Tanzania tunahitaji wabunge kama hawa ambao wako huru kifikira na kiutendaji sio wale wenye kufungwa na itikadi za chama kiasi cha kuona 'nyekundu' ni 'Nyeupe'
Kusaini muswada hakuzuii mabadiliko? wanachi ndio watakao amua, katiba ya kuwalazimisha wananchi haiwezi kudumu kwa sababu siyo yao! hivyo vyovyote atakavyofanya tutaandika nyingine baada ya wananchi kuchagua serikali yenye kuwajali.
Hapa nadhani umekosa ufahamu wa nini maana ya "wise people" "get informed that wise people sometimes change their mind" and hence their decision. natumaini wabunge wa-CCM hawatakuwa tayari kurudia kosa lililowafanya waonekane hawako makini mbele ya mwenyekiti wao, kiasi cha yeye kuurudisha...
Kinachotokea hapa ni udhaifu wa viongozi wetu kushambulia watu binafisi kwa lengo la kupoteza hoja iliyoko mbele yao!! hili ni tatizo kubwa! Viongozi wengi wanaotetea masilahi mapana ya kitaifa na wananchi kama Tundu Lissu hushutumiwa sana na viongozi wa chama tawala ili tu kuwafitinisha na...
Is it true? kwamba kiongozi yeyote wa kitaifa akisema au kufanya jambo linatokana na washauri? je viongozo hawana mitazamo, misimamo na hata uelewa wao wenyewe juu ya jambo wanalolisimamia? Huu utamaduni wa kusingizia washauri nadhani uko Tanzania pekee.
Bahati mbaya sana CCM hawaoni wala kuamini kuwa katiba ni ya watanzania wote! wao wanaona kuwa wanamiliki nchi na hivyo kutaka kufanya vile wao wanataka!! nadhani katika hili wamejipalia makaa, wapinzani sasa ndiyo sauti ya watanzania.
Hii nayo ina-sound kama mchezo wa kuigiza!!. Kweli CCM kuna tatizo! Mwenyekiti wa chama hicho ndiye mteuzi wa mawaziri akiwemo waziri wa elimu kwanini asimfute kazi badala ya kuja na ngonjera za majukwaani!!!! kazi tunayo nchi hii.
Hii ni hatua nzuri katika kujenga na kuimarisha chama, lazima wadau muendelee kutoa elimu, taarifa na ufafanuzi pale inapohitajika. Biashara asubuhi jioni mavuno.
Mara nyingi wanasiasa hushangaza sana! huyu Kinana anatetea muungano wa serikali mbili ambao umejaa migogoro na kuonekana kutotakiwa na kutoaminiwa na pande zote mbili, haya ni maajabu ya wanasiasa!! CCM katika hili wanasumbuliwa na matatizo yao ya kutopenda mabadiliko kwa kujifanya wao ni...
Nadhani watanzania itatuchukua muda mrefu sana kujitambua, ikiwa hadi leo bado kuna watu wenye mawazo kama hayo! inashangaza sana. Hali ya kisiasa hufikia kuwa sawa kwa sababu vyama tawala havipendi kuachia madaraka kwa amani pale vinaposhindwa! anyway, tutaendelea kutoa elimu ya uraia! mtaelewa...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.