Marahaba mwanangu hujakosea kabisa kwa umri huo, aliyesoma nasi alikuwa mdogo kuliko wote darasani kwetu anastaafu 2020 mimi mwezi huu mwishoni naaga serikalini naachia gari za serikali nikajue kununua mafuta sasa [emoji86][emoji3]
Aisee nimeamini watu wanajua kutunga jamani daaa, Siwale tunamfaham in and out bidii yake ya usimamizi wa shule, kulikuwa na nidhamu ya hali ya juu, shule ilikuwa safi mno, kilimo kilikubali sana shule ilijitegemea kwa chakula hapo ndipo alipoanza kupata umaarufu hadi Rais Nyerere akaja kujionea...
Enzi hizo hakukuwepo na haya maswala ya ngono kwa kiasi kikubwa, na heshina ilikuwepo kwa wanafunzi, hivyo watu wazima waliwaheshimu sana watoto na wanafunzi heshima hiyo imetoweka kipindi hiki cha mitandao na tamaa ya pesa.
Hakukuwahi kutokea kiongozi yeyote achukue mwanafunzi pale kwa kweli, na tulifungiwa sana tulikuwa na ruhusa ya kutoka mara moja kwa mwezi kila week end ya mwisho wa mwezi na mwisho wa kuingia shule ni saa 11.30 jioni na si vinginevyo
Nilisoma korogwe girls mwl Siwale akiwa Headmistress wangu, tuliingia pale 1973 Korogwe girls ilikuwa ya mchepuo wa kilimo, Siwale alitulimisha mashamba ambayo kila mmoja alipangiwa plot yake kuanzia mwanafunzi wa kidato cha kwanza hadi cha 6 bila kujali ni mtoto wa kiongozi au wa nani, na pale...
Pole sana kwa machungu uliyo nayo ila waase familia na wanajamii kutotumia vyeti au documents zozote zile za kuchonga au bandia ni kosa sana la kushtakiwa sema hao hao wanaotukanwa walilichukulia simple wakasamehe hapo wote tuliwashukuru masna mdogo wangu nae ni mhanga wa hicho kitu
Mi nakuomba usipoteze muda wa mtoto wakati unatafuta aendelee kusoma alikopangiwa ila kupata serikalini boarding ilikuwa zamani muundo ulishabadilika na sasa hivi hakuna asiyetetea kitumbua chake kila mtu ni muoga ndg yangu kutumbuliwa nakushauri ukaombe apate shule ya kutwa yenye hostel ila...
Zile nzuri zinajaa kuna kiwango maalum cha idadi ya wanafunzi kwa darasa na wakaguzi wa elimu hupita kukagua ukikiuka unafungiwa shule labda uwe streams nyingi ili uwe na wanafunzi wengi ila ndio ufaulu unakuja kuwa hafifu waalim hawatoshi
Hata moro kuna shule nzuri sana za binafsi kama unataka mwanao afanye vizuri hangaika kupata hizo kuna shule inaitwa Lamirium girls wanaufaulu mzuri sana ila kusoma awe na bidii asipofikia wastani wao watamtoa tu
Hawezi kutoka day aingie boarding na sio bonding ndg, sheria hiyo imekuwepo muda mrefu sasa kwa government labda apate shule day lakini zina hostel .vinginevyo mpeleke za binafsi private japo kupata nzuri muda huu umeshachelewa sana
Ukipatwa na jambo ambalo hukulitegemea na likakuumiza utalaani milele hata kama aliyefanya hakukufanyia kwa makusudi, ukweli kutolewa kwa vyeti feki watu wote tuliumia lakini turudi nyuma pia ingeendelea hii tungekuwa na wasomi wa kweli? Au ni walionunua elimu maana ingekuwa mazoea mwisho...
Kwani hiyo iliyopo hapo ya nani vile pole kwa hisia zako kwa usilolijua utalijua baadae saana nakushauri utulie tu huna haja ya kufuatilia hiyo nyumba kwa kuwa wewe siyo mhitaji mwenye kuhitaji atanitafuta
Ninayo nyingine ipo Iringa road near kito hotel ina minazi zaidi ya hiyo na ilishaanza kuliwa uliza watu wa SUA wakusaidie jinsi mmea unavyoweza kustawi eneo ambalo mtu anahisi hauwezi kustawi
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.