Una uhakika na ulichoandika. Si kweli kabisa, Kenya ipo uber Nairobi na Mombasa. Wenzetu wameenda mbali zaidi kuna kampuni nyingine imeanzishwa iweze kushindana na uber.
Mkuu Sooth kwa kuongezea, hata magari yanayotoa huduma kwa mwavuli wa uber wamiliki ni watanzania. Kwa taarifa nilizo nazo, naomba nisahihishwe iwapo nimekosea, uber hana magari, anchofanya sasa ni kusajili magari yanayomilikiwa na watanzania. Wao wameleta mfumo tu.
Hapa ndio lilipo tatizo! Kwa nini itumike nauli ya taxi za vijiweni na si zile za uber? Kigezo gani ulichotumia kwamba Mlimani city to Kariakoo nauli iwe elfu 20. Nauli wanazochaji taxi drivers wa vijiweni ni za kimagumashi!
Taxi driver wa kijiweni yuko radhi apate elfu 60 kwa siku kwa trip...
Hili ni wazo zuri la wazawa kuwa na hisa ikiwezekana katika uber, au hata kuanzisha makampuni yao ili kuleta ushindani zaidi. Ukiangalia kwa undani taxi drivers wanaopinga uber, hawapingi kwa sababu ni kampuni ya kigeni, hapana, wao wanalalamikia mfumo wa uber uliosababibisha nauli kwenda chini...
Hatuongei kinadharia hapa! Tatizo hapa si uber kukosesha taxi drivers wanyonge vipato. Nimeongea na taxi drivers wengi waliojiunga na uber. Wanasema kuna unafuu sana sasa kulinganisha na awali: uhakika wa mapato na hata usalama wao (kuporwa magari n.k.). Kwa hiyo hoja ya kipato na cha ziada...
Hoja yako ni ipi hapa? Taxi drivers wa uber si Watanzania? Nani anamiliki magari yanayotoa huduma kwa mwavuli wa uber? Nani amezuia Mtanzania au Watanzania kuanzisha kampuni kama uber?
Mbona unatoka nje ya mada uliyoianzisha wewe mwenyewe? Jibu hoja:
Mimi nina gari langu dogo, nakwenda kulisajili uber, ili nitoe huduma ya taxi kwa uwazi na unafuu. Uber watanikatalia? Na kama wataniruhusu nikasajili gari langu, sitakuwa nimewekeza? Kutokana na nilivyokuelewa wewe, mwekezaji...
Kama huyo jamaa ni mtaalamu wa tehama alitakiwa atoe suluhisho la hili tatizo kwa kutengeneza mfumo utakaowasaidia taxi drivers anaowatetea. Watanzania tuache porojo!!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.