Article hii sio ya LISSU bali ni ya kutunga. EL asingeweza kwenda IKULU bila maelewano na chama chake. Naamini alitumwa kupeleka ujumbe wa chama huko katika njia ya kiungwana. Amini usiamini ukweli ndio huo.
Huwezi kujua kasoro ya mtu kwa uchunguzi wa siku chache tu. Siku alipotangaza nia kilikuwa kipindi chenye mambo mengi yaliyojificha. Angalia Mh. Magufuli, alipotangaza nia hakusema mengi na watu wengine waliona hatatufaa. Lakini sasa ona anayofanya. Anasifika nje na ndani ya nchi. Nani alijua...
Membe anaweza kufaa kabsaaa. Rais anayetakiwa ni yule anayefuata sheria/katiba, anayeheshimu mawazo ya wenzake, anaye chukia rushwa, anayethamini uhai wa binadamu wenzake akijua kuwa wana wapendwa/familia inategemea uhai wake, mkweli n.k. Sifa hizi Membe anazo kabisa. Ninamfahamu vzr sana wala...
Iwapo polisi watafanya kazi yao barabara, wakawakamata wakorofi kama hao na kesi zikapelekwa mahakamani wakahukumiwa ipasavyo wakorofi hao watashika adabu. Rais wetu mpendwa analazimika kutoa amri za namana hiyo labda baada ya kuona watu tumezidi ukorofi na vyombo vyake havifanyi kazi kwa wakati.
Mimi naona ni bora tuheshimu na kufuata taratibu za kisheria kwa kila kosa linalotendwa na yeyote. Hakuna kosa lisilokuwa na adhabu yake hapa nchini. Na mamlaka halali inayoruhusiwa kuamua kosa (kuhukumu) lililotendwa na mtu ni mahakama. Na mahakama imepewa pia mamlaka ya kuamua adhabu kwa kosa...
Suala la VPL liko hivi: Tenda haikutangazwa bali ilikuwa Closed Tender. TFF ilichagua kampuni 3 kushindania tenda hiyo ikiamini kuwa kati ya hizo atakayeshinda atamudu vzr kazi hiyo. Kampuni hizo ni Startimes/TBC, Agape/TSN na Azam TV. Startimes/TBC 25billion/=, Agape 8billion/= na Azam Pay TV...
Startimes kwa hapa nchini inamilikiwa na wabia wawili tu. Wabia hao ni kampuni ya kigeni kutoka China iitwayo "Star Communication Networks Technology Company Ltd" ( 65%) na (TBC)Tanzania Broadcasting Corporation (35%) ya hapa nchini.
Ni kweli kabisa Azam Pay TV imesajiliwa Mauritius.Haijasajiliwa hapa nchini. Lakini hilo halimaanishi kuwa halipi kodi. Nadhani wanalipa kwa kuwa Magufuli ni mkali kama nge ila huko siku za nyuma sijui. Ila cha kushangaza AZAM PAY TV anashindanishwa na TV zilizosajiliwa hapa nchini katika kuomba...
Ndugu zangu,
Mimi nilipatwa hilo tatizo la kukosa Local Channels. Niliwapigia simu Startimes kuuliza kulikoni kwa kuwa miaka yote tangu Digital TV iingie nchini nimekuwa naona bure channels za hapa nchini, hasa zile 5 traditional (TBC1, ITV, STAR TV, CH10 na EATV). Walinijibu kuwa wana matatizo...
Oh, jamani, Wapambe wa wagombea take care. Wakumbushe wazee wetu wasije achia Chadema kupita bila kupingwa
Hii sheria ni kandamizi. Oh, Lowassa wangu!!!
Ni jambo la kushangaza Waislaam kuikataa Bakwata kuwa ni chombo kinachoendeshwa na Serikali huku upande wa pili wanahitaji Serikali iwaundie na kuendesha Mahkama ya Kadhi. Hata serikali ingekubaliana namatakwa hayo mwishowe ungetokea mtafaruku mkubwa sana siku za usoni kwakuwa waislaam kama...
hako kajamaa ni kagonjwa jamani. Kwani nyie hamjui historia yake? Basi uombe uelezwe.jazba yake muionayo inatokana na tatizo hilo sio ushujaa wake binafsi.
jamani warioba hafai hata kidogo. Alipokuwa w/mkuu mliona alivyoboronga, mmesahau. Huyu hafai kabisa. Ni kwa kuwa hayupo uwanjani, akiingia uwanjani kucheza ndo mtaona barabara madudu yake. Atakuwa - the worst president ever seen.
nakubaliana na wewe. Ni juu ya jk kulijua hilo ili awalinde wateule wake katika midomo ya walafi wa raslimali za taifa. Wanatumia kila mbinu hata vyombo vyao vya habari kutimiza malengo yao kwa kuwaandama wale mawaziri wauri kama prf. Muhongo wanaokataa udalali katika sekta ya gesi. Heko...
Tatizo ni VITALU VYA GESI. MADALALI wanataka kuhodhi utajiri wa nchi katika familia zao.Baaada ya kufariki Nyerere, wafanyabiashara ndo wamepata nafasi ya kuleta ukoloni mambo leo. Wanatumia hata vyombo vyao vya habari kudhalilisha watendaji safi lakini wasiokubali kutii matakwa yao potofu...
Nappy ana usongo binafsi EL. Kwa marafiki wake wa karibu amekuwa akiwanongoneza kwa kiapo kuwa "over his neck" hataruhusu EL apitishwe kugombea Urais. naona amejidhatiti kumtoa katika race ya urais kwa kutumia kipengele cha kwenda kinyume na maadili kwa kuanza kampeini mapema.
Mengi alihangaika sana apate leseni ya multiplexer (digital broadcasting licence) kwa ajili ya kurusha matangazo ya tv hewani kwa mfumo wa digitali. Alihudhuria kila mkutano uliokuwa unajadili suala hilo hapo awali wakati tcra wanataka kutoa leseni za mfumo huo. Alipoona anatiliwa mashaka kuwa...
Wala hakuna haja ya kujibizana kwa hasira kama vile ni majuha. Matusi hapa sio mahala pake. Ukweli utabaki kusimama pale pale kuwa mengi na muhongo hawaivi chungu kimoja. Chanzo kwa kweli ni vitaku vya gesi. Sasa kama muhongo alimuonea mengi kwa kumnyima vitalu hivyo kutokana na mengi kutokuwa...
Kwa kweli mengi anatumia hicho chombo vibaya sana tena kwa manufaa yake au kuwaponda au kudhalilisha wenzake. Kama enzi za mwalim jk angekuwa amefunga kabisa. Sheria hazifuatwi na tcra kimyaaa!!!!!!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.