Wakuu natumaini mu wazima,
Natafuta mashine za kutengeneza vifuko vya plastik vile vinavyofungia ubuyu, barafu, ice cream home made etc kwa anaejua zinapatikana wapi dar na bei anisaidie tafadhali
The secretary usiwe na wasi wasi sio ugonjwa wa kwangu ana mwaka na miezi mitatu sasa haujafunga bado, ingawa alivyokua na miezi mitano hata mimi nilishangaa sana maana utosi ulikua unadunda mpaka naogopa, wakubwa waliniambia kwamba niliruka makaburi wakati mjamzito (huwa siamini local believes...
Wakuu habari,
Nataka nianze ujasiriamali, na ningependa kuuza nguo za mitumba za watoto. Sasa shida sijui mabel ya mitumba yanauzwa wapi dar/kariakoo na ningependa kuuza nguo first quality sio lonya. Naomba mnisaidie mahali naweza pata hiyo mitumba na ikiwezekana na bei
Na hizo pesa ndio zilimpa jeuri ya kumbeba g jumla ilahali akijua ni mume wa mtu. Hata yeye jambawazi tu alikwapua mume wa mwenzie.
Laana inamtafuna sasa
Nimeshtuka hapa utadhani mimi ndio mama wa huyo binti masikini, kabinti kangu kamezaliwa 2001 Mungu tuepushe nilianza kuzembea kusali sasa namrudia Mungu kwa kishindo maana hii ni hatari
Habari zenu wapendwa,
Natumaini wote mu wazima wa afya nawatakia heri ya mwaka mpya wote. Mwenzenu nina tatizo nina mtoto mdogo wa umri wa miezi kumi (10/12), tatizo toka nijifungue kila siku iendayo kwa Mungu nazidi kunenepa sio kwamba nakula sana la hasha mara nyingi jioni sili kabisa...
Pole mpatanishi nimeishi maisha mazuri tu utotoni baba yangu na mama yangu mpaka leo wanazeeka pamoja na wala sijwahi waona wakigombana kama unavyojua wazee wetu wa zamani walikua wanamalizia yao chumbani. Mtoto wangu ingawa baba yake alichukuliwa na nyumba ndogo nakwambia ana maisha mazuri...
Kwa upande wangu ambao niko sawa kimtazamo na darlingtone nilibebewa mume na nyumba ndogo nikiwa na mtoto mmoja wala sina kazi. Nikapambana nikalea mwanangu na nakuhakikishia ana maisha mazuri kuliko wengi wanaoishi na baba na mama zao. Nyumba ndogo akiona anajifaidia baada ya muda huyo mume...
Ndio maana nasema watu hawazungumzii maisha halisi, watoto wa mtaani wengi ni umaskini tu na unakuta huyo omba omba bado anaendelea kuzaa bila kujali hana mume wala hana kazi. Wazazi wangapi wameachana na watoto wanaishi maisha mazuri? Chanzo cha watoto kuwa wa mtaani si nyumba ndogo ni wazazi...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.