Maelezo sahihi. Asante sana. Kwa kuongezea tu, wengi wetu huwa hatuna utamaduni wa kusafisha matenki ya mafuta ya magari yetu. Gari ya mwaka 2000, na unapenda kuweka Lita tano tano, na wakati unawekewa mafuta huzimi injini, mafuta yanaingia kwa msukumo mkubwa kwenye tenki na yanavuruga uchafu...
Unaweza kununua gari yenye km idadi yoyote, kutegemea mfuko wako. Wingi wa km inamaanisha pia uchakavu wa injini. Injini ndiyo kinu cha kufua nguvu ya gari. Ikiwa injini itakuwa imekwenda km nyingi, maana yake inaashiria kwamba msukumo sahihi wa injini hiyo utakuwa umepungua ukilinganisha na...
Hakuna tofauti ya ulaji wa mafuta kati ya injini mbili zenye ujazo sawa wa 2000 lakini tofauti ni idadi ya cylinder. Faida moja tu ya kuwa na cylinder nyingi kuliko chache ni kwamba kishindo kinachotokea baada ya mlipuko wa injini (impulse) kwa kila mzunguko wa injini (engine revolution)...
Shabiby hajakemea ukwepaji Kodi, bali anataka ukaguzi wa wachakachuaji upigwe marufuku eti wanaonewa wauza mafuta. Alikamatwa January mwaka huu, akalia kwa Prof Muhongo ewura hawakumwachia, akalia kwa PM hakuachiwa, sasa anataka utaratibu huo uachwe.
Susuma,
Baada ya uchakachuaji kubanwa, biashara kwa baadhi yetu ngumu, hivyo wengine wanaponea kupiga dili za transit. Ndo maana Lake Oil aliibuliwa, Sasa Shabiby, Mbunge wa David Matayo na Mansoor wa MOIL wote wameungana wanataka serikali iachane n fuel markIng ili warudishe pesa
King Kong, ukitafuta bei na uwiano wa hesabu za kushuka kwa crude oil kwa pipa kwa hesabu zako hutaweza kupata. Kwa sababu sote hatuna uwezo wa kujua gharama za kusafisha hayo mafuta, kuyasafirisha kutoka yanakosafishwa hadi yanakonunuliwa. Tanzania hatuagizi mafuta machafu. Tunanunua...
hiyo swali namba 1 mbona impact yake ilipita kaka? na hata ukiangalia kwenye machapisho ya ewura, miezi ya eneo hilo inajieleza tu. Nikipata chapisho hilo nitaliweka hapa. Kumbuka, kila Jumatano ya mwanzo bei hizi zinatangazwa na sisi tunabadilisha.
MKuu Adolay, jambo lingine unalosahau ni kwamba hizo data za world market siyo za mwezi au kipindi kimoja, siyo bei za mara moja. Ni hesabu za cummulative, unapoambiwa bei sasa zimeshuka hadi kufikia "more than 70% collapse in oil prices since the middle of 2014." haina maana sasa au mwezi huu...
MKuu Mkoroshokigori,
msikubali kudanganywa kirahisi. Nenda hapa Pump Prices
utapata bei za mafuta Kenya. Ukiona uvivu, Nairobi lita ya Petroli ni sh. za Kenya 88, ambazo hapa ni sawa na sh 1, 885. Mbona tunadanganywa kirahisi hivi na taarifa zote ziko mtandaoni?
Mwaraby wa Dubai, kila lita ya petroli unalipia kodi sh 752. Ina maana hata ungepewa bure kule, unabeba kwenye begi, bado hapa ungecheua sh 752 serikalini. Upo kaka?
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.