Search results

  1. Y

    Kila Kadi ya Simu ya Mkononi Kutozwa TShs. 1,000 Kwa Mwezi

    Mkuu, ili kuonesha kuwa unajali na ni mkweli ungetuwekea bandiko la hiyo hotuba ya Mhe. waziri, kipengele cha tozo la kila mwezi la sh. 1,000 ambacho Mhe. Zitto anasema kakikuwepo nawe wasema kilikuwepo.
  2. Y

    Kazi nzuri Tundu Lissu Antipas!

    Comments zingine huwa zinachekesha sana. Mkuu, kama hayo uliyoyasema ni ya kweli, inakuwaje serikali yenye vyombo madhubuti vya ulinzi na usalama ya Tz imeshindwa kuwachukulia hatua za kisheria hao wahusika uliowatuhumu kwa uchafu na makosa hayo uliyayataja???!!!!
  3. Y

    Kazi nzuri Tundu Lissu Antipas!

    Mkuu, pamoja na msimamo wako "ulio thabiti" kwa hoja hii, ni ukweli ulio wazi kwa wanaoamini uwepo wa Mungu kwamba yupo upande wao CDM. Hii ni kutokana na kuweza kuruka vihunzi na mikwamo mingi iliyopata kuwekwa juu yao. Kama hayo ni ya kweli kwa nini wasiamini kwamba Mungu yu upande wao?
  4. Y

    Askofu ambomoa Dk. Slaa, amuonya na dhambi ya uzinzi!

    Mkuu, naomba nikuunge mkono, aidha huyo askofu anataka kuuambia umma wa wa-TZ kwamba huko Israel hakuna watu wanaoishi bila kufunga ndoa? Ninamhurumia kwa kujiingiza katika ushabiki wa kisiasa.
  5. Y

    NAJIULIZA... Je ni hali ya Usalama Darfur au Muendelezo wa 'Vita Baridi' ya JK Vs Kagame?

    Mkuu, umeeleza mengi kuhalalisha mawazo yako kuhusu kinachosemekana kuwepo kwa kutokuelewana kwa mhe. JMK, Rais wa TZ na Kiongozi wa Rwanda mhe. Kagame. Binafsi siamini kwamba viongozi hawa wawili hawaelewani, kwa sababu ushauri alioutoa mhe. JMK kuhusu kufanyika kwa mazungumzo ya amani na...
  6. Y

    Uchaguzi Monduli, CHADEMA waambuliwa kuulizwa nyie ni akinanani? Lowassa afanya new style ya siasa

    Mkuu, kiingeredha chako kigumu!! hadi nimetoka kapa, ni cha wilaya gani ya TZ. Kwa nini usingeandika lugha ya Kiswahili ukaeleweka vizuri kuliko hicho ulichokiandika, ni aibu, sijui ni cha wapi?
  7. Y

    Dada Juliana Shonza, haya ni ya kweli?

    Mkuu, pole sana. Unadhani wewe ndiwe uliye sahihi katika Kiswahili? Hapana. Hilo neno "ndio" katika Kiswahili fasaha hutumika kamaanisha kundi au makundi. Hapa ulitakiwa utumie neno "ndiyo nini"?
  8. Y

    Dr slaa ataja matatizo matatu yanayokabili tanzania

    Mkuu, mleta mada ameleta kiushabiki. Kwa bahati mbaya sina huo ushabiki wa vyama. Ila nina kumbu kumbu ya rais wa awamu fulani ambaye alipata kukutana na waziri mkuu mstaafu wa Malaysia (Dr.....). Alipomwuliza kuhusu mbinu walizotumia kupata maendeleo ya kiwango kile akamjibu. Ili muendelee...
  9. Y

    My Apology to JamiiForums, by Chris Lukosi

    Mkuu, samahani hicho kiinglishi kimenipita mbali kwa sana, si unazijua Kayumba Skuli? Lakini ngoja nijaribu kidogo yawezekana Kiswahili hukijui kabisa. Are you a stranger in Tanzanian politics? Haven't recently ever heard about the release of a draft for the new constitution of Tanzania...
  10. Y

    My Apology to JamiiForums, by Chris Lukosi

    Mkuu, mambo mengine ambayo huwa unayaandika huwa yanajikanganya yenyewe. Unasema kushabikia kiingereza ni ulimbukeni, mbona nawe umeandika kichwa cha habari cha uzi wako kwa lugha hiyo hiyo ya kilimbukeni (tena kwa makosa)???!!! Lakini maelezo ya ndani kwa Kiswahili, je kulikuwepo na hiyo haja?
  11. Y

    Vyama hivi vya siasa lazima viathirike, kama rasimu hii itapita.

    Mkuu, ningekuona wewe kuwa ni GT wa JF iwapo uzi wako ungeambatana na mifano halisi ya "wabunge na wagombea urais wa kudumu" wa hicho chama CHADEMA waliopo. Weka mkazo katika "wa kudumu". Hapo ndipo mantiki ilipo.
  12. Y

    HESABU ngumu sana Kwa Wanasiasa

    Mkuu, ni Usovieti upi uliodumu kwa miaka sita?
  13. Y

    HESABU ngumu sana Kwa Wanasiasa

    Mkuu, naomba nikukumbushe kitu. Muungano wa Tanzania unafanana na iliyokuwa Soviet Union (USSR).Kipindi kile Sovereign republics zote zilizokuwa zinaunda Soviet Union zilikuwa na viongozi wa juu na katiba zao isipokuwa Russia. Sababu ilikuwa kwamba Russia ndiye aliyekuwa mhimili ya Soviet Union...
  14. Y

    Kwa rasimu hii, CCM inakufa

    Mkuu, hunijui, sikujui, matusi ya nini?
  15. Y

    Kwa rasimu hii, CCM inakufa

    Mkuu, pamoja na ushabiki wa kivyama, ni ukweli usiopingika kuwa, CCM kama chama tawala kimekuwa mstari wa mbele kupinga wagombea binafsi. Rejea kesi ya Mch. Mtikila dhidi ya Mwanasheria mkuu wa serikali ya TZ, na hukumu yake na nini kilifuatia kuhusu utekelezaji wa hukumu hiyo? Ndiyo maana huyu...
  16. Y

    Kwa rasimu hii, CCM inakufa

    Mkuu, tangu mwanzo wa uzi huu umekuwa ukimshambulia mleta mada. Ni dhahiri kabisa una chuki za kitoto na huyu bwana. Katika kuchangia mada si muhimu kujua nani kaileta, bali inahusu nini. Au ni kanuni ipi ya JF inayosema ili u-post mada ndani yake ni lazima uwe mwandishi wa habari...
  17. Y

    Prof Muhongo ni MUONGO au ANATANIA!!

    Mkuu, hakika ukipenda chongo utaita kengeza! Kweli kwa profesa wa sayansi ya miamba, ambaye vipimo vya urefu ndiyo lugha yake asijue sentimeta ni kitu gani hadi akichukulie kama kipimo cha ukuaji wa uchumi halafu useme eti ulimi umetereza bila kutilia shaka???!!! Hakika TZ haiishi vituko...
  18. Y

    Tanzania haina uhusiano wa kibalozi na Vatican

    Mkuu, hongera kwa kutujuza na hongera kwa kuandika ukweli kwa kujiamini. Sasa na sisi tusioelewa ninaomba utusaidie. Hivi balozi wa TZ, sijui ni nchini au jijini Roma anaitwa Kardinali nani?
  19. Y

    CCM mmeshindwa kulinda tembo wetu hata kiswahili?!

    Ahsante mkuu kwa kunifumbua macho, nilikuwa sijui kuwa Kiingereza ni lugha mahsusi ya TZ. Hata hivyo ninakuomba, ili kunipa uelewa zaidi nielekeze ni wapi pameandikwa na kusisitizwa kama ulivyoandika hapo juu kwenye wekundu. Ni katika katiba ya TZ au ni pahala gani? Tafadhali nielimishe.
  20. Y

    CCM mmeshindwa kulinda tembo wetu hata kiswahili?!

    Ahsante mkuu kwa kunifumbua macho. Nilikuwa sijui kwamba Kiingeeza ni lugha mahsusi ya TZ. Ili kunifumbua zaidi mkuu, ninaomba unielekeze ni wapi pameandikwa hivyo kama ulivyosema hapo kwenye wekundu? Ni katika katiba ya TZ au wapi?
Back
Top Bottom