchi tulipendekeza kuweko na mgawanyo wa madaraka kati ya Wananchi wanowakilishwa na Bunge, na serikali inayokabidhiwa uendeshaji wa nchi. CCM mkakataa mgawanyiko huo. Mnataka serikali iwe sehemu ya Bunge. Ni...
This is a clear picture of Mechievalian reasoning. You need to be critical and analytical and apologetic.At your age you need to have a litle bite of intellectual honesty.
Hapo umenigusa vizuri sana. Hatuwezi kuhubiri Amani bila kuhubiri Haki. Hakuna Amani mahali ambapo haki haitendiki au haionekani kutendeka. Hatuwezi kuhubiri Upendo kama hatuhubiri Haki. kuhubiri upendo bila haki ni kajeli.
Ninakubaliana na hiyo historia yako, lakini kuna upande mwingine haujautazama. Ukoloni uliukuta Uislamu na dini zetu sisi weusi za jadi. tulikuwa na sheria zetu na mila na desturi zetu za namna ya kuishi na kutatua matatizo yetu ya kijamii. Tatizo la mahakama ya kadhi ni sawa na la mahakama za...
tatizo la mijadala yetu ni kwamba tunawajadili watu badala ya mfumo. Huyo anayetajwa atafanya kazi na nani kama wote ni ukoo wa panya. kuna msemo usemao kwamba nazi mbovu ni harabu ya nzima. Hivi kwa CCM ya sasa ambayo wajumbe WOTE wa Mkutano mkuu wamenunua uwakilishi, wanaweza kupata mtu safi...
Katika historia ya kudai kusikilizwa, walalahoi wa Uingreza ambao utawaliwa na ukoo wa kifalme, walitaka na wao wawe na nchango wao katika sheria zinazowahusu. Katika kutafuta namna ya kufikisha matakwa yao kwa watawala wao, yaani Mfalme na watu wake, wakamtuma mmoja wao aende kama msemaji wao...
Hivi kuitwa mjinga tusi? kama hatuwezi kutofautisha maslahi ya umma wa Tanzania na ya wezi wala rushwa, ni kwamba hatujui, na hiyo ndiyo maana ya ujinga. Swali la msingi: kwa nini tunaendelea kuamini ngonjera badala ya takwimu za kiutafiti na hoja?
Kwa katiba ya Zanzibar tuliyo nayo sasa Muungano uliishavunjika. Na Raisi wetu ambaye alipaswa kutetea katiba aliyoahidi kuilinda hakufanya hivyo. Mwalimu Nyerere aliishatuasi kwa kusema Raisi hasiyetetea katiba aliyoapa kuilinda hatufai. Tume ya jaji Warioba ndiyo wanataka kurudisha Muungano...
jaribu kuelewa hoja ya lissu. Hawa wawili walikuwa mapacha wa dhana fulani yaani kuunganisha utawala kati ya cuf na ccm. Hayo ndiyo makubaliano. Ccm wangekuja na dhamiri ya umoja na maridhiano hayo, cuf wangeendelea kuwa wamoja. Kama mmoja kavunja makubalaino hapo upinzani unajitokeza wazi...
huyu Conchesta Rwamulaza anaonyeshwa kama Diwani huku akiwekwa kama MB. Mbona wabunge wa mwanzoni walipewa heshima au title tofauti: mfano Mhe. Hamis S. Kagasheki (MB) naye? Au ofisi za serikali kama vile ya Mkuu wa Wilaya nao wanafanya kazi kwa maelekezo ya Chama?
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.