Punguza ukali wa maneno.
Sina UKIMWI.
Nauliza suala la kiroho.
Inawezekana kweli mtu akaombewa na Mwamposa na kupona VVU?
Kama ni kweli,watu wangekuwa wanateseka na ARVs?
Wakuu habari!
Nilikuwa sehemu fulani jirani yetu kuna watu wengi wamekusanyika wanamuangalia Mchungaji Mwamposa kwenye TV.
Mara nasikia kuna mdada anatoa ushuhuda kuwa ameponywa V.V.U Kabisa.
Hili suala la Mwamposa kuponya V.V.U kwangu naona ni uongo wa mchana kweupe.
Au ni kweli??
Kwamba...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.