Hmm Warusi walikuwa na kazi nyingi kugandamiza upinzani. Kherson nakumbuka wananchi waliandamana sana wiki za kwanza hadi wengi walikamatwa na kupigwa. Putin alilazimishwa kuendesha referendum kwa mbio maana alihitaji kitu cha kuonyesha baada ya kupigwa vibaya vile katika maeneo ya Kharkiv...
Ona ramani ya LYman leo. Putin alikataza askari wake wasirudi nyuma. Hivyo alitoa hukumu ya mauti kwao (au ya kufungwa). Kuna njia moja tu kutoka Lyman kuelekea Mashariki - njia hii iko umbali kwa silaha za kila aina hata silaha ndogo za Ukraine.
Mara itakapotokea, tuwasikie tena waimbaji wa genius!
Safi. HAdi jana Waukraine hawakuruhusiwa na Marekani kupiga eneo la Urusi. Sasa wanaweza kuendelea kupiga eneo la Urusi na wakati huohuo wako nyumbani kwao...
Maskini, wanabaki peke yao kwenye uwanja. Hata wakijaribu kumchafusha Katibu Mkuu wa UM anayefanya tu kazi yake na kukumbusha misingi ya sheria ya kimataifa iko namna gani.
Tuone Putin anaweza kununua wangapi watakaotambua wizi wa maeneo hayo.
Mbona unaleta video ambayo huelewi?
Hao jamaa wote ni wageni na watalii wa kidini. Katika Ukraine kuna maeneo makubwa yaliyokaliwa hasa na Wayahudi hadi 1941 kabla hawajauawa (Maangamizi makuu dhidi ya Wayahudi wa Ulaya - Wikipedia, kamusi elezo huru).
Kuna makaburi ya marabi mashuhuri...
Muone hali ya mstari wa mapigano leo jioni huko Lyman karibu na Slyovansk / Kramatorsk. Nyekundu ni eneo linalosjikwa hapa na Warusi. Inasemekana Putin alikataza wasirudi nyuma. Hivyo wako hatarini kuzungushwa.
Jamani Mungu abariki roho yako ya kitoto! Waliondoka Urusi ni wanaume 300,000 hivi. Wewe unaamini ni majasusi?? 😂😂😂 Yaani miaka hii yote walikuwepo majasusi 300,000 nchini Urusi na huduma za usalama wa Putin hawakujua kitu?? Safi sana!!
Au ni kawaida yako kutumia maneno kama matusi tu bila...
Ndiyo, bomba la Northstream 2 kutoka Urusi hadi Ujerumani ilikuwa tayari tangu 2021 na kujaa gesi. Ndani ya Ujerumani kulikuwa na majadiliano kuifunga au la. Marekani, Poland na nchi za Baltiki pamoja na Ukraine zilipinga bomba hili zilidai Ujerumani lisitumie wakaona hatari ya kutegemea Urusi...
Mali ya Urusi? Kwa sababu Bwana Putin anaandika jina kwenye karatasi?? Unachekesha.
Kati ya Mikoa minne, kuna moja tu ambako ameshashika zaidi ya 90% - kwa sasa. Mji wa Zaporishia (makao makuu ya mkoa) hana. Donetsk ana 60% hadi sasa...
Unapenda hadithi za Abunuwasi ?
Hakuna aliyeleta habari kwamba Urusi haina chakula. Wote wanajua Urusi bado kuna chakula tosha. Unadanganywa na propaganda au umeamua kusambaza propaganda.
Habari ilikuwa vikosi kadhaa za Urusi zilitumwa (na zinatumwa) katika mapigano bila chakula cha kutosha. Ambacho ni ukweli Mtupu...
Nani anaathirika kiuchumi kutokana na kubomoa bomba ambako hakuna gesi inayosafirishwa? Maana tangu wiki hakuna m³ iliyopita??
Labda ile ya kuepukana na kulipishwa kwa kuvunja mikataba . . ?
Naamini una uwezo wa kusoma mwenyewe habari. Sijui kama unataka kusikia habari halisi. Ni shauri lako. Siwezi kufurahia kama nchi kama Urusi inatuma watu wake wafe - na wasioandaliwa watakufa wengi.
Habari za Warusi eti wanatumwa bila maandalizi ni nyingi. Orodha zinazorushwa na askari wapya...
Hizi habari za ajabu. Kuhusu askari mpya kupewa bunduki zenye kutu. Askari kutumwa mbele kwenye mapigano hata bila mafundisho ya wiki moja??
newsweek.com
Mobilized Russians Sent to War After Two Days of Training: Rights Group
Russian State Media Figures Rail Against Army’s Mobilization...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.