Hivi zile nondo za medicine mtu anawezaje kuzichanganya na siasa? Au ndio wale waliovuta degrees za third class a.k.a gentleman's. Manake ile PCB ya A'level tu ilikuwa haichanganyiki na chochote, na huko Muhimbili kwenye MD tumesikia simulizi nyingi za kushangaza jinsi shule inavyotesa. Huyu...
We mwongo tu. Usidhalilishe jeshi la polisi bure tu hapa. Ati SMG unasema ni AK47? Huzijui hizi silaha umezisoma tu kwenye hadithi za Willy Gamba sa unakuja kutafutia sifa hapa. Hii imebuma, tunga fiksi nyingine.
Mheshimiwa umesahau kuwa Kigwangala ni daktari wa tiba (MD), ambayo ni digrii ya kwanza sawa na nyingine kama BA, BSc, LLB nk, kwa hiyo usitake kumpima kwa kiwango cha PhD. Sifa za kujiunga digrii ya kwanza zinafanana kwa fani zote, sifa za kumaliza zinatofautiana kidogo kwa mujibu wa mahitaji...
Asanteni mlionipa updates. Naombeni wenye taarifa za kujazia kuhusu hao ambao taarifa zao hazijatosheleza mchangie kwenye huu uzi, nafikiria kuwa zikikamilika nitoe makala kabisa kwa faida ya wengi, wakiwamo wale wasio na fursa ya kutumia hii mitandao.
Mambo hayo ya ukiukwaji wa katiba hasa ndiyo yalisababisha. Hadi kufikia mwaka huu, ukiukwaji huo umeongezeka zaidi, lakini nguvu ya kudai Tanganyika imezidi kuwa dhaifu, hasa kwa sababu hakuna aliyeko mstari wa mbele waziwazi, wengi wanajificha nyuma ya rasimu ya Warioba, na wamesababisha...
Kila ninapowasoma hawa wazee na jinsi walivyothubutu kuiweka mbele hoja yao WAZIWAZI, nashangaa ni kwanini watetezi wa Tanganyika wa leo wanaogopa kupiga kura ya wazi katika bunge la katiba? Kwa sasa hivi adui mkubwa wa kupatikana kwa Tanganyika ni unafiki. Wapo wabunge ambao vipembeni...
Na wana ushawishi gani kwa hoja hiyo kwa sasa? Hapa nawakumbusha kuhusu hawa wazee, maelezo mafupi kuwahusu, na kwa wale ambao sina habari zao wengine mjazie. Watu wa kuenziwa hawa:
Njelu Kasaka: Huyu alikuwa mbunge wa Lupa mkoani Mbeya. Baada ya sakata lile mzee Ruksa alimpoza kwa...
Umeambiwa wazanzibari huko kwenye balozi ni experts, Tanganyika imewaajiri kama consultants kwa kuwa Tanganyika inahitaji huduma zao na haina watanganyika wenye sifa hizo, kwahiyo ikatafuta exoerts kutoka nchi nyingine. Na hilo linapaswa litambuliwe kuwa ni mchango wa Zanzibar kwenye muungano...
Hii kwangu ni quote of the week. Ni sababu tosha ya kuendelea kutetea serikali mbili, na tena Zanzibar wasibughudhiwe kudaiwa kulipa gharama za muungano, kwakuwa kimsingi wanazilipia tayari kwa kutumia manpower na expertise yao. Serikali mbili daima. CCM oyeeeee.
Kwa marekebisho yanayopendekezwa na CCM ndivyo itakavyokuwa. Kutakuwa na serikali mbili: Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Serikali ya jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo kiukweli itakuwa ni serikali ya Tanganyika kwa kuwa haitakuwa na mamlaka Zanzibar (hii ni baada ya Zanzibar...
Hujui unachokisema. Tanganyika ilipata uhuru wake na kuunda serikali ya jamhuri huru iliyodumu hadi 25 Apr 1964. Kwani kwa mawazo yako, walioitaka Zanzibar yao sababu zao ni za msingi au si za msingi? Mimi nitakutajia sababu yangu moja ya msingi ya kuitaka Tanganyika yangu: ituwezeshe kutumia...
Ile hotuba nilianza kuifurahia mwanzoni lakini baadae alinikata maini kabisa. Kwamba kwa mtazamo wake katiba inayofaa ni ile inayowatetea wazanzibari kwa kila wanachokitaka, lakini watanganyika haki yao haitamkwi wala kutetewa. Nilichukizwa sana na ule mfano aliotoa wa wapemba wanaolima vitunguu...
Mchakato umeshavamiwa, au ulivamiwa tangu mwanzo hatukujua. Tutarudishiwa katiba hiihii ya 1977 ikiwa na editing hapa na pale. Tumeibiwa pesa zetu maana kama hali ni hii hakukuwa hata na haja ya kuwepo mchakato huu. Kama maoni yamekusanywa na hamtaki yatumike, kwanini mmetusumbua?
Mkuu kwa mwelekeo uliopo sasa hivi hilo la serikali moja lishazikwa siku nyingi, halitatokea kamwe labda tu yafanyike mapinduzi mengine Zanzibar. Kwa hiyo tuking'ang'ania serikali mbili tunamaanisha:
Serikali ya Zanzibar na serikali ya Tanzania (ambayo ndiyo Tanganyika, kwa hiyo muungano...
"Isitoshe, kati ya waliogusia muundo, asilimia 30 walitaka serikali mbili, asilimia 37 walipendekeza serikali tatu, na asilimia 25 walitaka muungano wa mkataba; asilimia nane walitaka serikali moja.
Kwa hivyo, waliopendekeza serikali tatu ni theluthi moja tu ya waliogusia muundo wa...
Kama kuna jambo moja ambalo wazanzibari wameungana pamoja kulipigania bila kujali itikadi wala dini ni hili la kuitaka Zanzibar yao iliyo huru. Watanganyika wanapaswa kuiga mfano huo, wa kuungana bila kujali itikadi katika kuitaka Tanganyika yao iliyo huru. Ndipo nchi mbili huru zifanye Jamhuri...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.