Nimrudishie nini Bwana kwa ukarimu wake wote alionitendea? Nitakipokea kikombe cha wokovu na kuitangaza amani ya Bwana kwa neno lake, Zaburi 116:12.
Mungu wangu u mwaminifu sana kwangu hata sasa umenipa makumi mawili matatu hapa kwenye ardhi yako nikiwa timamu na afya tele, ahsante Mungu kwa...
Barabara ya Uhuru kwenye makutano ya mtaa wa Likoma eneo la Kariakoo pembeni ya Benki ya Akiba kuna shimo kubwa lililoachwa na wajenzi wa Barabara ambapo ni zaidi ya mwaka sasa.
Shimo hili ni hatarishi sana kwakuwa hata wauza nguo za kushikilia mikononi wanalizunguka shimo hilo muda wote ikiwa...
Kuna huu utangazaji ulioanzishwa na hii TV ya Mengi tangia vyombo vya habari vilipoambiwa "not to zat extent watch it" habari zake zimekuwa kama za TBC au hata kuizidi! Kama wahusika wamo humu watueleze kama hili ni la dhati kutoka moyoni mwao?
Sidhani hata yeye angeshirikishwa angekubaliana na hili! Au kuna mtakatifu yeyote aliyewahi kuua kisha akawa mtakatifu? tujuze wanazuoni wa kikatoliki tafadhari.
Hivi huyu Shana nani kampa kibali cha kuua? Maana kaua walioiba gari Costa kahama leo tena itv wanataarifu kuuawa waliokuwa guest house wamepumzika eti wanadhaniwa kuwa majambazi.
Tena anajigamba kumpiga risasi zisizo idadi anayesemekana kukimbilia juu ya dari hajatuambia kama naye alikuwa ana...
Kutokana na hali ilivyo nchini mwetu kwa sasa, ni bora mtu yeyote mwenye akili zake timamu akaacha kufanya siasa ili kunusuru maisha yake.
kwakuwa kupigania maslahi ya taifa kwa njia ya siasa kunahusisha kukutana na watu na kuzungumza na watu jambo ambalo limekatazwa kabisa na wanaotumia mabavu...
Nalazimika kuandika haya kuwataadharisha wana wa mageuzi hatari iliyoko mbele yenu. Lakini kabla ya yote napenda ku declare kwamba mimi sio mwanachama wa chama chochote cha siasa hapa nchini ila ni shabiki wa mageuzi.
Hoja yangu inajikita kwenye imani iliyokuwepo kwenye vyama vya siasa kabla...
Jamani Trafiki ebu tuoneeni huruma jamani doh mtatufirisi kama mkiendelea hivi, mnakaa kwenye mataa hasa pale Morocco mnakamata gari za watu kwa kuwabambikia makosa ya kupita taa nyekundu, na mtu asipowapa ya kubrashi viatu mnatwanga ya kwenye hiyo mashine zenu?
Mafuta yameshapanda jamani...
Ndugu Rais,
Tafadhari husika na somo tajwa hapo juu, maana nimeona nikuandikie kupitia jukwaa hili kama hutoisoma wewe lakini naamini vijana wako tulio nao humu watakufikishia ujumbe.
Nakupongeza sana kwa uamzi wako wa kuona suala la usafi wa mazingira na kuzuia kipindupindu ni muhimu na...
Tafadhali sana mkuu wa mkoa wa Dar utoe agizo kwa Halmashauri ya jiji ipambane na maji machafu yanayozagaa kila mtaa wa jiji, najua amri yako ina nguvu kama vile ulivyokomesha wamachinga na bodaboda mjini kwa sababu zinachafua jiji lako.
Picha hizi nimezipiga leo eneo la ofisi za jiji (City...
Wakati taifa linaadhimisha siku ya Mazingira Duniani hii ndio hali halisi ya jiji letu la Dar, japo wakubwa wako Mwanza kula kuku kwa tiketi ya Mazingira hayahaya!
Leo kwenye taarifa za habari tv one na itv yameoneshwa matukio mawili yanayohusisha polisi kuvamia watu, waliotulia na kuanzisha vurugu na kisha kuwajeruhi kwa mabomu ya machozi hata risasi za moto.
La kwanza ni tabora ambapo Dr Hamisi Kigwangwala alikuwa anaongea na raia wake huko tabora...
Ningependa kuuliza , hivi kweli Tanzania kuna wasomi? Na kama wapo je ni viashiria (indicators) gani vya kuonesha kuwa hii nchi ina wasomi tena wengi?
Naomba msinishangae kwakuwa aulizaye ataka kujua jamani, na kwakuwa nijuavyo mimi ni kwamba msomi ni yule anayetumia elimu yake kufanya...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.