Makosa hayohayo yanafanyika Kawawa road-kutoka magomeni kwenda roundabout ya kigogo. Mvua zikinyesha lazima tutapiga mbuzi. Huwezi weka daraja la upana usiozidi mita tatu tena bila kunyanyua juu tuta la barabara ukitegemea matokeo chanya. Bado tuna safari ndefu sana.
Kwa kujibu wa maelezo ya Mbunge Shabiby, nchi inatumia lita million 400 kwa mwezi. Hivyo ukitaka kujua TBS na hao wengine wanapata mgao kiasi gani zidisha makato yao mara lita 400m.
Hata mafuta yapande kwa kiasi gani, mfanyabiashara anaendelea kula TZS108 take kwa lita. Profit margin yake haishuki. Na wenye mapato yao nao wanachukua kiwango kile kile. Mtumiaji wa mwisho ndo anayebeba mzigo wote wa kupanda kwa bei.
Chama tawala wameamua kucheza ngoma ya wapinzani bila kujua, taratibu wanapoteza wafuasi wao (pro Magufuli). Kwa maana nyingine chama tawala wanashambuliana wenyewe kwa wenyewe, wakisaidiwa na wapinzani.
Kama jina lile lisingekuwa na nguvu, wasingesimama kujitetea kila siku kuwa watamaliza...
Nina wasiwasi kama fedha zinazorejeshwa huwekwa kwenye hesabu za mapato ya halmashauri. Huenda nazo hupotelea mifukoni mwa watu. Imagine hizi ni za kuanzia 2017, tukichukua miaka kumi nyuma itakuwaje?
Acheni kusema vitu ambavyo havina ushahidi. Hebu tutajie watu waliouwawa ama kutekwa. Acheni kuchuma Dhambi, mnahukumu utafikiri ninyi ni Mungu ama mlikuwepo wakati anauwa watu. Acheni kuhukumu.
Yesu akawaambia, Basi na asiye na dhambi awe wa kwanza kumpigia mawe mwanamke huyu.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.