Haijalishi leo kuna mvua kiasi gani ni muhimu kutangaza ubingwa haswa na msikasirike jamani ndo mchezo wenyewe huo. Ya kimataifa kialali sasa inasepa hata pembe hamjaiona lo!
NBC bank ni jipu, leo mei mosi lakini hadi sasa pesa za watu mmezikalia pasipo sababu zozote wakati waajiri walishazileta hizo pesa kwenu, Kwanini mnawacheleweshea watu pesa zao wakati ni saving acount, Je mnazifanyia biashara kwanza huku wahusika wanabaki wanapata tabu mtaani? Mchezo wenu huo...
Wakuu na washabiki wa mchezo wa kabumbu tayari wawakilishi wetu wote ambao ni Azam na Yanga wametolewa nje ya kinyang'anyiro haijalishi kwa uzembe au la! kufugwa ni kufungwa maana ufanyapo kosa ndo upenyo wa mpinzani wako anapoponyokea ili kujiweka sawa katika nafasi husiaka. Tufanye nini wakuu...
TFF napenda niwapongeze kwa maandalizi ya mchezo kati ya watani wa jadi Simba vs Yanga kwani mambo mengi yalienda vizuri Isipokuwa napenda niwakumbushe kuhusu swala zima la tiketi kwani kwa kitengo hiki bado hamjakidhi ubora wa mlaji(mashabiki) wanaoingia uwanjani kwa usumbufu wa kadi zao...
Naishi na mke ambae nyumbani wanamtambua ila yeye ninapomwambia twende kwao ili nijitambulishe anakataa na kusema haina haja, yapata miaka miwili sasa swaga ni zilezile.
Nifanyeje; Ushauri tafadhali.
Nimeshuhudia mwanamke anamuadhibu mwanae kama nyoka, kipigo alichopigwa yule mtoto ni ajabu maana inafikia mzazi unamuumiza mtoto wa miaka mitano huu ni ukatili. Wanawake tuwe na upendo kwa wanetu jamani kwani hata sie kama tungelelewa kwa njia hiyo ya kikatili nadhani tusingefika.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.