Habari za siku ,wana jukwaa kwa ujumla
Nina mdogo wangu amesoma Veta na nimeona tangazo kupitia portal ya ajira kuna nafasi ya walimu wa Veta.
Naomba mwenye uelewa wa mishahara ya walimu wa Veta ikoje? Je inafanana na kada za walimu wa shule za msingi au Sekondari?
Nitafutahi kupata uzoefu wa...
Habarini
Nilikuja kutoa matongotongo kidogo Dar na leo ninapoandika ujumbe huu natoka Kariakoo narudi zangu huko ambako hasa ndio tunazalisha chakula.
Nimefika Kariakoo nikasema ngoja nitafute chochote cha kuwabebea watoto,lahaulaaa la kwata!!, Nimeshindwa kuendelea kuzunguka njia zimejaa watu...
Habari za asubuhi wanajamii wenzangu,poleni na hongereni kwa kazi za kujitafutia ridhiki za kila siku.
Nipo hapa leo kuomba msaada kwenu kama mada nilivyoitambulisha hapo juu.
Laptop yangu ilizima ghafla na baada ya kumpelekea fundi aliniambia tatizo lipo kwenye mother body ya laptop hiyo na...
Nawasalimu nyote kwenye ukumbi huu kuhimu sana wa kupashana habari,matukio na ujuzi kutoka kwa wadau waliomo humu ndani.
Mimi ni mwanachama mwenzenu japo si wa muda mrefu sana.
Mimi ni mwajiriwa wa serikali wa muda kiasi ninaomba mchango wa mawazo na ushauri wenu kuhusu kujifunza fani au...
Kichwa kinajieleza labda wahusika wa makampuni ya simu wapo humo watuambie.
Hivi karibuni kampuni kadhaa ikiwemo kampuni ya simu ya Tigo wameongeza bei za vifurushi vya internet.
Changamoto hiyo ipo kwenye muda wa kutumia bundle hizo. Kwanza bundle zinaisha haraka sana, nawauliza tatizo nini...
Nawasalimu wanajamvi wote,hongereni kwa majukumu ya kujenga taifa. Leo nimekuja kwenu kuomba ushauri ni kipino gani kinatumika kupata bei ya ujenzi wa nyumba?
Nimempata fundi aniinulie boma kuanzia msingi hadi kwenye hatua ya lenta,mahesabu yake aliyopiga ni shs 500 KWA tofari moja gharama...
Habari Wana jamvi, nimekuja kwenu kupata suluhisho la tatizo linalosumbua nyumbani kwangu.
Kuna lile tanki la maji taka linalokusunya uchafu kutoka chooni na bafuni ambalo sasa limekuwa kero.
Siku za nyuma niliweka bomba fupi tu na bado bomba halikuwa linatoa harufu lakini kwa siku za usoni...
Niliwahi kuja na hoja ya ujenzi wa nyumba kwa shilingi 25000000/ milioni ishirini na tano kwa Dar na ikaonekana kuwa siwezi kupata nyumba ya kisasa.
Leo nimekuja na wazo la kujenga au kupata nyumba kwa mortgage, utaratibu wa kununua nyumba au kukopa pesa ya nyumba kwa mfumo huohuo na marejesho...
Tafadhali naomba TUPEANE uzoefu kwa wale waliokuwa kwenye mahusiano , lakini mahusiano yao hayakwenda kama walivyotarajia.
Je, mlio vunja uhuano mlikuja KUJUTA baadae? Nini kilikufanya umrudie kama ulimrudia? Je, kwa ambao waliendelea na maisha na kuoa na kuolewa na wengine changamoto gani...
Tafadhali naomba mchango wa mawazo kwa wale wenye uzoefu wa ujenzi wa nyumba za makazi.
Ninataka kujenga nyumba ya vyumba vitatu vyenye sitting, dinning, store na kitchen pamoja na public toilets je gharama ya ujenzi inafika shilingi ngapi kwa nyumba ya kawaida?
Nataka nijenge nyumba walau...
Mimi ni mwanajukwaa mwenzenu japo si wa muda mrefu ila naheshimu Sana jukwaa hili kuwa ni mahali pa kupata maarifa mapya, ushauri kutoka kwa wabobezi.
Kwa kufupisha tu ni kwamba nimekuwa nikijiwekea akiba kidogo kidogo ili walau na mimi muda ukifika nipate japo ka usafiri ka kutembelea...
Habari wanajambo, mimi ni mpenzi kiasi wa kuangalia movie lakini kutokana na majukumu ya hapa na pale sikuwa na muda wa kuangalia.
Kipindi hiki ni cha kukaa nyumbani kutokana na hali halisi ya dunia. Natamani walau kutumia muda huo kukaa na familia kuangalia movie ili walau kupunguza muda wa...
Wadau, naomba msaada wenu kwa wenye uzoefu wa kwenda Singida. Sijawahi kusafiri kwenda mkoa huo na ninataka kusafiri mwanzoni mwa mwezi wa Machi mwaka huu.
Ninaomba kuelekezwa mambo yafuatayo ili niweze kupanga bajeti yangu vizuri.
1. Nauli kutoka Dar hadi Singida Igunga
2. Gharama za malazi...
Wadau naomba kuuliza maana naona Kama makampuni haya yanawaibia wateja.Mimi natumia mtandao was tigo lakini kwa wiki Sasa wamekuwa wakipunguza data Mara baada ya kujiunga hata vifurushi vya internet.Nawaza kuitupa line yangu kwa kuwa waliwahi kuwa na hii tabia na wakaacha na Sasa wameanza tena...
Naomba kufahamu kuhusu kununua bidhaa mtandaoni na kwenda kununua vitu kariakoo ipi ina unafua wa bei na faida inayoridhisha? Hapa namaanisha kununua mzigo mkubwa.
Asanteni kwa muda wenu
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.