Sasa tayari umeshasema kuvaa hirizi ni jambo la kawaida kwenye jamii zetu, why in hell do you need to know Kakobe ameonaje hirizi ya huyo kiongozi? Huoni jinsi ambavyo unajichanganya?
Hivi wewe si juzi juzi tu ulipayuka humu kulaani jarida la The Economist lilipomuita Magufuli "bulldozer"; iweje wewe leo umuite "bully" na "intimidator" na iwe sawa?
Ukweli ukisemwa na wageni ni fedheha ila ukisemwa na wenyeji ni sawa?
Awe amekaangwa au hajakaangwa, awe ametoka kwa sababu za maana au za hovyo the point remains ameamua kuondoka CCM na ameshafanya hivyo.
Haya mengine ni umbea na ufukunyuku tu kwa masuala binafsi ya mtu. It's not gonna put food on your table or pay your next salary.
Ule ugonjwa mkuu duniani kuna stage ukifika huwa unadhuru akili na kumfanya muathirika kuwa na hasira za ajabu ajabu na mihemko sababu ya kuchanganyikiwa.
Hakuna coincidence yoyote, usijenge taswira isiyokuwepo. Jaji Maraga ni muumini wa dhehebu la Wasabato na hata wakati wa usaili wake alisema hatafanya kazi siku ya Jumamosi. Kwenda kusali leo ni kawaida yake hivyo usitafute kuwachota watu akili kirahisirahisi.
Hivi hii dhana ya "Watanzania tunataka maendeleo" mnaitoa wapi? Unaposema unataka maendeleo unamaanisha yatoke wapi ili yaje? Hivi kwa akili zinazofanya kazi (ambazo sidhani kama unazo) unaona kabisa hili ni taifa linaloweza kuendelea? Kwa kukusaidia tu ni kwamba hakuna popote duniani taifa...
Unapoandika habari za Magufuli na utumbo wa CCM yake unatakiwa kutumia jina "Mwenyekiti wa taifa wa CCM" na si Rais, umesikia?
Sitaki kurudia hili suala tena.
Kelele za chura tu kutaka kutokea kwenye vyombo vya habari. Enzi za Dar Mpya mlimsifia hivi hivi sijui leo Dar Mpya imefia wapi. Hii ya leo baada ya wiki mbili hamna atakayeikumbuka wala kuizungumzia na litatafutwa jingine jipya.
Akili zilezile, Bashite wenu yuleyule matokeo tofauti yatoke...
Mleta mada na yule waziri wa viwanda wote mediocre. Kila uzi unaoanzisha unahusu Chadema au unailenga Chadema, vipi kuna kitu unawadai wanakuzungusha kukulipa?
Ni sahihi kwamba nchi ilikuwa na mfumo usiofaa kiuchumi na kimaisha lakini kudai au kuamini kwamba yanayofanyika sasa hivi ni maandalizi ya mambo kuwa sawa ifikapo 2018 ni aina nyingine ya udhaifu wa fikra.
Umewahi kusikia economic strategy yoyote toka kwa Magufuli? Katika mazingira ya namna...
Inaonekana hujaelewa kinachozungumziwa. Swali ni kwamba huo mchanga unaozuiliwa Tanzania hatuwezi kuichakata hiyo 20% ya dhahabu iliyomo kwa sababu hatuna kinu cha kufanyia hivyo.
Sasa jambo la kujiuliza ni kwamba mchanga unazuiliwa halafu ufanyiwe nini?
Tuna tatizo la uzalendo usio na akili...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.