Mie ningemuuliza kwa nini kuumba warembo (jamani kuna warembo!) halafu hapo hapo kubandika Amri ya Sita?
Kwa nini ametuacha tukatengeneza pesa halafu inatunyanyasa? Kwa nini anakubali ndugu zetu wengine wawe vichaa?
Umesahau ni yeye aliyewanyang'anya visiwa watu waliokuwa wamemilikishwa visiwa vidogo vidogo katika bahari ya Hindi enzi za awamu ya pili. Alipopewa tu uwaziri wa ardhi akatangaza kuvirudisha serikalini visiwa vyote
Kwa Katiba na muundo wa Tanzania ya sasa inawezekana Zanzibar kufanya mambo yao wenyewe kwa yale mambo yasiyohusu Muungano. Lakini haiwezekani "Tanganyika" kufanya mambo yake nje ya muungano. Hii ni kwa sababu Tanganyika haipo tena, sasa kuna "Tanzania Bara". Kwa mujibu wa katiba mambo ya...
Kwa nini Ngeleja asimamishwe kwa kushindwa kuleta unafaa na maendeleo katika wizara anayo iongoza kwa miaka 4 na zaidi sasa?
Kwa sababu huo sio utaratibu wetu. Mtu akipewa uwaziri hapimwi utendaji wake. Anaachwa tu hata kama hakuna analofanya, alimradi hajakorofisha wakubwa atakaa miaka yote...
Kwa kweli hapa ndo Bunge letu linatakiwa lioneshe kama kweli ni Bunge lenye meno au ni danganya toto tu. Kwa mtizamo wangu:
1. Hoja ya CAG kwamba ni kawaida taasisi kuchangishwa fedha wakati wa kupitisha bajeti ni hoja ya kizembe na ya ajabu kabisa. Sawa, ni kawaida, lakini je, hiyo ni kawaida...
Ni kama wengi wanatilia shaka ukweli wa habari hii, mimi nilisimuliwa na mfanyakazi wa TBA siku ile ile Waziri alipofanya vioja hivyo katika ofisi za TBA. Yote hayo ni kweli kabisa, japo ni ngumu kuamini kama Magufuli ndo angeweza fanya hivo.
Hata hivyo nasikia kuna kigogo mmoja ambaye ndo...
Watanzania tuna kazi kweli! Kila kitu kinatiwa siasa, mpaka kazi ya mwandishi! Ndo maana inakuwa ngumu kuchukulia habari ya gazeti fulani at face value mpaka tuchunguze chunguze kujua ni kweli au la! Sasa katika hali hii tutafika kweli? Tungetegemea gazeti la Gov likawa neutral lakini da!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.