Nimekuwa mwanachama mwaminifu wa CHADEMA ninayemiliki kadi no. CDM 0413468 tangu mwaka 2009. Nimewahi kukitumia chama katika nafasi ya uongozi nilipokuwa chuo kikuu na hata mtaani huku kanda ya ziwa. Nilipata kufanya kazi kwa ukaribu kabisa na viongozi wakubwa...
Nimefuatilia kwa umakini mkubwa kuhusu kinachoitwa Kamati ya Maadili ya CCM na kugundua kwamba ni genge la viongozi waandamizi wanaofanya pamoja na kazi nyingine, kubwa ni kupandikiza viongozi wapya madarakani ili waende kulinda maslahi yao. Wakati ambapo kina Steven Wassira wakiwapiga ngumi za...
Hakika kwa kila mmoja aliyepata kushuhudia hotuba ya Mhe.Mbowe katika mkutano wa kumkaribisha aliyekuwa Waziri Mkuu wa awamu ya nne Mhe.Edward Ngoyai Lowassa ametoa hotuba bora sana. Kwa wale waliodhani kiwango cha elimu ni kipimo cha ustaarabu, hekima na uelewa basi...
Wakati ambapo wadadisi wa mambo ya kisiasa wakichunguza na kufuatilia kwa umakini ikiwa sheria ya uchaguzi ya kudhibiti gharama za uchaguzi iliyotungwa august, 2010 itafanya kazi lakini mambo ni yamethibitika kuwa tofauti kabisa.
Licha ya ukimya wa TAKUKURU kuhusu tuhuma zilizosambaa mjini...
Katika moja ya wosia wake Baba wa Taifa, Mwl.Julius Kambarage Nyerere aliwahi kusema, "haitoshi kwa mtu mmoja kuwa mwadilifu maana kuna vishawishi vya ndugu, jamaa na marafiki hivyo ni lazima mtu awaambie ukweli, hata wale wanaomzunguka kwamba IKULU ni mahali patakatifu..."...
Katika safari ya maisha ya siasa kuna hatua nyingi kama vile kuzaliwa kwa chama cha siasa, kukua, kuimarika,kudumaa na kuanguka. Leo kwa kukiangazia chama cha zamani CCM, pamoja na sifa nyinginezo katika political life cycle, chama hiki kilishafikia hatua kuu mbili za mwisho yaani...
Nawasalimu wanajukwaa wote! Kama alivyowahi kunena George Herbert kwamba, "The best mirror is an old friend". Kutokana na harakati za uchaguzi BAVICHA kushika kasi, nimeona ni vema mkamtambua mmoja kati ya Kamanda anayetajwa kugombea Uenyekiti BAVICHA-Taifa ndugu Patrobass Paschal Katambi...
Wasalam ndugu,
Suala hili linaniumiza kichwa sana tangu harakati za awali za kutafuta namna ya kutatua kero za muungano mpaka hatua ya kuandika katiba mpya.
Bila shaka, mpaka sasa kuna makundi yaliyogawanyika kwa mujibu wa maoni yao...
Mimi nilifunzwa adabu na utii tangu utotoni mpaka sasa, hivyo awali ya yote napeleka heshima zangu kwa Mzee Mangula kwani amekuwa na mchango mkubwa kwa chama cha zamani licha ya kushindwa kuwatimua ndani ya miezi 6 wa-NEC waliopita kwa rushwa. Kwa jinsi nilivyomfuatilia huyu...
Wasalamu ndugu; Mara nyingi huwa natenga muda kuchunguza yanayozungumzwa na viongozi leo kwa kulinganisha na yale waliyonena jana. Kama ilivyo ada kwamba mkubwa ni jalala, nimeamua kupima kauli za Mwenyekiti wa CCM na Rais wa JMT Mhe.Dr.Jakaya Mrisho Kikwete na kugundua...
Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA (Zanzibar) ameacha gumzo na hamasa kubwa ya kisiasa mjini Geita kutokana na darasa alilotoa jana katika uwanja wa magereza.
Kamanda Said Issa Mohammed amezima gafla propaganda chafu zilienezwa na CCM kwa muda mrefu kwamba CHADEMA ni chama cha ukristo kwa vile...
Previously:
Updates:
Hatimaye Kamanda wa anga awasili kwa helikopta na umati mkubwa unamshangilia Mhe.Mbowe. Hali ya hewa si nzuri sana kwani mvua imenyesha na manyunyu yanaendelea lakini watu wanazidi kumiminika kuja katika uwanja wa magereza hapa Geita Mjini. Nitakuwa nawapa kila updates!
Mungu Ibariki Tanzania! Napenda na uneni wa wenye busara kwamba ukweli ni uhuru wa fikra na mwili.Na katika mfumo wa taasisi za kisiasa, ukweli ni msingi wa ushindi wa kisiasa kwa mantiki kwamba ukithibitika mbele ya umma kwamba taasisi inausimamia...
Awali nawatakieni happy boxing day. Bila shaka jukwaa hili ni kitovu cha hoja mbalimbali za kisiasa hivyo nami naweka rekodi yangu katika historia yangu, kwa upande wa pili nawasilisha mtazamo wangu juu ya umuhimu wa kuheshimu taasisi (chama) badala ya watu binafsi nikiwemo mimi. Mpaka...
Ndugu zangu sina papara za x-mass wala mwaka mpya.Papara zangu ni kutafuta kitambaa cheusi cha kujifutia machozi endapo msiba wa anguko la elimu mwaka 2012/2013 halitajirudia tena kwa msimu wa 2013/2014. Nakumbuka fika mwezi mei, 2013 pindi mjadala wa matokeo...
Kila mtu ana swali lake kuhusu sakata la Mhe.Zitto kusaini kiapo cha kukiri kutokuwa na majina ya Watanzania walioficha fedha haramu nchini Uswisi.
Hakika Mhe.Zitto Kabwe amejidhalilisha/amedhalilishwa sana na sakata hili kwa kuonekana mzushi, mwongo, na...
Habari wana MMU, Leo naomba tujuzane na kujadili athari ya watoto katika mahusiano baina ya wanandoa. Jambo hili linaweza kudhaniwa kuwa dogo lakini ukweli ni kwamba mahusiano ya wanandoa wapatapo watoto hutetereka kiasi kwamba mahaba ya busu,vicheko,kupapasana, n.k hubakia kuwa historia na...
Hodi hapa jamvini! Nimepita pita mara nyingi jukwaani MMU,nimegundua kuna watu wanateswa na mapenzi lakini majuto mengi sana hutoka jinsia ya kike. Mara nyingi nimeshuhudia wanawake wakitulaumu wanaume eti, "Wanaume hawatulii, wanaume...
Katika kile ambacho Mwanafalsafa Andrew Carnegie anakitambua kama, "Uncontrolled desire for something for nothing" viongozi wa Chama Cha Mapinduzi akiwemo Mwenyekiti wake kitaifa Mhe.Dr.Jakaya Kikwete wameonesha kukosa mantiki ya msimamo wao kuhusu haja ya kutambua kikatiba uwepo wa Tanganyika...
Sherehe za uhuru wa "TANGANYIKA" zimedoda. Mitaani watu hawana habari kwani wanaona mafanikio ya uhuru yamekuwa neema kwa wachache huku wengi wakiachwa kwenye wimbi la ujinga,maradhi na umasikini kinyume na ilivyotarajiwa na waasisi wa uhuru mnamo...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.