Kuendelea kutumia nguvu nyingi kumdhibiti Tundu Lissu ni kujitafutia hasira ya Mungu iwashukie kwa kasi Kubwa. Kwanamna nyingine nawezs kusema Kutumia nguvu nyingi kumdhibiti Tundu Lissu ni kutumia nguvu nyingi kushindana dhidi ya nguvu ya Mungu.
Enyi wanadamu mbona mmefungwa akili kiasi hicho...
Taifa Limependelewa na Mungu katika Mambo mengi sana,lakini hakuna Muujiza Mkubwa Mungu ameutenda ndani ya Taifa letu kwa Kumuokoa na kifo mmoja wa Raia wa nchi yetu ambaye alimiminiwa Risasi nyingi na bado Mungu hakuruhusu Roho ya Mh.Lissu kuacha Mwili.
Ili kama Taifa tuonekane tumerudisha...
CCM kwa muda wa miaka mitano mlivizuia vyama Vya upinzani visifanye siasa wakati huo nyinyi mkiendelea na kufanya siasa,Kipindi cha miaka yote mitano kwenu kilikuwa ni kipindi cha kampeni mkizunguka kila pembe ya nchi kufanya kampeni.
Inasikitisha kuona Leo hii wenzenu wa upinzani kila...
Tumeshuhudia kwa muda wa miaka minne CCM imefanya siasa za kiuchoyo kwa kuzuia vyama vingine visifanye siasa,kwa kisingizio kuwa ni muda wa kuchapa kazi.
Tumeshuhudia bunge letu likiingizwa gizani kwa kisingizio kuwa kurusha live ni gharama lakini tumeona kila Leo wakionyesha Mubashara ziara...
Najiuliza Swali hilo hapo juu Lakini nakosa jibu. Mwl Nyerere alitufundisha kuwa Binadamu wote ni sawa. Cha ajabu Leo hii uthamani wa Mwafrika aliyeko Marekani na Mwafrika aliyeko Bongo ni tofauti.
Wabongo wanalaani vitendo viovu vinavyo tendwa na wazungu dhidi ya Waafrika lakini hawalaani...
CCM ni kweli Wananchi wapo kimya, lakini msidhani ukimwa huu wa Wananchi ni kuonyesha kuwa wanafurahishwa na mambo yanayoendelea. Watu wengi wana hasira moyoni na wapo kimya kwa sababu wanajua wakiongea watakutana na kesi za uhujumu uchumi. Lakini ukitaka kujua hasira walizo nazo wananchi juu...
Hivi karibuni kuna Mtu mweusi ametendwa vibaya huko Marekani kitendo kilichozusha fujo Kubwa, huku watu wakikemea kitendo hicho. Lakini cha ajabu ndani ya Afrika Waafrika wenyewe wakinyanyasana kwa kiasi kikubwa sana.
Vitendo Vya kunyanyasani ndani ya Afrika ni jambo la kawaida lakini cha...
Nchi hii tangu tupate Uhuru IPO chini ya CCM na siyo Mbowe.
Umaskini wa nchi hii umeletwa na CCM siyo Mbowe.
Ufisadi Mkubwa tangu tupate Uhuru umefanywa na CCM.
Ukosefu wa elimu bora katika Taifa tangu tupate Uhuru umefanywa na CCM.
Uvunjwaji Mkubwa wa Sheria za nchi tangu tupate Uhuru...
Afrika ni makaburi ya waafrika.
Viongozi,wafanyabiashara na watu maarufu wakipata hela wanawekeza kwenye mabenki ya nje ya bara la Africa mfano Swaziland, UK n.k. wakiumwa wanaenda kutibiwa nje ya bara lao la Africa., watoto wao wanasoma kwenye mashule ya nje ya bara la lao la Africa.., lakini...
Mara kwa mara vijana wa CCM waliomwagwa mitandaoni kupiga propaganda kuwa Chadema imekufa inaonekana wazi wanapata tabu sana baada ya kuona malengo yao hayajatimia.
Lengo la CCM ilikuwa ni kuona Chadema imekufa kabla ya 2020, na mpaka sasa kwa kujifurahisha wanawasadikisha wale walio watuma...
Katika hali ya kawaida mtu yeyote ambaye dhamiri Yake haipo Hai (imekufa)anaweza kufanya jambo lolote baya na akajiona yupo sawa hata kama jamii nzima inamshangaa.
Katika Siku za hivi karibuni limeibuka kundi la vijana linafanya kazi moja tu ya kumshambulia kwa maneno makali pengine hata matusi...
Katika Siku za hivi karibuni kumeibuka kundi la vijana wa kike na wa kiume wakiporomosha matusi ya nguoni kwa Mh.Mbowe na vijana hawa hatusikii wakichukuliwa hatua yoyote na vyote vyetu Vya ulinzi.
Tabia hii inazidi kushamiri huko fb na hata hapa jamii forum mpaka nashangaa hawa vijana ni...
Nimekaa natafakari nimekumbuka namna CCM wanavyogawa vitu bure wakati wa kampeni huku kipindi hiki cha korona wanashindwa kugawa bure barakoa?
Ina Upendo wenu kwa wananchi ni wakati wa kampeni tu? Nafikiri kipindi hiki ni kipindi kizuri cha kuonyesha Upendo wa kweli kwa wananchi, kwani kutokana...
Mh. Rc Tafadhali tunakuomba achana kwanza kuwa mtetezi wa wabunge waliofukuzwa uanachama huko Chadema, badala Yake Shughulikia kwanza tatizo la bei ya nyanya kule Mgama.
Kilimo cha nyanya ni kilimo kigumu sana kinachohitaji uangalizi wa karibu sana,sasa watu wamehudumia nyanya na sasa wamefikia...
Wadau napata shida kidogo kuelewa, nimejaribu kufuatilia sakata mameya kuondolewa madarakani kwa sehemu kubwa unaona ni wakuu wa mikoa ambao nafasi zao ni za kuteuliwa ndiyo wamekuwa watengenezaji wazuri wa figisu zinazo watoa mameya madarakani.
Wateule hawa kama hawakupendi wanatumia madaraka...
Mhe. Alex Kimbe wakati nikiendelea kukuombea katika sala zangu, naomba nikupe ujumbe huu kuwa MUNGU YUPO UPANDE WAKO NA ANAKUPENDA SANA. Safari ya binamu duniani ni safari yenye dhoruba kubwa.
Binadamu anapozaliwa anazaliwa akiwa hana kitu chochote, hata nguo anayovalishwa baada ya kuzaliwa ni...
Siku chache zilizopita Marekani walimpiga marufuku Paul Makonda kuingia Marekani kwa kuwa mtu huyu ana tabia za kuvunja haki za binadamu, pia Ana Tabia za kudhurumu uhai wa watu.
Jana Makonda ameonekana akifurahia mtoto wa Mbowe kukutwa na Corona, ni wazi sasa kuwa Makonda anakosa usingizi...
Wakati Dunia ikiwa katika heka heka Kubwa dhidi ya ugonjwa wa Corona, Sisi tupo katika heka heka Kubwa sana Za kuondoa umoja wa kitaifa.
Matendo yanayofanywa na Baadhi ya watawala yanatia shaka juu ya uzalendo kwa Taifa. Leo Dunia IPO kwenye taharuki kutokana na corona lakini baadhi ya watawala...
Niwe tu mkweli,Mara baada ya tetemeko la Kagera mpaka juzi Mimi nilijiaminisha kuwa Watanzania hawawezi tena kuchangia tukio lolote la kijamii,mawazo yalitokana na watu wengi kukatishwa tamaa kutokana na hela zile kutopelekwa kwa walengwa.
Ni mazoea ya Watanzania kuchangiana wakati wa...
Nchi ni moja, Bunge ni moja, Serikali ni moja, Jeshi la polisi ni moja inakuwaje watuhumiwa tofauti wenye tuhuma za aina moja wanashughulikiwa kwa mitindo tofauti?
Sheria zetu kuna baadhi ya watu zimewafanya kuwa special? Inakuwaje wengine waendelee kusota lupango huku upelelezi haujakamilika...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.