kwenye instagram yake kuna hii video, inwezekana ndiyo shule anayoiongelea.
Angalia: Krystyna Pyszková on Instagram: "In Sonta foundation, we have started with new school construction where we will be able to provide quality education for the children. The school is supposed to be finished by...
Changamoto za kilimo haziishi. Yaliyonikuta, mahindi bado yapo shambani hayajakauka kufikia kiwango cha kuvuna yamepigwa na upepo yamelala chini, yanaanza kuharibika. Sina stoo ya kuyaweka na jua la kuyaanika halipo. (Video clip imekuwa kubwa imekataa kuattach)
Bei yenyewe hivi sasa ni ndoo ya...
Pandisha maji kwenye huo mwinuko then jaza kwenye tank zilizo juu ya huo mwinuko. Kutoka kwenye hizo tanks waweza kutumia drip irrigation kama unataka kusave maji pia kutegemea aina ya mazao, au fanya furrow irrigation japo hii inatumia maji mengi laki ni ni rahisi kutengeneza majaruba.
Kama...
Ni sawa mkuu, ila miaka mitatu iliyopita maji yalijaa sana. Kuna mahali nilikuwa nmeweka mbao za kusimika mashine (maboriti makubwa ya inchi4 kwa 6) Yote yalifuknikwa na maji. Ni bahati kuwa mashine ilikuwa haijasimikwa kwenye zege, ningepata hasara kubwa. Wenyeji wananiambia hiyo inaweza...
Engine no ya kichina, ni 20hp, na water pump ni zaidi ya hp 15. Inavuta maji inch nne na kuyasukuma kwa inchi 2 ndiyo maana yaweza kwenda juu zaidi. Angalia icha hizi
Tuanze , tufanye halafu tuone tunakwama wapi. Kama ni mtaji mkubwa tuiambie serikali iwekeze kwenye miudo mbinu ya kuvuta maji toka ziwani, kama ni sheria na sera tuiambie serikali iweke sera rafiki. Kwa mfano sera ya mita 60 ikitumika bila busara inzweza kuwa kikwazo lakini busara ikitumika...
Video ya mashine ikisukuma maji imekuwa ndefu hadi iwee edited.
Baada ya maji kufika shambani nilifanya jaribio la kulima mahindi ya kiangazi. Nilipanda mwezi wa nane. Unaweza kuona video hiyo yakiwa mwezi wa kumi October 2022. Hiyo video ya pili, maji yamefikishwa umbali wa mita 600 na urefu wa...
Pamoja na kwamba sikuwa na mahesab ya kitaalamu, ni kweli ilinigharimu sana, Lakini sasa maji yameshafika shambani umbali wa mita 300 na mwinuko wa kama mita 20 hivi.
Hapo maji hayajapanda unauliza kulima? Hatua kwa hatua utanipa ushauri maji yakishafika shambani.
Naamini mazao yoyote yanaweza kulimwa na yakaleta pesa maana unavuna wakati wngine hawana!
Mitambo yote hiyo ikishasimikwa lazima kuzuia isinyeshewe na mvua na kupigwa na jua pia. Hivyo kuna kukamilisha jengo dogo ambalo pamoja na kuhifadhi engine na pump, laweza kutumika kutunzia vifaa vidogo vidogo kama spanners, vipuri nk.
Unaweza kuona ziwa nyuma yake
Mimi natumia diesel engine. Naendelea kuweka maelezo kwenye thread ya kilimo cha umwagiliaji kwa maji ya maziwa. Fuatilia hapa Kilimo cha umwagiliaji kwa maji ya maziwa
KUJENGA MAHALI PA KUSIMIKA MASHINE
Pump nyingi zilizo madukani zina uwezo wa kuvuta maji kati ya mita 4 hadi 8. Kwa hali hiyo inabidi engine na pump isimikwe karibu kabisa na chanzo cha maji (ziwa). Katika maeneo mengi yanayofaa kwa kilimo, kando kando ya ziwa ardhi huwa ni tifutifu. Kujengea...
Tanzania imezungukwa na maziwa makubwa yenye maji mengi kama vile ziwa Victoria , ziwa Tanganyika, Ziwa nyasa nk. Mara kwa mara viongozi wetu wamesikika wakisema tutumie maziwa haya kwa kilimo cha umwagiliaji, na wakati mwingine watu hujishangaa kwa nini maji haya hayatumiki kwa umwagiliaji...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.