Nimeona niliweke hili ili kuwaweka huru wengi wetu, ambao tunakimbilia kununua simu za bei ghali halafu mwisho wa siku unaweka bando la mia tano (500) kwa mwezi.
Hizo hela za simu afadhari ungeweka bili ya maziwa ya ng'ombe kwa Massawe kuhimarisha afya ya mwili na akili.
Tusipende kuiga ili...
Hili ni wazo jipya la kuishauri serikali, kwa sababu hii nchi ni kubwa, kuwe na dawati la kero mtandaoni kwa kila wilaya. Hii itasaidia viongozi wa juu kuona live kupitia mtandao kero za wananchi mojamoja bila kupitia kwa wakurugenzi au kwa viongozi wa wilaya.
Hii ni dawati huru la wananchi...
Utakuta mtu biashara ya gesti wanaolala ni waswahili, lakini bango huko nje limeandikwa " Peice guest house" hakimanisha peace. Wengine utakuta JB HAIR SALOON badala ya salon. Wengine utakuta wameandika HALF LONDON LOGDE badala ya Lodge. Hivi ukitumia kiswahili wateja utakosa??? Ni lini...
Mimi sijui kwa nini ile reli yetu ya kaskazini ilikufa na tufanyeje ili hii iliyofufuliwa isife kamwe? Tumejifunza mengi sana kwa hayati John Magufuli, na Mungu amuweke mahala pema peponi. Mimi nahamini kila binadamu ataenda peponi na hilo ndiyo kusudio la Muumba wetu.
Je kuna nini cha...
Heri ya Chrismas na mwaka mpya wapendwa wote na Watanzania kwa ujumla.
Tumuombe Mungu wetu atujalie upendo na amani katika kipindi hiki cha sikukuu.
Ujumbe: Chombo cha moto na pombe ni mauti. Tuepuke ulevi kama utaendesha vyombo hivi.
Sent using Jamii Forums mobile app
Nimenunua kitabu hiki bei nzuri sana. Ni kitabu cha mtandaoni kwa ku-download kipo Amazon, ni hadithi ya kweli kwa huyu mganda. Bei haizidi elfu saba 7000 za Tanzania. Kwa wale tusiopenda hadithi ndefu sana kwenye vitabu, hiki kizuri sana. Tatizo lugha ni kizungu, lakini kinaeleweka. Ahsante.
Wanajamvi, mimi natafuta kazi ya udereva wa magari makubwa au madogo si za abiria. Nina leseni ya magari magari ya mizigo lakini toka nimalize chuo cha udereva huu kazi bado sijapata.[emoji18] [emoji18] nina umri wa miaka 37. Sinywi kelevi wala sivuti sigara au mengine. Ahsanteni
watu wanasema "siasa mchezo mchafu", ni kweli kabisa. Yaliyotokea Kenya ni kuonyesha kukua kwa demokrasia nchini huo na ni mfano wa kuigwa baran Afrika. Pamoja na kwamba Kenya imeonyesha njia kwa nchi nyingine, lakini bado tunajiuliza kwa nini uchaguzi urudie ? kwa nini wasifanye kuhesabu kura...
Kila mtu anajua umuhimu wa mawasiliano popote pale ulipo kuwasiliana na jamaa au ndugu kwa kikazi pia. Swala langu ni kwa nini iwe rahisi kupiga simu Kenya kutoka Uk kuliko Tanzania? Utakuta bei ya kupiga kenya ni 6.6p/m wakati huo huo Tanzania ni 21.9p/m unashika Kichwa na kuwaza kuna...
Ningeomba sana serikali yetu iwakumbuke Alibino kwa kuwapa mafuta na miwani ya kuzuia makali ya mionzi ya jua bure au kuondoa kodi zake zote ili wenzetu wapate unafuu wa mafuta haya. Nasema hivi kwa sababu hili ni tatizo la taifa na siyo mtu mmoja mmoja uwezo na nia ya kuwasaidia kama taifa ipo...
Kitu gani tufanye kikubwa na chenye akili ili tuonekane na sisi ni binadamu wenye vipaji vikubwa na hatukustahili kuuzwa kama mbuzi enzi za utumwa?
Sent using Jamii Forums mobile app
Ni mambo ya kusikitisha sana na inafedhehesha wateja haswa wenye vibegi na mifuko kuwaomba wakabidhi kaunta kabla ya kuingia kwenye maduka yao haswa makubwa.
Yaani mteja ni mwizi badala ya mfalme?Kwanini ukabidhi vitu vyako kutoka maduka mengine au mali zako kaunta? Biashara mnayofanya...
Obama hakupenda sana Trump kuingia Ikulu lakini basi Demokrasia ndiyo imeamua.Siyo lahisi kuimiliki demokrasia ya kweli. Uzuri wa demokrasia ya kweli ukifanikiwa kuimiliki hudumu milele.
Sent using Jamii Forums mobile app
Kama wewe ni muislam, mkristo, mpagani au huna dini. Ni kipindi kizuri sana cha kuiombea nchi yetu kwa imani yako. Ili utukufu na amani ya Tanzania iendelee kudumu milele na Mungu awe kiongozi wetu siku zote. AMEN
Sent from my HUAWEI M2-A01W using JamiiForums mobile app
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.