Nakurudisha miaka mitatu iliyopita, Rais Samia alipotangaza msiba wa Magufuli alitangaza siku 7 za maombolezo kwa mara ya kwanza. Wakati huo hakuwa anajua Katiba inatambua siku 21. Hili linatosha kuonesha kuwa Viongozi wengi walikuwa hawana ufahamu na katiba
Mahojiano ya Mabeyo ya hivi karibuni...
Nimeangalia data kutoka TRA kujua tumekusanya shilingi ngapi tangu serikali iweke tozo kwenye miamala ya simu, hadi sasa tumeshakusanya Tsh Bilioni 362.1281, hii ni kuanzia zilipoanzisha hadi robo ya pili ya mwaka wa fedha 2023/24
Ukiangalia takwimu hizo kuanzia Juni 2022 makusanyo yalipungua...
Uchumi wa Tanzania kwa asilimia kubwa upo kwa wageni. Yes! Matajiri wengi waliopo Tanzania sio watanzania kwa asili, wengi wana asili za nchi nyingine. Hii ni kwasababu hatuna akili za biashara kabisa. Niliposoma gazeti hili la majira kuhusu sakata linaloendelea ndio nikaona shida zaidi.
Agha...
Achana na maandamano ya CHADEMA, miaka kadhaa iliyopita kulikuwa na maandamano ya wamachinga. Mtu mmoja ambaye alitajwa kuwa msemaji wa wamachinga alirekodiwa akiwataka watu wengine wasiandamane kwa kuwa wakivunjwa miguu watakaoathirika ni wao na sio walioandaa maandamano.
Nilipoona video ile...
Matokeo ya kidato cha nne yameacha kujadiliwa, kama kawaida waandishi wameripoti bila kwenda kiundani zaidi kusema matokeo haya yana maanisha nini kwa jamii. Hata hivyo kuna mtu ndani ya JF alienda mbali kufananisha ufaulu wa hisabati na Urai na aliangalia pia fedha zinazowekwa kwenye hisabati...
Kiafrika Rais ana nguvu kubwa sana, mtu akizeeka uwezo wake wa maamuzi hupungua, hivyo kuwa na marais wazee ni kujiingiza kwenye hatari zaidi ya kupata maamuzi mabaya yatakayoathiri taifa kutokana na nguvu ya rais na umri wa rais.
Suala la tuanze na umri gani kwa mtu kuwa rais, kwanini miaka...
Nchi kadhaa zimekuwa na mijadala juu ya ukomo wa umri ambao rais anatakiwa kutovuka ili kuendelea kutawala. Hata hivyo, baadhi ya marais wamekuwa wakibadili katiba zao ili kuhakikisha wanabaki madarakani. Hii sio shida lakini ni muhimu ukomo wa umri uwepo ili kutokuwa na marais wazee ambao...
Nilinunua sukari nyingi ya kunitosha mwaka mzima (Kwa kuwa naishi mwenyewe ni rahisi). Baada ya kuja suala la kudhibiti bei ya sukari, nadhani wafanyabiashara wako katika mgomo fulani. Jana nimeenda supermarket wamenambia hawana sukari.
Nadhani badala ya kudhibiti bei kuna namna sahihi zaidi ya...
Mtandao ya simu imerahisisha huduma ya kulipa vitu mbalimbali ikiwemo malipo ya serikali na biashara binafsi. Ni kawaida kwa sasa kukuta biashara ina LIPA NAMBA ambapo mtu anaweza kulipa kwa namba hiyo.
Hata hivyo katika kutumia lipa namba, kuna gharama ambayo mteja anakatwa, lakini gharama...
Mvua zimeleta majanga na kuacha majanga. Lakini Mvua zisingekuwa na maafa makubwa kama tungekuwa na mifumo mizuri ya maji taka. Kwa kuwa na mifumo mibovu maji yamejitengenezea njia zake na kuharibu miundombinu mingine. Barabara nyingi sana haziko katika hali nzuri na zinaweza kuharibu magari...
Katika bara la Afrika, nchi zimekuwa tegemezi kwa mazao machache ya chakula. Sasa hivi, spishi 20 za mimea zinatoa asilimia 90 ya chakula chetu, na tatu kati ya hizo – ngano, mahindi, na mpunga – zinaleta asilimia 60 ya kalori zote zinazotumiwa kwenye bara hili na duniani kote. Hii inaondoa...
Historia ya utungaji na upitishaji sheria nchini Tanzania, kwa mujibu wa tovuti ya bunge ni kuanzia mwaka 1963. Miaka miwili baada ya kupata uhuru, mwaka 1963 tukaunda sheria 246, hizi ndio idadi kubwa ya sheria kuwahi kupitishwa katika historia ya Tanzania. Aidha baada ya mwaka huo mwaka...
Maxence Melo, Mkurugenzi Mtendaji wa JamiiForums ameteuliwa kuwa mmjoa wa wajumbe wa Bodi ya Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi kwa muda wa miaka mitatu. Suala hili limezuia mijadala hata kwa wanachama wa JamiiForums wakidhani uhuru wao utakuwa umeminywa.
Unayopaswa kujua
Bodi inayoundwa ni kwa...
Bunge la Rwanda limeidhinisha muswada unaosimamia usalama wa maumbile, lengo likiwa kushughulikia hatari inayoweza kutokea kwa GMOs ili kulinda bioanuwai na kuhifadhi wa mazingira.
Viumbe vilivyobadilishwa maumbile(GMO), kama vile mazao, ni vile vilivyobadilishwa kwa kuongeza jeni kutoka kwa...
Kifungu cha 171A cha Kanuni za Adhabu kimejinaisha Ponzi Schemes na Pyramid schemes ambazo kwa muda mrefu zimekuwa zikiwaingiza mamilioni ya watanzania katika kilio.
Kulikuwa na DECI, Kalynda, ambazo zilikuwa Ponzi Scheme, hata hivyo kwa Pyramid Schemes zimekuwa nyingi huku wengine wakitumia...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.