Kitila Mkumbo ni msomi aliyebobea na hata ushauri wake ni wa kisomi. Kweli kakosea ila kusamehewa pia kungefaa sana maana hata kumvua nyadhifa zake ni adhabu ya kwanza tosha. Ila yote yamepita ikitokea tena tupunguze hasira kabla ya kufanya maamuzi.
Hiyo iko wazi kbs kuwa vodacom wana matatizo makubwa sana hata ya usikivu wakati unaongea. Hili la wizi limekithili kwani unawekewa wimbo na kukatwa bila ya wewe kuomba wimbo husika. Huu sio mtandao kabisa jamani.
Nafikiri yaliyoandikwa yote huyo Bi. Senso msemaji wa jeshi la Polisi ameyasoma na kuyaona na wote walioandika si wajinga na si wote hawalipendi jeshi la polisi ila ajibu swali kuwa Yuko wapi mtuhumiwa, nafikiri angejibu alipo yote yaliyoandikwa yasingekuwepo.
Ni vema matatizo haya yakashughulikiwa kwa karibu maana hizi kauli za viongozi wa juu zinaweza tumiwa vibaya, serikali ichunguze na kuhakikisha kuwa waliohusika wanakamatwa hata kama wamo ndani ya serikali.
Mh. Pinda nenda taratibu hata mikutano yenu watu wataisusia maana wataogopa kupigwa, kumbuka kauli ya Rais wetu wakati akiongea na wazee Dar. kuwa wafanyakazi kura zao hazitaki ilivyosumbua chama. Nafikiri ni kuangalia wale wanaoleta fujo na wakathibitika kwani kuna wakati unahudhulia mkutano na...
Inatakiwa Police wajue kuwa wao ni walinzi wa usalama wa raia na mali zao maana si kweli kuwa hakutakuja kuwa na mabadiliko nchini, hilo lazima walijue hivyo wao waangalie usalama wa raia 2.
Nafikiri hawa wabunge we2 wanapaswa kufikiri kabla ya kuongea kwani inaonekana ni namna gani thinking capacity yao ilivyo ndogo na ndo maana wanapitisha baadhi ya sheria wakitoka nje ya ukumbi ndo wanaona makosa yake; kwa hili machali hatakiwi kulaumu direct CDM maana pale jukwaani walikuwepo...
Nafikiri Bw. Mwigulu utajipima sasa kuwa ni kwa namna gani watu hawakupendi kwa ambayo yanasikika kutoka kwako, jua kuwa hata mchawi anawanga peke yake usiku lakini asubuhi watu wanajua, kwa hiyo nawe jitathimini na angalia utendayo na heshimu vyama vingine pia. Kumbuka kuwa kuna siku chama...
Sitaki kuamini na kufuata malumbano ya hapo juu ila yote kwa yote tusubiri uchunguzi na tuiamini serikali maana bila kuiamini serikali tutakuwa hatutendi democrasia ambayo ndiyo tulioiweka madarakani ili ituongoze.
CDM tulieni panganeni vizuri malumbano ni sehemu ya maisha, baada ya hayo gangeni yajayo na kila mchezaji ashike no.yake vizuri tuhakikishe hatufungwi goli lolote maana mkiendeleza malumbano mtafungwa mabao mpaka basi na nyumba nyeupe mtaiona ikikaliwa na wale wale wa miaka yote bila mabadiliko.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.