Nimesoma gazeti la Mwananchi la leo tena bila kupepesa macho na kurudia mara tatu juu ya tamko ya Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Bwana Nape Nnauye. Nimegundua kitu kimoja, miaka ya nyuma CCM ilikuwa inatamba kuwa ina Wanachama zaidi 1,000,000 nchini lakini tamko la Bwana Nape Nnauye kwenye...
Heshima mbele wana JF wote,
Ni muda mrefu sana nimekua sipatikani hapa JF. Baadhi yetu wamekuwa mkini PM na kuniuliza Vipi TUMBIRI? Umeng'olewa meno na kucha au?
Kimsingi nimebanwa na shule Wakuu. Lakini leo wakati napita pita huku na huku kutafuta literature za kusapoti Dissertation yangu...
Heshima mbele Wana JF!
Nimesikitika sana na taarifa kwamba timu ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliyokwenda Uholanzi ikiongozwa na Rais Jakaya Mrisho Kikwete amelakiwa wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Uholanzi. Nimesikitika zaidi baada ya kusoma kuwa hata mazungumzo waliyokuwa...
Wakuu wote heshima mbele,
Kama tunavyojua miezi michache ijayo CHADEMA itaingia kwenye kinyang'anyiro cha kuwania Ubunge wa Jimbo la Sumbawanga. Ni muda muafaka tutafakari kwa pamoja na kumshauri Katibu Mkuu wetu Dr. Willbrod Slaa namna atakavyounda timu ya kampeni hususani timu kuu ya kuratibu...
Mhadhiri Mwandamizi wa Uchumi wa Chuo Kikuu cha Mzumbe Dk Honest Ngowi amesema ripoti ya utafiti uliofanyika hivi karibuni uliodhaminiwa na Shirika la nchini Norway (Norwegian Church Aid) imegundua kwamba asilimia 89 ya Watanzania hawalipi kodi kutokana na mfumo uliopo sasa katika ulipaji kodi...
Wanabodi na Moderators heshima mbele,
Wakati harakati za uchaguzi Mkuu nchini marekani zikiendelea, Mpinzani mkubwa wa Barack Obama, Bwana Mitt Romny anakabiliwa na tuhuma nzito kama tuhuma zinazowakabili baadhi ya Viongozi waandamizi wa CCM za kuhifadhi kiasi kikubwa cha fedha nchini Uswiss...
Wakuu heshima mbele kama kawaida,
Walau hadi sasa tunaweza kuandika tofauti za kisiasa kati ya kizazi cha Dotcom na hiki cha SLP. Tofauti hizi ni kama ifuatavyo:-
No
Kizazi cha Dotcom
Kizazi cha S.L.P
(i)
Wengi ni wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)
Wengi ni wafuasi...
Wakuu heshima mbele,
Leo nimetoka kuperezi Facebook Wall ya W. J. Malecela nimekuta amendika hivi "People need your prayer, kesho ninaingia kwenye uchaguzi ninagombea nafasi mbili za kuwakilisha mkoa na saa 1 kesho asubuhi nitakuwa Star Tv Radio kuchambua kwa kina Bunge la Bajeti!! SO NEED YOUR...
Wakuu heshima mbele,
Naomba kuuliza swali moja kwa anaejua. Muhingo Rweyemamu ambaye ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Korogwe hivi karibu na Salvatory Rweyemamu a.k.a Salva ambaye ni Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu ni ndugu?
Maana naona wote ni wanatumia Surname ile ile na wote...
Licha ya kuwa Balozi zetu zimetajwa kwamba ni miongoni mwa pori kubwa la ufisadi wa kodi zetu kulingana na ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za serikali1, natabiri Ndugu Bernard Membe kuendelea kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa kimataifa kutokana na uswahiba kati yake na bwana...
Malaya jela kwa kuuza miil yao
WAKAZI wawili wa Dar es Salaam, wamehukumiwa kifungo cha wiki mbili jela baada ya kukiri shtaka la kufanya biashara ya kuuza miili yao kinyume cha sheria. Washtakiwa hao ni Aisha Nassoro (20) na Upendo Julius (39), wote wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi...
Wakuu heshima mbele,
Nimekuwa nikiisoma Ripoti ya Serikali ya Mdhibiti na Mkaguzi wa hesabu za Serikali ya mwaka wa fedha uliopita (2010/2011) yenye kurusa 216 na nimekuwa pia nikiilinganisha na Taarifa zake za miaka ya fedha iliyopita hususani ya 2008/2009 na 2009/2010.
Katika ripoti ya...
Wanabodi,
Ufuatao ni mchanganuo wa gharama ya safari ya Rais Kikwete huko Brazil. Gharama za posho vimezingatia viwango vya posho kama zinavyoelekeza kwenye waraka wa serikali wa Malipo ya posho Safari kwa Viongozi na Watendaji wa Serikali. Katika mchanganuo huu imekadiriwa gharama ya tiketi ya...
Wakuu,
Tangu jana nimekua nikiisoma ripoti ya Serikali Kuu ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ya mwaka wa fedha 2010/2011 yenye kurasa 191. Nilipofika ukarasa wa 90 nikashtuka kuona baadhi ya wabunge wetu wametajwa kuchukua pesa za Perdiem kwa ajili ya vikao vya Bungeni mjini...
Wakuu,
Leo hapa Dar es Salaam gazeti la Mwanachi halipo kabisa kwenye soko. Nilipomuuliza muuza magazeti mmoja ameniambia ni kwa sababu wanaugomvi na ma-agent (mawakala) ambao wameweka mgomo wa kutolipokea na kulisambaza gazeti hilo kutokana na malipo kiduchu inayotoa gazeti hilo.
Wakuu Wanabodi,
Hapa Dar es Salaam kumekuwa na mlipuko mkubwa wa ugojwa wa macho maarufu kama Red eyes. Hata mimi hapa nilipo kwenye keyboard ninaumwa vibaya mno na natoa taadhari tu msome kwa umakini hii thread nisije nikawaambukiza.
Concern yangu mimi ni kwa nini Serikali imekaaa kimya hadi...
Sielewi tuna sheria gani na kanunu za Uchaguzi. Mfano katika Uchaguzi mdogo unaotarajiwa kufanyika April Mosi katika Jimbo la Arumeru Mashariki, mmoja wa Wagombea amewekewa pingamizi na mgombea mwenzake lakini cha kushangaza wote wemezindua kampeni huku shauri likiwa bado halijatoka.
Kuna haja...
Kuna watu wengi wamekuwa wakihoji kwa nini Waziri wa Afya ajiuzulu? Hata Waziri Mkuu, Mizengo Pinda nae alihoji swali hili wakati akizungumza na Waandishi wa habari hivi majuzi na akaenda mbali kwa kusema Waziri Mponda ni mgeni pale Wizarani na hadly ana kama mwaka mmoja ofisini. Kwa wale ambao...
Wakuu wanaJF, nimekuwa nikiona mara kwa mara mavazi ya Ndugu Nape Nnauye siku za hivi karibuni yakiwa katika rangi ya kijani yaliyoshonwa Kimagwanda.
Binafsi ninavyofahamu vazi la Magwanda katika harakati za kisiasa kwa hapa nchini kwetu liliasisiwa na Freeman Aikael Mbowe wakati wa uchaguzi...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.