Huyo wa kukutana nae kwa mara ya kwanza at least angetumia kinga.
Ila kwa mtu wako hakuna namna km kaamua kukucheat...lkn pia kuna haja ya kujenga utaratibu w kupima. Just ushauri tu ingawa tunaishi kwa kuaminiana sana bila ya kujua kila mmoja ana dhamira gani kwa mwenziwe
Nimepoteza paka wanne ndani ya week 1, wameumwa hatujui nini mpk Leo...kutapika, kukosa appetite ht maji walikuwa hawawezi kunywa. Watatu wadogo wana km 2 months tu, na mmoja mkubwa kiasi alizaliwa mwaka jana. Kabaki mama yao tu na hivi km mwezi nilimfungisha uzazi. Yaani naandika hapa machozi...
Mie nna waswas hata hao wavuvi sijui kama wanakula hao samaki
Zanzibar vibua 4 elfu 10 kweli. Wakati zamani kdg tu hapo hio elfu 10 unapata ndoo nzima ta vibua
Kuna wanawake wanakuwa wapole na wakimya sana...kuongea wanajifunza wakishakuolewa kwa sababu ya maudhi ya wanaume zao. Sio kila mwanamke anampigia mwanamme makelele kwa sababu anapenda, wanaume wengine mmezidi maudhi, mnawadharau wake zenu, kwa sababu tu mtu anatoka kutafuta mkate basi anakuwa...
Wanaume hio michi yenu inajua kuwaponza. Wengine hamchagui minutes nyie mnatwanga tu. Hamjui kama minutes nyengine vinaleta mitosis na mabalaa. Utamu gani huo wa kuwatoa akili kiasi hicho khaaa!!
Uk, America, na nchi nyingi hizo zinazoitwa za kimataifa wananchi walifanya maandamano huku wakiwa wameshika mabango yalioandikwa free Palestine. London Bridge ilitaka ku fall down kwa uwingi wa watu
Hao Waisrael wanne hawawezi kubadilisha chcht, waache fujo
Ami au hio uloandika ammy ni baba mkubwa au baba mdogo. Mjomba ni hio hio mjomba yaani ndugu wa mama
Funga mlango pia unaweza kusema komea mlango. Na hio Korlmea au tia pete yaani ni ku lock. Lkn funga ya ku shut tunatumia hio hio funga mlango.
Hapo nilitegemea ungeongelea tunavyokata maneno...
Ila bokoboko zanzibar ni chakula hiko, ngano kwa kuku au nyama vinapikwa pamoja mpk vinakuwa laini sana then vinasongwa vinakuwa kama mseto wa mchele na chooko. So ukiwa zanzibar ukisema bokoboko wanajua bi hiko chakula.
Wali ukiwa mlaini sana huku kwetu unaitwa bondo. Ubwabwa mara nyingi...
Kweli, akikaa na mmakunduchi huyu au mtu wa nungwi haambulii kitu japo wanaongea kiswahili.
Mie nipo zanzibar miaka lkn mmakunduchi akichowea sifaham kitu
Au umsikie mpemba wa kijijini huko ndio utablow 🤣
Mkuu umesoma mass na volume pamoja na scales ⚖️ zake au physics ya form 1 ushaisahau.
Kuna vipimo vya uzito vinatumia spring balance au beam balance ndio hivyo vya kg. Na kuna vipimo vya volume-ujazo ndio hivyo vya lita. Mfano mafuta, maziwa, petrol ⛽️ n.k
Vipimo vipo vingi, cha kwako umetolea mfano wa fraction. Lkn kuna kipimo cha Kilogram ambazo ni gram elfu 1, nusu kg ni gm 500 na robo kg ni gm 250. Mchele, unga, sukari, nyama vinatumia hivo vipimo. Either kilo kamili au nusu au robo na kuna mawe special ya hivo vipimo wanatumia kwenye mizani...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.