Search results

  1. Lorenzo Samike

    Funzo la Sabaya: Watawala hawana rafiki isipokuwa katika maslahi

    Huyu Sabaya japo siujui uovu wake kiundani sana, lakini ninachofahamu ni kuwa alikuwa akiwapigania watawala sana. Huenda ilikuwa ni ajira yake, lakini alikuwa hodari sana wa kuitetea serikali na kuipigania. Alishiriki kuwakakandamiza wapinzani kwa namna moja ama nyingine ili kulinda maslahi ya...
  2. Lorenzo Samike

    Kukatika umeme kila siku Arusha; Mamlaka zimeshindwa kazi?

    Tuliwaambia humu, jikiteni kumalizia ujenzi wa Bwawa la Mwalimu Nyerere, mkaanza kuleta siasa uchwara!!! Oooh tunataka gesi! Vizungu uchwara viiingiiii, oohhh gesi is cheap sijui nini nini!! Kumbe mna michongo ya kitapeli kule kwenye gesi. Gesi zenyewe mmewakabidhi wachina wanavuna jinsi...
  3. Lorenzo Samike

    Uanaume haufundishwi; Ushoga ni kichaka cha kutowajibika

    Sijui tu hii dhana watu waliitoa wapi! Kwamba eti ili mwanaume awe rijali lazima afundishwe na aelekezwe, ikiwemo na pamoja na kuoneshwa hulka za kiume ili aziige. Wengine wakasema kwamba, sababu mojawapo ya watoto wa kiume kuwa mashoga ni ukosefu wa malezi ya baba. Eti hawakuwa na 'role...
  4. Lorenzo Samike

    Tuache usanii wa kuvaa barakoa

    Haya mabarakoa yamejaa usanii mtupu. Ukiingia ofisi ya umma unalivaa. Ukitoka unalivua. Hata mama yetu akiwa ughaibuni analivaa. Akishuka uwanja wa ndege analivua anaendelea kupuyanga. Mabarakoa yamekuwa kama fasheni ya kubandika na kubandua. Unaangalia tu mazingira muafaka. Barakoa...
  5. Lorenzo Samike

    Rais Samia usifungue milango ya uchawi: Uchifu ni mamlaka za shetani

    Hakuna mahali popote katika historia ya nchi hii, kabla ya ukoloni, kwamba palikuwa na machifu. Machifu ni watawala wa mkoloni waliosimikwa kwa ajili ya kazi ya mkoloni. Divide and Rule tactics. Hawa ndio waliohusika kuwauza wenzao utumwani. Neno lenyewe ni la Kiingereza "CHEIF". Baada ya...
  6. Lorenzo Samike

    Rais Samia usikaze shingo, Ndugai anayo hoja

    Hii tamaduni ya marais wa nchi kugangamara kwa kila jambo hauna afya kwa taifa. Umeelekezwa, sikiliza. Rais sio Mungu, lazima ukosolewe ikibidi. Lazima nchi ijifunze kujitegemea. Huwezi kuwa taifa la kuomba omba kila siku. Ni kujilemaza. Ni kweli, inawezekana kujitegemea kiuchumi ni jambo...
  7. Lorenzo Samike

    Rais Samia, nchi haijengwi kwa kuzurura

    Mpendwa Mama Samia, Nchi hii haiwezi kujengwa kwa kuomba omba. Nchi inajengwa kwa kazi, bidii, na nidhamu ya utumishi wa umma. Nchi yetu imebarikiwa kila aina ya rasilimali: Maji, Mito, Mabwawa makubwa, maziwa, madini ya kila aina, gesi, mafuta, chakula, nishati, ardhi kubwa yenye rutuba...
  8. Lorenzo Samike

    Rais Samia katika uzani wa Magufuli : Duru za Uchaguzi mkuu 2025

    Kwa jinsi ambavyo hii nchi ilikuwa inaendeshwa na genge la mafisadi chini ya utawala wa awamu ya nne, ni wazi kwamba bila Magufuli, CCM ingeshakuwa imejifia kabla ya 2015. Uzembe, udhaifu, wizi, ubadhirifu, ulegevu na mauchafu ya kila aina yaliyoratibiwa na Rais wa awamu ile, yalifanya wananchi...
  9. Lorenzo Samike

    Rais mlalamikaji: Je, ni udhaifu?

    Kwanini huyu mama yetu mpendwa samia analalamika tu bila kuchukua hatua? Wananchi wanapenda kuona Rais mwenye uwezo wa kutumia Mamlaka tuliyompa. Yaani watu milioni sitini wa nchi hii, wote kwa pamoja tumekukabidhi wewe mamlaka yote lakini bado unalia lia tu kama mtu mwingine wa kawaida...
  10. Lorenzo Samike

    Rais punguza safari, jikite kujenga nchi

    Nawasalimu kwa Jina la Mungu muumba wa mbingu na ardhi. Jamani, kusafiri ni jambo jema katika kujenga diplomasia na mahusiano ya nchi na nchi. Haipingwi wala haina neno. Lakini hii kutwa mama wa nchi kukimbizana angani kila wiki inakuaje? Leo yuko Scotland, kesho Cairo, kesho kutwa Ubelgiji...
  11. Lorenzo Samike

    Usalama wa Taifa mchawi

    Kuna mzee mmoja ana umri wa miaka 70 hivi. Ni mstaafu wa Idara ya usalama wa Taifa. Mimi sifahamu vitengo vilivyo ndani ya idara hii, kwahiyo sijui ni kitengo gani ndani ya idara alichokuwa anafanya kazi lakini alikuwa humo. Alikuwa ni Land lord wangu miaka kama minne iliyopita. Ni mzee lakini...
  12. Lorenzo Samike

    #COVID19 Mahakama iweke zuio dhidi ya chanjo za UVIKO-19

    Cc: Andiko hili liwafikie wanasheria na wote wenye kuhusika. Nchi yetu ina Katiba, sheria, kanuni, miongozo na taratibu — za ndani na za kimataifa. Katiba yetu inatambua haki ya kuishi, kulindiwa afya, kuwa na maamuzi sahihi na taarifa sahihi juu ya yote yahusuyo mustakabali wa maisha yetu...
  13. Lorenzo Samike

    Kodi mpya za miamala: Mahakama iweke zuio la haraka

    Huu uharamia wa kodi mpya za miamala ya simu unapaswa kusimama. Wanasheria wetu mtusaidie hili. Hakuna kitu kinachoitwa sijui "kodi ya uzalendo" — Lazima Mahakama iweke ZUIO la hizi kodi za kitapeli. Hauwezi ukakata kodi mara tatu kwenye muamala mmoja. Huo ni uhuni na wizi. Hizi ndizo kodi za...
  14. Lorenzo Samike

    RC Anthony Mtaka ana sifa gani spesheli?

    Huyu anayeitwa Anthony Mtaka ni muda sasa nimeanza kumsikia lakini sikumtilia maanani kivile. Hata wakati wa Magufuli nilikuwa namsikia sikia tu kwamba ati ni Mkuu wa Mkoa bora. Akapewa sijui na tuzo! Binafsi sikuwahi kumfuatilia kwa sababu sikuwahi kuvutika nae. Nilikuwa namsikia sikia tu kwa...
  15. Lorenzo Samike

    Kiingereza cha Diamond ni "chefu chefu"

    Ukisikia "kizungu-chefu chefu" ndio cha huyu Bwana mdogo nguli wa bongo fleva. Huyu Bwana mdogo wa Tandale sijui katoa wapi hii kizungu ya kimarekani? Sijui ndio kuwa NIGGA? — Bado sijamuelewa vizuri. You garrah gooh... i garrah duuh, i garrah fyoko, yoooo ma nigga, i garrah nyokooh...
  16. Lorenzo Samike

    #COVID19 Corona iko maeneo gani Tanzania?

    Hey, Nawasalimu kwa Jina la Jamuhuri Ya Muungano wa Tanzania. Hivi majuzi juzi tumesikia taarifa lukuki kuhusu corona. Wengine nimesikia wanasema kwa sasa hili ni wimbi la tatu — Wengine wanaita sijui DELTA kitu gani gani?? Majina yamekuwa mengi kidogo. Kuna DELTA na kuna wimbi. Kiuhalisia...
Back
Top Bottom