Mzee tangia dunia iumbwe, labda mripuko wa volcano, lakini mlima kuporomokea mji na kuufukia usichukulie poa namna hiyo.
Hata kama ni mabomu yatarindima yataishia kuubaraza tu mlima kama huo lakini hayawezi kuuporomoa.
Mkuu siishi kwenye chungu, ninaishi tu mitaani.
Kusikia 'mtaani wapo kibao', unamaanisha jambo hili lipo sana katika jamii yetu, yaani: mwanamke mmoja kuweza kufanya mapenzi ama kuolewa na ndugu wawili wa damu, aidha mtoto na babake au mtu na kaka yake kwa kujua na maisha yakaendelea...
Anza kwanza uchambuzi wa maoni yako mtoa mada.
Kutuacha tujadili wanajamvi halafu wewe upo pembeni unatuzoom ni sawa na kutupia mbwa marapu rapu kisha ukajiweka pembeni kufurahia wanavyoyafakamia.
Ukweli kabisa kutoka moyoni utauexpose kwa mtu tu barabarani asiye mwandani wako?
Tangu dunia ianze kustaarabika haijatokea hivyo hata kwa wahenga.
Utamaduni wa salamu ni mfumo uliowekwa wa kiubinadamu kuonesha upendo na nidhamu, lakini si kwa malengo ya kuelezeana madhila na madhaifu pamoja...
Mkuu unaamini kabisa kuwa binadamu hana chanzo(mwanzo)?
Hii mijadala ya kuumiza ubongo tuwe tunakuja na mpangilio wa rejea pamoja na evidence zake.
Vinginevyo tukubali kutokukubaliana.
Kuna umasikini mkubwa, bora angelikuwa kaleta maendeleo sasa!
Nzega vijijini ni jimbo la mwisho Tz kwa kuunganishiwa miundo mbinu ya maji na umeme.
Tunavyoongea, vibomba na nguzo za umeme ndo wanaanza kutandika.
Kwenye jimbo lake wananchi hawataki kusikia hizo taka taka zake za kilaghai...
Hiyo nadhani inatumika kudistinguish maneno ili msomaji aielewe taarifa kwa usahihi.
Kama ni hivyo, habari hii yote haiwezi kusimuliwa kutokana na wahusika wote kukosa sifa za viwakilishi.
Mfano: mchumba-siyo mchumba kwa sababu bado hawajafika nyumbani na kutambulishana na kisha kutolewa...
Kiuhalisia hii habari siyo halisi kwa vigezo vifuatavyo:
Kutembea na huyo mzee na kisha kuchumbiwa na kijana bila kujua siyo kosa.
Binti kwenda kutambulishwa kwa wazazi na kukuta hawara yake ndiye mkwe, jambo hilo na uchumba huo ungeliishia hapo hapo na thread hii ingeliletwa kwa kichwa cha...
Fikra ni kula tu basi!
Kikitaka kufanyika hiki kwa ajili ya maendeleo pamoja na kesho ya vizazi vijavyo, utasikia hoja za kula kula zinaanza!
WaTz tumegawanyika kimaoni pakubwa sana na ndiyo maana tunatawalika kwa sahani za wali na tisheti.
Kabla ya kukueleza cha kukusaidia, tueleze kwanza, katika hayo maisha yenu ya siku mbili tatu umempenda pigo zake?
Namaanisha namna ambayo wewe unataka mwanamke awe(nje ndani).
Ukileta hilo jibu, mengine yote ni mepesi namna ya kuyaweka sawa na kusaidiana.
Swali ulilouliza ni la utata mno kwa watu wengi kiuhalisia.
Tofauti na dini na madhehebu mengi yalivyo.
Uyahudi unaenda na vyote ulivyouliza na kuvitolea majibu: dini, kabila na tamaduni. ie: kuna wayahudi wa dini lakini rangi, tamaduni na mataifa tofauti.
Kuna wayahudi wa rangi na taifa...
Nimesikiliza, kwa kweli hajui kujieleza.
Si yeye peke yake aliyeshindwa, bali ni viongozi wengi waliosimama kutaka kuokoa jahazi wameshindwa kutafsiri maana na kazi halisi za Tarula ni nini!
Mi sijawahi kufoji mkuu.
Ila ninafahamu kinagaubaga ghushi zilianza mwaka '74, sera ya elimu ya msingi ilipobadilika kupiga marufuku watoto wasirudie wanapofeli darasa la saba.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.